Skip to main content

HIZI HAPA CHANAGAMOTO ZINAZOWAKWAZA WANAWAKE KUTOKUWA VIONGOZI MAJIMBONI

 


NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR

Hali ya wanawake, ikiwa pamoja na kushika nafasi za uongozi zinatafuatiana duniani kutokana na sababu nyingi.

Miongoni mwa hizi sababu ni sera za nchi hizo, sheria, mila, tamaduni na dhana potofu ya kumchukilia mwanamke kama mtu ambaye haki zake kama binaadamu hazistahili kuwa sawa na zile za mwanamume.

Matokeo yake ni kuona wanawake wengi wanakosa haki zao nyingi, ikiwa pamoja na za elimu, urithi , kushika nafasi za uongozi na kuwa na sauti inayosikika na kuheshimika katka kufanya maamuzi.

Ripoti ya mwaka 2018 inayohusu uwiano wa kijinsia ulimwenguni imeweka picha halisi ya haki za wanawake katika siasa, uchumi na elimu ili kuutanabahisha ulimwengu kasoro ziliopo na kuelezea umuhimu wa kufanyika marekebisho.

Hivi sasa ziaonekana zinafanyika jitihada mbalimbali kurekebisha dosari hizi ili kuhakikisha mwanamke, anakuwa ni sehemu ya uongozi, ikiwemo kwenye mambo ya kisiasa kwa vile huko ndiko anapofanyika maamuzi muhimu ya kimaisha, kisiasa na kiuchumi.

Changamto hizi za kila aina zimekuwa zinawarudiasha nyuma kutimiza ndoto zao za kuwa na maisha bora na kuwa na maendeleo kwao wao, familia zao na kwa taifa lao.

Katika kuzizungumzia changamoto hizi, hasa za wanawake wa Zanzibar kushika za kuwa Wawakilishi wa majimbo, Naibu katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Zanzibar Tunu Juma Kondo, alisema jamii  haina elimu ya kutosha na ndio maana ni wanawake wachache wanaojitokeza kutaka nafasi hizo kupitia vyama vya siasa.

Aliwaasa wanawake wenziwe wasibaki kulalamika pembeni, bali wajishirikishe katika vyama vya siasa na jitihada zao ziwasaidie kufungua milango ya kuwaptia uongozi wa majimbo.

Mwanasiasa kutoka chama cha Wananchi (CUF), Nadhira Ali Haji, alisemakwa bahati mbaya  jamii  inamuangalia mwanamke kwa  dharau na hivyo kuona hawezi kuongoza.

Katika uchaguzi mkuu wa miaka miwili iliyopita wapo wanawake walojitokeza kugombea uongozi  kwenye majimbo, lakini kutokana na changamoto zilizowakuta baadhi yao walikata tama ya kuendelea kutaka nafasi hizo za uongozi.

Mtumwa Feiz Said, Naibu Mkurugezi wa Chama cha ADC, alisema amepata changamoto mbalimbali wakati wa kugombea jimbo la Mfenesini katika chaguzi za mwaka 2015 na 2020 .

Hio ni pamoja na vitisho mbalimbali vilioambatana na kupigwa, hali ambayo ilimkatisha tamaa ya kuendelea kugombea uongozi.






 Mdau wa masuala ya wanawake na uongozi, Said Suleiman Ali, alisema moja ya njia itayowasaidia wanawake kupata haki yao ya kuwa viongozi katika majimbo ni kuwa wamojana kujipangia mkakati utaowavusha daraja hili kwa salama.

Miongoni wa maeneo yanayotakiwa kufanyiwa kazi ni la kuepukana na ubaguzi unaotakana na tafauti zao za vyama.

Eneo hili hivi sasa linafanyiwa kazi na tasisi mbali mbali za kitaaluma na kiraia kwa lengo la  kuwainua wanawake kuwa viongozi na moja ya taasisi hizo ni Jumuiya ya Wanasheria wanawake (ZAFELA).

Mratibu wa mradi wa kuwainua wanawake katika uongozi (SWIL), Khamis Ali Rashid, alisema changamoto moja kubwa inayopeleka wanawake kutopata nafasi za uongozi mifumo ya vyama vya siasa.

"  SWIL tulishanya mikutano zaidi ya 100 kwa lengo la kuwasaidia wanawake, kuweza kuwatatulia changamoto hizo,’’alisema.

Mmoja wa wanasiasa ambae hakuta jina lake litajwe alipendekeza  ofsi ya msajili wa vyama vya siasa sasa iweke sheria inayolazimisha mfumo wa uongozi wa juu wa chama uwendane na usawa wa kijinsiaKwa mfano, Mwenyekiti akiwa mwanamume Katibu wa chama awe mwanamke..

Ofisa kutoka Idara ya Maendeleo ya Vijana Zanzibar, Suhaila Abdallah Saleh, alisema  wanajikita katika harakati zitazopeleka wanawake kujpatia nafasi zaidi za uongozi.

"Tunawashajihisha kwa kuwapa elimu, ikiwemo juu ya kuzingatia ushiriki wa wanawake na kuwajengea uthubutu watoto wa kike ili wafikie malengo yao," aliongeza.

Mwanasheria wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa Zanzibar, Fatma Haji Mohamed, alisema wnatumia njia tafauti ambazo zitawasaidia wanawake kuondokana na changamoto zinazowakabili.

" Sheria ya vyama vya siasa Zanzibar ni ya muda mrefu na sasa hivi Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amelekeza pafanyike taratibu za kurekebisha sheria mbalimbali za vyama vya siasa,’’alisema.

Mwaka jana vikao vya Kikosi kazi vilipokea malalamiko ya wanawake ya kuwepo nafasi finzu kwa wanawake  kushiriki katika nafasi za uongozi katika vyama na hatimaye ndani ya serikali.

Mkurugezi wa Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Thabit Idarous Faina, alisema katika  majimbo 50 ya Wawakilishi wa kuchaguliwa wanawake ni wanane tu.

Anasema wabunge wanawake wanaowakilisha Zanzibar ni wanne tu, sawana asilimia 8, huku mawaziri wakiwa sita, sawa na asilimia 33 na makatibu wakuu ni saba, sawa na asilimia 39.

Kwa upande wa wakuu wa mikoa, mwanamke ni moja tu , swa na asilimia 20, wakuu wa wilaya ni wanane, sawa na asilimia 36 na masheha wanawake ni 68, sawa na asilimia 17 kwa masheha wote ambao ni 389.

 

Mwisho


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch