Skip to main content

WASTAAFU WATARAJIWA PEMBA WANOLEWA KUYAKABILI MAISHA YA URAIANI

 


NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

WATUMISHI wa umma wanaotarajiwa kustaafu wametakiwa kuwa makini wanapopokea ushauri wa watu mbali mbali, ili waepuke kupoteza fedha nyingi bila ya mafanikio.

Akifungua mafunzo kwa wastaafu hao watarajiwa, leo Machi 5, mwaka 2025 Afisa Mdhamin Ofisi ya Rais Katiba, Sheria Utumishi na Utawala Bora Pemba Halima Khamis Ali alisema, kuna watu wengi watajitokeza kuwapa ushauri wa mambo mbali mbali, hivyo wawe makini katika kuupokea na kuutekeleza.

Alisema kuwa, wastaafu bado wana mchango mkubwa kwa taifa, hivyo kuna haja ya kujipanga mapema katika kujitafutia miradi ambayo itaendeleza maisha yao baada ya kustaafu.



"Kila mtu atakujia kukushauri kufanya biashara na wingine watakushauri kufanya vitu vyingine, lakini muwe makini ili fedha zenu za kiinua mgongo, zitumike kuwakomboa kimaisha na sio kuwasababishia matatizo," alisema Mdhamini huyo.

Aliwataka watumishi hao wayafanyie kazi mafunzo waliyopatiwa, kwani wanakwenda kulitumikia taifa kwa upande mwingine, kutokana na kuwa, bado wana nguvu ya kufanya kazi katika kijiletea maendeleo katika familia zao.

"Tunamchango mkubwa kwa taifa hili, kustaafu sio mwisho wa maisha, maisha lazima yaendelee, hivyo ni lazima tujipange katika kujikomboa kimaisha," alieleza.



Mapema Kaimu Mkurugenzi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Pemba Omar Nasib, alisema lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha wanakuwa pamoja na wastaafu hao, ambapo jukumu lao ni kuhakikisha wanapata mafao yao kwa wakati.

"Tunahakikisha mnapewa mafao stahiki na kwa wakati, ili muweze kuendelea na maisha bila ya usumbufu, hivyo muzingatie mafunzo mtakayopewa kwa maslahi yenu na taifa," alifahamisha Kaimu huyo.

Akiwasilisha mada ya matayarisho ya kustaafu na maisha baada ya kustaafu, muwezeshaji mafunzo ya wastaafu kutoka taasisi ya Uhusiano Tanzania (TIA) Williamson Ferdinand aliwataka kufikiria miradi ambayo itawakwamua kiuchumi kabla ya kustaafu kwani wataweza kujipatia fedha sambamba na kufanya mazoezi.

"Mazoezi ni muhimu kwa sababu ni afya, hivyo utakapoanzisha miradi ya maendeleo basi sio kwamba, utapata pesa tu bali hata magonjwa yatapungua," alisema muwasilishaji huyo.

Mshiriki wa mafunzo hayo Kheri Juma Basha aliwashauri wastaafu hao watarajiwa kujipanga vizuri na kufanya kazi bila ya kujiumiza, ili maisha yaendelee vizuri na yasiwe ni changamoto kwao baada ya kustaafu.

"Jambo la kwanza uzingatie utafanya nini, wakati gani na lengo gani, nje kuna fursa mbali mbali tuzichangamkie tutafanikiwa sana katika haya maisha," alishauri.



Kwa upande wake mshiriki Ali Mohamed Ali aliwaelekeza wenzake kujikita kwenye ufugaji wa nyuki kwani utaweza kuinua kipato chao kwa haraka kutokana na kuwa kila kinachotokana kwa ufugaji huo, ni mali.

"Milioni zako tatu tu unaweza kuwekeza kwenye mradi huu, kila anaehitaji aje nimuelekeze, hakuna kitu kinachotoka kwa nyuki kisiwe na kipato," alisema mshiriki huyo.



Katika mafunzo hayo mada mbali mbali ziliwasilishwa ikiwemo mpango mkakati kabla na baada ya kustaafu, lishe na ulaji unaofaa, msongo wa mawazo, matayarisho na taratibu ya mstaafu pamoja na afya ya akili.

                          MWISHO.


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...