Skip to main content

RC SALAMA: ASEMA JAMBO KUHUSU ZSSF, MASHEHA KASKAZINI PEMBA

  

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@@

MKUU wa mkoa wa kaskazini Pemba, Salama Mbarouk Khatib amesema vikao kazi kwa masheha na watendaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar ‘ZSSF’ vinasaidia kuongeza ushirikiano na ufanisi wa kazi.

Alisema, unapokuwa karibu na ofisi ya tawala za Mikoa ndio umeifikia jamii kwa urahisi, na kiyume chake ni kudhoofisha utendaji kazi ofisi isiyotaka ushirikiano na masheha.

Hayo yameelezwa leo Machi 7, 2025 na Mkuu wa wilaya ya Wete Abdalla Rashid Ali, kupitia hutuba ya Mkuu huyo mkoa, wakati wa ufunguzi wa kikao kazi, cha masheha na watendaji wa ZSSF, kilichofanyika ukumbi wa mikutano Jamhuri Wete.

Alisema, ushirikiano huo ambao ‘ZSSF’ wameuomba ni eneo zuri la utendaji kazi, kwani chanzo cha jamii na kuifikia kwa haraka na wepesi ni uwepo wa masheha.

Alieleza kuwa, kilichofanywa na ‘ZSSF’ kinaashiria umoja na mshikamo katika kufanikisha majukumu ya kila siku, yanayosimamiwa na viongozi wakuu wa nchi.



Alifahamisha kuwa, ndani ya wilaya na mkoa, wamekuwa hawafanikiwa, bila ya kuwatumia masheha katika kazi zao mbali mbali, na hasa ikiwa zinawahusu wanajamii.

‘’Masheha kwetu ndio ‘ingine’ ya kufanikisha kila jambo na ndio maana, wamekuwa wakifanya vyema katika majukumu yetu mbali mbali,’’alifafanua.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa, aliitaka ZSSF kufanya tathmini kila mwishoni mwa mwaka, ili kupata sheha bora na ikiwezekana kupewa motisha, katika kazi zao.

‘’ZSSF ikiwapendeza, ni  vyema sasa mkaangalia uwezekano kila mwaka, masheha na hata wa Zanzibar nzima, mkawa mnawatunza kwa aliyefanya vizuri zaidi,’’alifafanua.

Mapema Kaimu Meneja ‘ZSSF’ Pemba Omar Nassib Ramadhan, alisema lengo la kikao hicho, ni kujenga ushirikiano bain yao na masheha.


Alieleza kuwa, masheha ni nyenzo muhimu katika kufanikisha kazi zao za kila siku, ikiwemo kupunguza udanganyifu wa baadhi ya wanachama wao hasa kwa kesi za ugonjwa na vifo.

‘’Hakuna mwanachama wa ‘ZSSF’ asiyeishi katika shehia moja ama nyingine hapa Zanzibar, na ndio maana sasa tunakuja kwenu, ili kuongeza ushikiriana katika kuligundua hilo,’’alifafanua.

Akiwasilisha mada ya dhima ya masheha kutoa huduma za ‘ZSSF’ Mkuu wa kitengo cha mafao kutoka mfuko huo  Zanzibar, Mussa Yussuf Mussa, alisema hawana wasi wasi na masheha, katika kufanikisha kazi zao.


Alieleza kuwa, masheha walikuwepo kabla ya mwaka 1964, ingawa baadae, walianzishishiwa sheria yao kuanzia mwaka 1998, wakati wa kuasisiwa kwa ZSSF na kutakiwa kushirikiana nao kati kazo zao.

Akitaja mafao yanayotolewa na ‘ZSSF’ alisema ni pamoja na yale ya uzeeni, ulemavu, uzazi kwa wanachama wa mfuko, warithi ambayo hupewa wale warithi wa marehemu ambae hakulipwa mafao ya uzeeni.

‘’Lakini hata mafao ya upotevu wa ajira, kwa wanachama alifanyakazi na kisha kumaliza kazi yake, mfano ujenzi wa barabara, hoteli kwa ambae hakuongezwa mkataba, na bila ya kutokezea uzembe,’’alifafanua.




Kuhusu fidia kwa wanachama, alisema ni kwa yule aliyeumia kazini, mafao ambayo awali yalikuwa yakilipwa na Ustawi wa jamii, ingawa kwa sasa yamehamishiwa ZSSF.

‘’Zipo taasisi tunashirikiana nazo, katika kutoa mafao hayo, mfano ulemavu na uzazi tunashirikiana na wizara ya Afya, ingawa kwa vifo masheha ni watu muhimu kutoa kumbu kumbu zenu,’’alifafanua.

Baadhi ya sheha hao, waliahidi kushirikiana na ZSSF, kwani imekuwa karibu nao, katika kufanikisha majukumu yao ya kila siku.

Mwenyekiti wa masheha wilaya ya Wete Othman Ali Khamis, alisema daftari walilokabidhiwa, kwa ajili ya kumbu kumbu za watumishi wa tasisi binafsi, waliomo shehia mwao, watalifanyia kazi.

Mwisho 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...