Skip to main content

WATEULE 'EJAT' MWAKA 2023/2024 HAWA HAPA

                                



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Dar es Salaam, Alhamis, Septemba 19, 2024

 MAJAJI saba wa Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT) wamehitimisha kazi ya kutathmini ubora na weledi wa kazi zipatazo 1,135 na kuwateua waandishi wa habari 72 watakaoingia katika kinyang’anyiro cha kumtambua mshindi wa kwanza, wa pili na wa tatu na mshindi wa jumla.

Kati ya waandishi wa habari 72, wanaume ni 45 (sawa na 62.5%) na wanawake 27 (sawa na 37.5%). Kati ya wateule hao, wateule 14 (19%) wanatoka katika runinga; 13 (18%) wanatoka vyombo vya mtandaoni, redio 20 (28%) na wateule 25 (35%) wanatoka kwenye magazeti.

Wateule wamepatikana kwa kukidhi vigezo vya ubora ambavyo ni pamoja na ukweli, usahihi, uanuai, haki, kina, utafiti, ubunifu, uvumbuzi, upekee, uchambuzi, uwajibikaji, ufichuaji maovu, uadilifu, uwasilishaji unaoeleweka na uchunguzi. Ifahamike pia kwamba vigezo maalum vilitumika kuzingatia aina tofauti ya vyombo vya habari kama vile redio, televisheni, magazeti na habari za mitandaoni.

Kabla ya kutaja majina ya wateule hao 72 ni muhimu ifahamike kwamba kinyang’anyiro cha kumtambua mshindi wa kwanza, wa pili na wa tatu na mshindi wa jumla kwa makundi 20 ya kushindaniwa kitakuwa siku ya Jumamosi, tarehe 28 Septemba, 2024 ambapo mgeni rasmi katika siku ya kilele cha kinyang’anyiro atakuwa ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Mabunge Duniani, Dkt Tulia Akson.

Mgeni rasmi ndiye atakayemkabidhi tuzo mshindi wa jumla atakayewapiku kwa umahiri waandishi wengine 71 katika hafla itakayofanyika katika ukumbi wa Aga Khan Daimond Jubilee, Dar es Salaam. Hii itakuwa ni mara ya 15 kutoa tuzo za umahiri wa uandishi wa habari Tanzania.

Moja ya jambo la kipekee katika kilele cha kinyang’anyiro hicho ni pamoja na kusikia kutoka kwa jopo la majaji kuhusu viwango vya uandishi wa habari za magazeti, redio, televisheni na mitandaoni  kwa habari zilizohusu uwekezaji wa kampuni ya DP world katika bandari za Tanzania, habari kuhusu Ngorongoro na wamasai na kuhusu maporomoko ya Hanang.

Jambo la pili la kipekee ni kumshuhudia Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mheshimiwa Jerry Silaa akizindua Jarida la Tuzo na Tuzo magazine ambayo yanajikita kuhamasisha umahiri katika sekta mbalimbali Tanzania na nje ya Tanzania. Kwa kuanzia majarida hayo, moja la Kiswahili na lingine la Kiingereza yatabeba maudhui ya tuzo za umahiri wa uandishi wa habari Tanzania (EJAT).

Moja ya maudhui katika majarida yote mawili ni simulizi ya maisha ya wateule wote. Kazi ya kuandika simulizi hizo inaanza leo, hivyo wateule wote wawe tayari kufikiwa na waandishi wa Jarida la Tuzo wakati wowote kuanzia sasa. Maudhui mengine ni ya wafadhili wa tuzo ambao simulizi zitahusu mchango wao katika kubadilisha maisha ya watu ikiwemo kukuza na kujenga tasnia ya habari.

Aidha ikumbukwe kuwa kwa mara ya kwanza kazi za kihabari kwa EJAT 2023 zimeongezeka hadi 1,135 kutoka kazi 893 za EJAT 2022. EJAT 2020 kazi zilikuwa 396 na EJAT 2021 kazi zilikuwa 608.

Waandishi wa habari wa mkoa wa Dar es Salaam kwa mwaka huu waliongoza kwa kuwasilisha kazi 290, wakifuatiwa na mkoa wa Arusha uliokuwa na kazi 81, Mwanza kazi 74, Iringa ilishika nafasi ya nne kwa kuwa na kazi 72, wakati mkoa wa Mtwara ulishika nafasi ya tano kwa kuwa na kazi 49.  Kwa upande wa Zanzibar, kazi zilizopokelewa ni kutoka Kaskazini Pemba (36) Pemba Kusini (43) na Mjini Magharibi (29).

Dirisha la kupokea kazi za waandishi wa habari lilifunguliwa tangu Novemba 15,  mwaka jana na kufungwa Februari 28, mwaka huu. Kazi ya kuchambua na kutathmini ubora wa kazi za kihabari za mwaka 2023 ilianza tarehe 7 hadi 15 baada ya Naibu msajili wa mahakama kuu, Morogoro, Mheshimiwa Fadhil Mbelwa kuwaapisha majaji.

Jopo la Majaji liliongozwa na Halima Shariff, katibu wake Dkt Egbert Mkoko na majaji wengine wakiwa ni pamoja na Ndugu Mkumbwa Ally, Eshe Muhiddin, Jeniffer Sumi, Halima Msellemu na Absalom Kibanda.

Jopo lilichaguliwa na wakuu wa taasisi za kihabari zinazounda kamati ya maandalizi ya EJAT kwa kuzingatia uadilifu, ujuzi na uzoefu katika uandishi wa habari, uwezo wa kuchambua na kutoa tathmini sahihi, uelewa wa mabadiliko ya kidigitali, uzoefu wa kimataifa au wa kijamii.

Aidha, jopo la majaji lilizingatia uwiano wa kizazi kipya na cha zamani, waliopo kazini na waliostaafu, wabobezi wa maudhui mahsusi, usawa wa kijinsia, uwakilishi wa Zanzibar na Tanzania Bara na uwakilishi wa aina ya vyombo vya habari (magazeti, redio, luninga na  mitandao).

Mbali na Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari, mchakato wa kumtafuta mshindi wa Tuzo ya Maisha ya Mafanikio Katika Uandishi wa Habari (LAJA) 2024 unatarajiwa kuhitimishwa leo na wakuu wa kamati ya maandalizi. Tuzo hii humtambua mwandishi ambaye katika maisha yake ametoa mchango mkubwa katika kuiendeleza tasnia ya habari.

Taasisi zinaounda Kamati ya Maandalizi ni Wakfu wa Vyombo vya Habari (TMF), Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Jukwaa la Wahariri (TEF), HakiElimu, Umoja wa Waandishi wa Habari za Mazingira (JET)Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Umoja wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Sikika, Misa –  Tan  na Twaweza.

Sasa nimalizie kwa kusoma orodha ya wateule wa EJAT 2023 pamoja na vyombo vyao:


NA.JINAJINSIACHOMBOMKOA
1Thomas Masalu LunyaloMMazingira FMMara
2Abdallah Bakari NassoroMNipasheMtwara
3Jacob Mogesi MusendaMThe CitizenDar es Salaam
4Marco MaduhuMShinyanga Press ClubShinyanga
5Salum Vuai IssaMZanzibar LeoZanzibar
6Jackline Victor KuwandaFThe ChanzoDodoma
7Stanslaus LambertMSwahili 360Dar es Salaam
8Zacharia NyamogaMIPC Mkombozi TVIringa
9Irene MwakalingaFTBC1Iringa
10Said Ally SindoMStorm FMGeita
11Joshua StephenMNuktaDar es Salaam
12Samweli MpogoleMHighlands FMMbeya
13Shekha SuleimanFZBCPemba
14Abel KilumbuMDar 24Dar es Salaam
15Khamis MohamedMZanzibar LeoZanzibar
16Abdiel Jumanne SiffiMUFMDar es Salaam
17Julius Maricha MarichaMThe CitizenDar es Salaam
18Eliya SolomonMMwanaspotiDar es Salaam
19Huwaida Nassor Moh’dFAs Salaam FMZanzibar
20Rehema Evance MwaikemaFUTVSimiyu
21Philip Mwihava MwihavaMClouds FMDar es Salaam
22Zourha John MalisaFMwananchiDar es Salaam
23Linus Ananias GamarwaMTBCDodoma
24Catherine SekibahaFPangani FMPangani Tanga
25Herieth MakwettaFMwananchiDar es Salaam
26George HelahelaMMwananchiDar es Salaam
27Esau Ezra Ng’umbiMNukta HabariDar es Salaam
28Benson Eustace JacobMUTVKagera
290Mariamu Ally AbdallahFPangani FMTanga
30Adam Gabriel HhandoMCG FMTabora
31Sanula Renatus AthanasMNipasheDar es Salaam
32Elizabeth Edward KusekwaFMwananchiDar es Salaam
33Pamela Nasphory ChilongolaFMwananchiDar es Salaam
34Rodgers SimonMITVDar es Salaam
35Mukrim Mohamed KhamisMKTV TZ OnlineZanzibar
36Ephrahem Edward BahemuMMwananchiDar es Salaam
37Mkwaji Reuben MasatuFUTVDar es Salaam
38Lukelo Francis HauleMThe ChanzoDar es Salaam
39Benjamin MzingaMITVDar es Salaam
40Dickson Shukran KanyikaMRFANjombe
41Hamisi Makungu HamisiMPangani FMPangani Tanga
42Halfan ChusiMNipasheDar es Salaam
43Kelvin Paul MatandikoMMwananchiDar es Salaam
44Waryoba Musa WaryobaMMontessory TanzaniaMwanza
45Anna Peter  MbuthuFTBCArusha
46Egan SallaMBBCDar es Salaam
47Imma Rashid MbuguniMMajira OnlineDar es Salaam
48Haika E. KimaroFThe CitizenMtwara
49Margareth Msafiri GeddyMTBC SafariDar es Salaam
50Yohana Chance ChalleMMwanaspotiMbeya
51Mgongo Kaitira MafuruMMwananchiMwanza
52Mercy Yasin MbayaFUTVDar es Salaam
53Imani Raphael MakongoroFMwananchiPwani
54Fatma Abdallah ChikaweFUTVDar es Salaam
55Brown Benny MbwawaMWasafi FMMbeya
56Ayoub Stanley NyondoMShamba FMIringa
57Warioba Igombe WariobaMUhuruMara
58Salome Gregory SumbyaFThe CitizenDar es Salaam
59Veronica Natalis MatabaFDW SwahiliArusha
60Saa Mbwana ZumoFPangani FMPangani Tanga
61Said Ali NgambaMUyui FMTabora
62Lugendo MadegeMUFMDar es Salaam
63Anna PotinusFMwananchiMwanza
64Christina MwakangaleFNipasheDar es Salaam
65Rauhiya M ShabanFBomba FMZanzibar
66Hazla Omary QuireFThe Tanzania TimesArusha
67Lucy Patrick SamsonFNuktaDar es Salaam
68Mohamed Hammie RajabuMHabari LeoDar es Salaam
69Amina Deogratias SemagogwaFRadio KwizeraKigoma
70Hellen Nachilongo MkisiFThe CitizenDar es Salaam
71Alfred Bulahya JakubaMDodoma FMDodoma
72Waziri Iddi SukaMTumaini TVDar es Salaam

Hongereni sana kuingia katika kinyang’anyiro cha Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT) 2023.

Ernest S. Sungura

Mwenyekiti

Kamati ya Maandalizi ya EJAT 2023



Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan