Skip to main content

'ATCL' LAZINDUA SAFARI ZAKE ARDHI YA PEMBA

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

SHIRIKA la Ndege la Tanzania 'ATCL' limerejesha tena huduma zake za usafiri kisiwani Pemba, baada ya miaka 30.

Shirika hilo limekuja kivyengine kisiwani Pemba, maana limeanza na punguzo maalum la nauli, na ili kulijua punguzo hilo, unatakiwa kuzitembeleza ofisi zao zilizopo mjini Chake chake mkabala na Ofisi ya CCM.

Kwa taarifa zaidi soma hapo chini......

WAZIRI wa Uchukuzi wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania Prf: Makame Mbarawa Mnyaa, amesema kuanza kwa safari za Shirika la Ndege la Tanzania ‘ATCL’ kisiwani Pemba, ni eneo jingine la kukifungua kisiwa cha Pemba, kiuchumi, kama ilivyokuwa ahadi ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

 Ameyasema hayo leo August 20, 2025 kwenye uzinduzi wa safari za ndege za shirika hilo, hafla iliyofanyika uwanja wa ndege wa Pemba na kusema zitaanzia baina ya kisiwa hicho, Unguja na Tanzania bara.


Alisema ATCL, sasa litawarahisihia zaidi wananchi wa Pemba, wakiwemo wafanyabiashara, kufika safari zao kwa wakati, ikiwa ni hatua muhimu ya kufikia ndoto zao za kiuchumi.


Alieleza kuwa, ndege hiyo itafanya safari zake mara tatu kwa wiki ndani ya siku za Jumanne, Ijumaa na Jumapili na zitachukuwa abiria kati ya 76 na nyingine hadi 50.


"Niwatake wananchi wa Pemba, muitumie ndege hii kutokana ubora na umathubuti wake na uhakika wa safari zake za kuanzia, hapa Pemba, Unguja, Dar-es Saalan na mikoa mingine kadhaa ya Tanzania," alieleza.


Alifafanua kuwa, ndege hiyo imekuja baada ya utekelezaji wa Ilani ya chama cha Mapinduzi kwa viongozi wa pande zote mbili za Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibari.

 



Aidha, Waziri huyo aliipongeza hatua ya serikali ya kuona sasa inatanua mbawa zake kwa shirika hilo la ndege, jambo linalokuza pato la nchi.




kwa upande wake, Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la ndege Tanzania Peter Ulanga, alisema kupitia shirika hilo,  mwezi Machi mwaka huu, lilizindua safari katika mikoa  ya Mtwara na Iringa na kupitia mji Kinshasha ya Kidemokrasia ya Congo.


Alisema safari hizo ziliweza kupokekewa vizuri sokoni humo, na zaidi ya abiria 320 hutumia Air Tanzania, katika safari zao na wastani wa abiria 370 wakitokea upande wa mkoa wa Mtwara na 500 kwa DR. Congo kila wiki katika vituo hivyo.


Alifafanuwa kuwa, kupitia shirika hilo, wanajivunia mno, kuwepo kwa ndege mpya 15, ambazo zinafanya kazi, pamoja na ile moja maalum kwa ajili ya mizigo.


"Niwajulishe kuwa, katika ndege hizo, saba zimenunuliwa na serikali ya Jamuhuri ya awanu ya sita chini ya uongozi wa Rais Samia, jambo linalotupa ari ya kufanyakazi kwa bidii na hamasa,"alieleza.


Mkuu wa wilaya ya Chake chake Mgeni Khatib Yahya alisema, Pemba ni kisiwa cha kikubwa chenye historia ya kitalii kinachounganisha kivutio cha kiuchumi kama vile fukwe.


Alisema imeweza kufunguka kiuchumi na kuunganishwa sehemu mbali mbali, kutoka nchi na ndani ya Zanzibar, jambalo ambalo kuja kwa ndege hiyo, ni hatua nyingine.


"Tunamshukuru sana Rais wa Zanzibari kwa kukifungua Pemba kiuchumi tena kwa vitendo, kutokana na usafiri huu, utaweza kurahisisha na uchumi kukua kwa kasi," alifafanua.





Aliongeza kuwa, kuwepo kwa ndege hiyo na kuanza safari zake kisiwani humo, italeta maendeleo makubwa kwa wananchi na kurahisisha safari zao mbali mbali.


Ilifahamika kuwa, kampuni hiyo, imefanikiwa kuongeza miinuko, kutoka 20 kwa siku hadi 140 kwa wiki, katika maeno mbali ya ndani ya nje na kuweza kuiunganisha Tanzania na dunia.

 Shirika la Ndege la Tanzania ATCL, lilianzishwa Novemba mwaka 2002, chini ya sheria ya Makampuni ya Tanzania, ambapo lilichukua majukumu ya shirika la zamani la ndege la Tanzania, ATC.



Kwa mujibu wa taarifa za hivi karibuni ATCL linamiliki ndege 16, ikiwemo aina ya Bombardier Dash 8 Q400, Bombardier CS300 (Airbus A220-300) na Boeing 787 Dreamliner.

Aidha inafahamika kua, Julai 2019, ATCL lilizindua safari baina ya Tanzania kwenda Mumbai- India.

Hata hivyo, mwezi Machi 2021, BBC Swahili, iliripoti kuwa, ACTL lilipata hasara ya shilingi bilioni 60, kwa miaka mitano iliyopita, ambapo ni kwa mujibu wa ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali ‘CAG’ ya mwaka 2019/20120.

  MWISHO

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...