Skip to main content

MAFUNZO YA UTUNZAJI WA MISITU YA MIKOKO YAANZA RASMI COMMUNITY FORESTS PEMBA

 



BY MUNIRA KAONEKA, ZANZIBAR@@@@

Katika jitihada za kuimarisha uhifadhi wa mikoko na matumizi endelevu ya rasilimali za asili, Jumuiya ya Community Forests Pemba (CFP) imefungua mafunzo maalum kwa Watoa Mafunzo ya Jamii (ToTs) kuhusu uhifadhi wa mikoko na usimamizi wa rasilimali za jamii. Mafunzo haya, yalifanyika kuanzia tarehe 19 hadi 21 Februari katika ofisi za CFP Unguja, na yalilenga kuwawezesha washiriki kuwa viongozi wa uhifadhi wa mazingira katika jamii zao.

Mafunzo haya yameandaliwa ili kuongeza uelewa wa washiriki kuhusu umuhimu wa mikoko, mbinu za kuhifadhi misitu, na namna ya kushiriki katika usimamizi wa rasilimali za asili kwa njia endelevu. Kupitia mafunzo haya, ToTs watapata ujuzi wa vitendo na mbinu za kufundisha ambazo zitawawezesha kuwa mabalozi wa mabadiliko katika maeneo yao.

Akifungua rasmi mafunzo haya, Mkurugenzi Mtendaji wa CFP alisisitiza kuwa uhifadhi wa mikoko ni jukumu la jamii nzima. “Uhifadhi wa mikoko na urejeshwaji wake ni kazi ya pamoja, na ni muhimu kwa maendeleo endelevu. Tunapaswa kuwa mabalozi wa kulinda rasilimali hizi ” alisema. Pia, aliishukuru jamii kwa kujitolea na kushiriki katika juhudi za uhifadhi wa mazingira.


                                          ToT wa mikoko wakipokea mafunzo darasani

Mafunzo haya yalihusisha jumla ya washiriki 35, wakiwemo wanaume wanne (4) na wanawake 31, huku wanawake wakipewa kipaumbele kwa kuwa mara nyingi wao ndio waathirika wakubwa wa mabadiliko ya tabianchi lakini hawashirikishwi ipasavyo katika maamuzi. Washiriki walitoka katika maeneo ya Unguja Ukuu (17) na Uzi (18). Walichaguliwa kwa ujuzi wao na namna wanavyojitolea kwenye utunzaji wa mikoko, wakiwemo wanachama wa kikundi cha uhifadhi wa mikoko cha Unguja Ukuu, Mikoko ni Urithi Wetu.

Mafunzo haya yaliendeshwa na maafisa wa CFP waliobobea katika uhifadhi wa mikoko, wakiwemo Khadija Abdulrahman Hamdu (Afisa wa Mikoko) na John Ngonyani (Afisa wa CoFMA). Washiriki walipata elimu kuhusu:Umuhimu wa mikoko katika mazingira na jamii, Mbinu za uhifadhi na urejeshwaji wa misitu ya mikoko, matumizi endelevu ya rasilimali za mikoko na changamoto zinazokumba uhifadhi wa mikoko na jinsi ya kuzitatua.

Kwa mujibu wa Afisa wa Mikoko kutoka CFP Khadija Hamdu, “Mafunzo haya yatasaidia katika kuengeza ujuzi na uelewa wa wanajamii katika masuala ya mikoko. Pia yatasaidia katika kupunguza athari zitokanazo na uharibifu wa mikoko.”

Baada ya vipindi vya darasani, washiriki watafanya ziara ya mafunzo kwenye misitu ya mikokoi ili kujifunza kwa vitendo mbinu bora za uhifadhi wa mikoko.

Mafunzo yalikua mazuri na tumejifunza mengi na sasa nina ujasiri wa kufanya yale niliyohitaji kufanya (kwenye utunzaji wa mikoko)”alisemaBi.Rukia Haji Hamisi, mvuvi na mkulima kutoka Uzi

Baada ya mafunzo haya, washiriki wanatarajiwa kuwa viongozi wa uhifadhi wa mikoko katika jamii zao kwa kuelimisha wanajamii kuhusu faida za uhifadhi wa mikoko na jinsi inavyoweza kuwanufaisha kiuchumi, kushiriki katika urejeshwaji wa mikoko kwa kupanda miche mipya, na kuhamasisha ushiriki wa wanawake katika uhifadhi wa misitu kupitia nafasi za uongozi.

 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...