Skip to main content

HIZI HAPA CHANAGAMOTO ZINAZOWAKWAZA WANAWAKE KUTOKUWA VIONGOZI MAJIMBONI

 


NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR

Hali ya wanawake, ikiwa pamoja na kushika nafasi za uongozi zinatafuatiana duniani kutokana na sababu nyingi.

Miongoni mwa hizi sababu ni sera za nchi hizo, sheria, mila, tamaduni na dhana potofu ya kumchukilia mwanamke kama mtu ambaye haki zake kama binaadamu hazistahili kuwa sawa na zile za mwanamume.

Matokeo yake ni kuona wanawake wengi wanakosa haki zao nyingi, ikiwa pamoja na za elimu, urithi , kushika nafasi za uongozi na kuwa na sauti inayosikika na kuheshimika katka kufanya maamuzi.

Ripoti ya mwaka 2018 inayohusu uwiano wa kijinsia ulimwenguni imeweka picha halisi ya haki za wanawake katika siasa, uchumi na elimu ili kuutanabahisha ulimwengu kasoro ziliopo na kuelezea umuhimu wa kufanyika marekebisho.

Hivi sasa ziaonekana zinafanyika jitihada mbalimbali kurekebisha dosari hizi ili kuhakikisha mwanamke, anakuwa ni sehemu ya uongozi, ikiwemo kwenye mambo ya kisiasa kwa vile huko ndiko anapofanyika maamuzi muhimu ya kimaisha, kisiasa na kiuchumi.

Changamto hizi za kila aina zimekuwa zinawarudiasha nyuma kutimiza ndoto zao za kuwa na maisha bora na kuwa na maendeleo kwao wao, familia zao na kwa taifa lao.

Katika kuzizungumzia changamoto hizi, hasa za wanawake wa Zanzibar kushika za kuwa Wawakilishi wa majimbo, Naibu katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Zanzibar Tunu Juma Kondo, alisema jamii  haina elimu ya kutosha na ndio maana ni wanawake wachache wanaojitokeza kutaka nafasi hizo kupitia vyama vya siasa.

Aliwaasa wanawake wenziwe wasibaki kulalamika pembeni, bali wajishirikishe katika vyama vya siasa na jitihada zao ziwasaidie kufungua milango ya kuwaptia uongozi wa majimbo.

Mwanasiasa kutoka chama cha Wananchi (CUF), Nadhira Ali Haji, alisemakwa bahati mbaya  jamii  inamuangalia mwanamke kwa  dharau na hivyo kuona hawezi kuongoza.

Katika uchaguzi mkuu wa miaka miwili iliyopita wapo wanawake walojitokeza kugombea uongozi  kwenye majimbo, lakini kutokana na changamoto zilizowakuta baadhi yao walikata tama ya kuendelea kutaka nafasi hizo za uongozi.

Mtumwa Feiz Said, Naibu Mkurugezi wa Chama cha ADC, alisema amepata changamoto mbalimbali wakati wa kugombea jimbo la Mfenesini katika chaguzi za mwaka 2015 na 2020 .

Hio ni pamoja na vitisho mbalimbali vilioambatana na kupigwa, hali ambayo ilimkatisha tamaa ya kuendelea kugombea uongozi.






 Mdau wa masuala ya wanawake na uongozi, Said Suleiman Ali, alisema moja ya njia itayowasaidia wanawake kupata haki yao ya kuwa viongozi katika majimbo ni kuwa wamojana kujipangia mkakati utaowavusha daraja hili kwa salama.

Miongoni wa maeneo yanayotakiwa kufanyiwa kazi ni la kuepukana na ubaguzi unaotakana na tafauti zao za vyama.

Eneo hili hivi sasa linafanyiwa kazi na tasisi mbali mbali za kitaaluma na kiraia kwa lengo la  kuwainua wanawake kuwa viongozi na moja ya taasisi hizo ni Jumuiya ya Wanasheria wanawake (ZAFELA).

Mratibu wa mradi wa kuwainua wanawake katika uongozi (SWIL), Khamis Ali Rashid, alisema changamoto moja kubwa inayopeleka wanawake kutopata nafasi za uongozi mifumo ya vyama vya siasa.

"  SWIL tulishanya mikutano zaidi ya 100 kwa lengo la kuwasaidia wanawake, kuweza kuwatatulia changamoto hizo,’’alisema.

Mmoja wa wanasiasa ambae hakuta jina lake litajwe alipendekeza  ofsi ya msajili wa vyama vya siasa sasa iweke sheria inayolazimisha mfumo wa uongozi wa juu wa chama uwendane na usawa wa kijinsiaKwa mfano, Mwenyekiti akiwa mwanamume Katibu wa chama awe mwanamke..

Ofisa kutoka Idara ya Maendeleo ya Vijana Zanzibar, Suhaila Abdallah Saleh, alisema  wanajikita katika harakati zitazopeleka wanawake kujpatia nafasi zaidi za uongozi.

"Tunawashajihisha kwa kuwapa elimu, ikiwemo juu ya kuzingatia ushiriki wa wanawake na kuwajengea uthubutu watoto wa kike ili wafikie malengo yao," aliongeza.

Mwanasheria wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa Zanzibar, Fatma Haji Mohamed, alisema wnatumia njia tafauti ambazo zitawasaidia wanawake kuondokana na changamoto zinazowakabili.

" Sheria ya vyama vya siasa Zanzibar ni ya muda mrefu na sasa hivi Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amelekeza pafanyike taratibu za kurekebisha sheria mbalimbali za vyama vya siasa,’’alisema.

Mwaka jana vikao vya Kikosi kazi vilipokea malalamiko ya wanawake ya kuwepo nafasi finzu kwa wanawake  kushiriki katika nafasi za uongozi katika vyama na hatimaye ndani ya serikali.

Mkurugezi wa Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Thabit Idarous Faina, alisema katika  majimbo 50 ya Wawakilishi wa kuchaguliwa wanawake ni wanane tu.

Anasema wabunge wanawake wanaowakilisha Zanzibar ni wanne tu, sawana asilimia 8, huku mawaziri wakiwa sita, sawa na asilimia 33 na makatibu wakuu ni saba, sawa na asilimia 39.

Kwa upande wa wakuu wa mikoa, mwanamke ni moja tu , swa na asilimia 20, wakuu wa wilaya ni wanane, sawa na asilimia 36 na masheha wanawake ni 68, sawa na asilimia 17 kwa masheha wote ambao ni 389.

 

Mwisho


Comments