Skip to main content

JAMII TOENI USHAHIDI MAHKAMANI KESI ZIPATE HATIA

 



NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

WANAJAMII wametakiwa kuwa makini katika suala la kutoa ushahidi mahakamani, kwani ndio unaoweza kumtia hatiani mshitakiwa au kumuachia huru.

Azungumza na wananchi wa Daya shehia ya Mtambwe Kusini, Hakimu wa Mahakama ya Wilaya Wete Maulid Hamad Ali alisema, ushahidi ni kitu muhimu katika kesi, hivyo kuna haja ya kutoa ushahidi kwa kina pale unapohitajika.

Alisema kuwa, kuna makosa mbali mbali yanayotendeka katika jamii ikiwemo ya udhalilishaji, wizi na madawa ya kulevya, hivyo wasipokuwa makini katika kutoa ushahidi, washtakiwa wataendelea kuachiwa huru huku wanajamii wataendelea kulalamika.

‘’Ushahidi ndo ambao utamtia mshtakiwa hatiani au kuachiwa huru, kwa sababu unaangaliwa uzito wa ushahidi, hivyo tuwe makini tunapokwenda mahakamani kutoa ushahidi,’’ alisema Hakimu huyo.

Aidha aliwataka vijana kuacha kutumia madawa ya kulevya kwani yanasababisha kujiingiza katika mambo maovu ikiwemo kuiba na hatima yake kuishia chuo cha mafunzo.


Alisema kuwa, vijana wanapaswa kujielewa na kujitambua, ili waepukane na mambo yatakayowapeleka pabaya na badala yake wajishughulishe na vitu ambavyo vitawaletea maendeleo yao na taifa.

Kwa upande wake Mratibu kutoka Jumuiya ya Wasaidizi wa Sheria Wilaya ya Wete (WEPO) Rashid Hassan Mshamata aliwataka wazazi kukaa karibu na watoto wao na kuwafuatilia nyenendo zao ili watakapofikwa na matatizo waweze kutambua haraka.

‘’Udhalilishaji upo wa aina nyingi, hivyo endapo pia mnawakaripia watoto pia ni udhalilishaji na hasara yake ni kwamba hata afanyiwe ukatili popote hawezi kukwambia, tuishi nao kirafiki,’’ alieleza.

Akijibu suali la mmoja wa washiriki wa mkutano huo kuhusu suala la mashoga kutochukuliwa hatua, Mratibu huyo alieleza kuwa ni vyema wanajamii wapeleke taarifa kunakohusika na kuwa tayari kutoa ushahidi, kwani ipo sheria inayoruhusu kustakiwa na kutiwa hatiani.

‘’Tatizo lenu nyinyi, wafanyaji na wafanywaji mnawajua lakini mnakaa kimya, baadae mlailamu Serikali kwamba haichukui hatua, je mmewapeleka kwenye vyombo vya sheria wakaachiwa?,’’ alieleza.

Nae Msaidizi wa sheria Said Rashid Hassan akijibu swali katika kutano huo alisema, mwanamke nae anaweza kutiwa hatiani ikiwa amepatika na kosa la kuruhusu, kusaidia ama kushawishi kubakwa kwa mtoto wa kike au hata kuazima sehemu ambayo litafanyika jambo hilo.

Mapema washiriki wa mkutano huo walisema kuwa, kuna haja ya kuwakamata wanaofanya mapenzi ya jinsia moja na kuwashitaki kwani ndio wanaopelekea kuwaharibu watoto wengine katika jamii.


‘’Kwa kweli hao wanaofanya mapenzi ya jinsia moja wanaharibu jamii nzima, wanahitaji kufungwa maisha yao, hapa tutakuwa tumewasaidia watoto wasilawitiwe,’’ alisema Sid Mohamed Hamad mkaazi wa Daya.

Mwananchi Silima Othman Haji wa shehia hiyo aliiomba Serikali kudhibiti madawa ya kulevya yasiingie nchini, ili jamii iwe na maendeleo na kupata taifa lenye vijana imara na wachapa kazi.

                                       MWISHO.      

                                                         

                                

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan