Skip to main content

VIKUNDI VYA WATU WENYE ULEMAVU, VYAONESHWA NJIA KUHIFADHI FEDHA KIUSALAMA

 


 NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@

MFUMO mpya wa kidigitali utasaida kuhifadhi fedha za vikundi vya kuweka na kukopa vya watu wenye ulemavu kwa usalama zaidi, na kuondokana na kuhifadhi kwenye masanduku kama ilivyo sasa.


Ameyasema hayo Meneja program wa shirikisho la jumuiya za watu wenye ulemavu (SHIJUWAZA) Sophia Azidihery Leghela, alipokuwa akitoa mafunzo ya kuwajengea uwezo vikundi vya watu wenye ulemavu na wawakilishi wao, ukumbi wa Samail Chake chake Pemba.

 


Alisema mfumo mpya wa digital utasaidia watu wenye ulemavu kuhifadhi pesa zao kiusalama zaidi wa kuweka na kukopa, ili kuondosha hofu ya kupotea kwa fedha zao.

 


Alieleza kuwa, lengo la mafunzo hayo ni kujifunza kuhusiana na mfumo wa kuhifadhi, kuweka na kukopa, kwenye vikundi vya kijaluba kwa njia ya digitali kwa watu wenye ulemavu.


"Niwatake mutumie mfumo huu wa kidigitali wa kuweka na kukopa kwa kuhifadhi fedha zenu, ili kuondoka na kutia ndani ya masanduku," alifafanua.


katia hatua nyingine, alieleza kuwa lengo la kuingia kwenye mfumo huo, ni kuhakikisha usalama wa fedha za watu wenye ulemavu wanaimarishwa hali ya kiuchumi na kiustawi.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la jumuiya za watu wenye ulemavu Ali Machano, alisema lengo la kuundwa vikundi hivyo, asili yake ni watu wenye ulemavu pamoja na mjumuisho wao.


Alifafanuwa kuwa asilimia 60 ya vikundi hivyo ni watu wenye ulemavu na asilimia 40 ni walezi, wazazi na watoa huduma kwa watu wenye ulemavu.


Alieleza kuwa ndani ya kikundi cha watu 30, ni lazima watu wenye ulemavu wawe 18 na  wasimamizi wao wawe 12.



"Lengo la vikundi hivi, tumewalenga watu wenye ulemavu kwa asilimia kubwa, hasa kutoka na ulemvu wa aina tofauti ndio tukapendekeza wasaidiwe na wasaidizi wao wa karibu," alifafanua.


Mjumbe wa shirikisho la Jumuiya ya watu wenye ulemavu Aziza Mussa Alawi, alisema watu wenye ulemavu ni watu muhimu, na wamekuwa wakifanya vizuri kutokana vikundi vivyoundwa.


Alfafanuwa kuwa, jamii ielewe kuwaunga mkono watu wenye ulemavu, ili kuondokana na dhana mbaya itayowaharibia maisha yao.


"Ni vizuri kumsaidia mtu mwenye ulemavu kwa kuwaunga mkono na kumsaidia katika miradi  kadhaa ya maendelo," alifafanua.


Aliongezea kuwa mtu mwenye ulemavu anapaswa kuwekwa mbele katika kumuwezesha masuala ya ajira, taaluma, uwezeshaji na afya.



Mradi huo unaendeshwa kwa pamoja na Shijuwaza, Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA, Jumuiaya ya wasioona ZANAB, kwa unafadhiliwa Norway umekuja baada ya mafanikio ya majaribio, kwenye kijaluba kwa miaka  miwili na sasa umeongezwa hadi mitano ijayo.
                 MWISHO

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...