Skip to main content

WAJASIRIAMALI WAOMBA KUPATIWA MBINU UZALISHAJI BIDHAA BORA

 



NA FATMA HAMAD, PEMBA@@@@

WAJASIRIAMALI kisiwani Pemba wameomba kupatiwa elimu ya usarifu wa bidhaa, ili waweze kutengeneza zenye ubora na viwango, ambazo zitauzika katika  soko la ndani na nje ya Pemba.

Wajasiriamali hao walitoa ombi hilo katika mafunzo ya ujuzi wa kidijitali yaliyofanyika kituo cha uwalimu TC Wingwi wilaya ya Micheweni Pemba.

Biamu Omar Mbrouk mwanakikundi cha hapa kazi cha Wingwi, kinachojishughulisha na utengenezaji wa sabuni, mafuta na unga wa mwani, alisema wamekua wakitengeneza bidhaa, ingawa zinashindwa kupata soko, kutokana na kukosa ubora.

Alisema mwani umebainika kuwa ni moja ya dawa inayotibu magonjwa mengi katika mwili wa mwanadamu, hivyo ni vyema kupatiwa elimu, ili wawe wazalishaji bora.

‘’Tunatamani siku moja kuona kwamba, na sisi tunaziuza Tanzania bara na hadi nchi za nje bidhaa zetu, kwani kutatuwezesha kutambulika na pia kuinua uchumi wetu,’’alisema.

Ali Khatib Ali mjasiriamali wa kikundi cha Tumuombe Mola cha Makangale, kinachojishughulisha na ufugaji wa vitango bahari, alisema wanahitaji kupatiwa elimu juu ya usarifu wa mazao, ili kuzalisha kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu.

Alisema kuna utaalamu wa kulima na kuchakata wakati wanapovuna, ingawa bado wanafanya tu, jambo linalopelekea kukosa bei wanayoihitaji.

 ‘’Mukisha kuwavua wanautaalamu wake wa kuwachakata, ingawa sisi hatujui, bali tunawachemsha tu na baadae ndio tunawauza, kikukweli tunahitaji kupewa elimu,’’alishauri.

 Alisema, endapo watapatiwa elimu kutawasaidia kufuga kwa uwelewa, na kupata bei nzuri inayolingana kilimo hicho, ambacho kitawawezesha kujikimu kimaisha.

Nae Abdalla Salim Massoud mwanakikundi cha Ipo sababu, kinachojishughulisha na ukulima wa mwani, alisema wanahitaji kupatiwa elimu ya utengenezaji wa pagi za plastiki, kwa ajili ya kufungia mwani wao, ili waondokane na na changamoto ya uharibifu wa mazingira.

‘’Tunapokata pegi za mikanda au mibura haturuhusiwi, kwani tunaharibu mazingira, hivyo tunahitaji kupatiwa elimu tutengeneze pegi za plastiki, ili tuondokane na usumbufu tulionao sasa,’’alishauri.



Alisema Kampuni ya mwani ya Sea weed Corporation walishawahi kwenda na kufanya utafiti wa kutengeneza pegi hizo, ingawa hadi sasa hawakurudi tena kwa ajili ya kuwaendeleza.

Akifungua mafunzo hayo kwa niaba ya Mratibu wa Fawe Winnifred Yatuma Manawi, Mjumbe wa bodi ya hiyo Zanzibar Biubwa Mohamed Msellem, aliwataka  wajasiriamali hao, kuyatumia mafunzo watakayopewa, ili waweze kuleta mabadiliko.

‘’Nyinyi wajasiriamali ambao mmebahatika kushiriki mafunzo haya, naomba muyachukue na muyafanyie kazi, ili muendeleze vikundi vyenu na muweze kuzalisha kwa mazao kwa wingi,’’alisema.

Alisema lengo la FAWE,  ni kuwakomboa wanawake na vijana kiuchumi, hivyo ni vyema kuhakikisha wanayafanyia kazi, ili wawe wazalishaji na watengenezaji wazuri wa bidhaa.

Mafunzo hayo ya siku mbili kwa vikundi vya wajasiriamali yameandaliwa na Jumuia inayoshughulikia na kutoa masuala ya wanawake na watoto, vijana na watu wenye ulemavu (FAWE)chini ya ufadhili wa UN WOMEN.

         MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...