Skip to main content

WAMBAA, CHUMBAGENI KUFANYA MASHINDANI YA QUR-AN MWISHONI MWA MWEZI HUU

 


 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

JUMUIYA ya kuhifadhisha kur-an ya kanda ya Wambaa na Chumbageni wilaya ya Mkoani Pemba, inakushudia kuendesha mashindako ya kanda, mwishoni mwa mwezi huu, na kuwaomba waumini wenye uwezo, kuiunga mkono jumuiya hiyo, kwa ajili ya zawadi za washindi.

Hayo yameelezwa jana na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo ustadhi Hassan Othman Khamis, kwenye mfululizo wa vikao vya maadalizi, vilichofanyika Chumbageni chini ya msaidizi mlezi wao, Abrhaman Mohamed Khamis.

Alisema, tayari Jumuiya hiyo imeshafanya mashindano ya mchujo uliofanyika Machi 1, mwaka huu, hivyo sasa inatoa nafasi kwa kuandaa mashindano makubwa, mwishoni mwa mwezi huu.

Alieleza kuwa, ni nafasi kwa wenye uwezo kushirikiana na Jumuia hiyo, kwa ajili ya kukitangaaza kitabu cha Allah (S.W) kupitia mfumo wa mashindanI kwa wanafunzi.

Mwenyekiti huyo, aliwakumbusha wale wenye nia ya kuungana nao, kuwa mwenye kuchangia jambo jema hasa katika mwezi huu mtukufu wa ramadhan, Muumba ameshahidi malipo makubwa kwa mja wake.

‘’Niwaombe wale wote wenye uwezo wa kifedha au zawadi nyingine kuungana na kamati yangu, ili kuona tunafanikisha mashindani yetu ya tano kwa mwaka huu,’’alieleza.

Akizungumzia juu ya wakaazi wa shehia za Wambaa na Chumbageni, aliwakumbusha kuendelea kuwaunga mkono kama ilivyokuwa kwa mwaka jana, kwani mpango huo sasa wa mashindani utakuwa kila mwaka.

Katibu wa Jumuiya hiyo ustadhi Abdalla Haji Ali, alisema fedha wanazohitaji ili kufanikisha mashindani hayo pamoja na zawadi kwa washindi na washiriki wingine ni shilingi milioni 1.6.

Alifahamisha kuwa, hadi sasa waumini wenyewe wa shehia za Wambaa na Chumbageni wameshachangia shilingi 640,000 jambo ambalo bado nguvu zinahitajika.

Hata hivyo alisema, kamati ndogo iliyoundwa kuratibu mashindani hayo, inaendelea kupita kwa waumini wa makundi mbali mbali, ili kuomba sadaka zao.

‘’Bado kamati yangu ya kuratibu jambo hili, inaendelea kuwatembelea waumini kama wafanyabiashara, wamiliki wa hoteli, masheha na waalimu wa skuli, ili nao kutoa sadaka zao,’’alieleza.

Msaidizi mlezi wa Jumuiya hiyo sheikh Abrhaman Mohamed Khamis, alisema ili kufanikisha mashindano hayo makubwa kwa kanda ya Wambaa na Chumbageni, ni waumini wenyewe kutoa sadaka zao.

‘’Ikiwa waumini wa dini ya kiislamu wataamau kwa moyo wa dhati, tunaweza kufanikisha mashindani haya ya tano, kama tulivyojipangia, na hasa katika eneo la zawadi,’’alisisitiza.

Mjumbe wa Jumuiya hiyo Raya Juma Khamis, alipendekeza kuwa, ni vyema kwa wazazi na walezi kuwaunga mkono watoto wao, hasa katika kuwatunza.

Katika mashindani hayo ya tano kwa mwaka huu, yatashirikisha madrassa saba kutoka Wambaa na Chumbageni, kwa juzuu ya kwanza, pili, tatu, tano, saba, 10, 15 na 20.

Mwisho 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...