Skip to main content

ZSSF: 'MASHEHA WARIPOTINI WANACHAMA WETU WANAOFARIKI KUONDOA UDANGANYIFU'

 


 NA FATMA HAMAD, PEMBA@@@@

MASHEHA wa mkoani wa kusini Pemba, wametakiwa kutoa taarifa kwa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF), endapo kutatokea  kifo cha mwanachama wa mfuko huo katika shehia zao, ili kupunguza udanganyifu hasa katika malipo ya fedha za serikali.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mafao kutoka Mfuko huo Zanzibar, Mussa Yussuf wakati akiwasilisha mada ya dhima ya masheha, katika utoaji wa huduma za ZSSF, kwenye kikao kazi kilichofanyika leo Machi 6, 2025 Tibirinzi Chakechake Pemba.



Alisema kumekuwepo na baadhi ya watu wamekua wakipeleka taairifa za vifo vya jamaa zao  katika mfuko huo, ambazo sio za ukweli, hivyo endapo watapeleka taarifa wataepusha kutokea kwa udanganyifu  huo.

‘’Wamekua wakitujia watu na taarifa za jamaa zao kufariki na kudai mafao yao, lakini tukifanya uchunguzi tunagundua kwamba sio ukweli ni uzushi mtupu, hivyo mtusaidie,’’alisema.


Alifafanua kuwa, endapo Masheha watatoa taarifa na kupeleka vielelezo  sahihi vya marehemu, watasaidia warithi wake kupata mafao yao kwa haraka na kwa wakati.



Akifungua kikao hicho Mkuu wa wilaya ya Mkoani Dk. Hamad Omar Bakar kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Rashid Hadid Rashid, aliwataka  masheha hao kuwa na ushirikiano wa hali ya juu, na ZSSF, ili kufanikisha azma na malengo ya mfuko huo.



‘’Ndugu masheha nyinyi mnadhima kubwa katika Jamii, hivyo ni vyema mkaweka ushirikiano na ZSSF, ili kuona  kila mwanachama anapata mafao yake,’’alisisitiza.

Nao baadhi ya masheha walioshiriki mkutano huo, walisema watahakikisha wanalifanyia kazi agizo hilo, la kuripoti matukio ya vifo yanapotokezea shehiani mwao, ili kuepusha malalamiko kati ya wanachama na ZSSF.





‘’Tunalichkua na Tutahakikisha mabuku  tuliopewa kwa ajili ya kuripoti matukio ya vifo  tunayatumia na tunaripoti kwa  ZSSF,  kwani kutamfanya kila mwanachama, apate stahiki zake,’’alieleza.

Sheha wa Kilindi Nassor Mohamed Khamis, aliomba kwa uongozi wa ZSSF kuzifanyia marekebisho sheria zao, ili sasa masheha nao wawe wanuafaika wa mfuko huo.



Mapema Kaimu Meneja wa ZSSF Pemba Omar Nassib Ramadhan, alisema mfuko daima, umekuwa ukitoa mafao na haki nyingine kwa wakati, pindi mwanachama akitimiza vigezo husika.

MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...