Skip to main content

WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII ZANZIBAR KUSHIRIKI MKUTANO WA 'MMMAM'

 





Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inarajiwa kuwa mdau katika Mkutano wa Kimataifa wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (MMMAM) unayotarajiwa kufanyika Mwezi Machi mwaka huu, jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Akizungumza ofisini kwake Kinazini Unguja na Viongozi kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum bi Abeida Rashid Abdallah amesema Wizara hiyo imefanya jambo jema kuishirikisha Wizara yake kuwa mdau katika mkutano huo unaotarajiwa kufanyika tarehe 11-14 Machi 2024 Katika ukumbi  wa Kimataifa ya Mwalimu Julius Nyerere.

Amesema ni wazi kwamba Serikali zote mbili, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na Jamhuri ya Mungano wa Tanzania (SMT) kwa pamoja zinalengo la kuisaidia jamii katika Malezi, Makuzi, na Maendeleo ya Mtoto. Kwani mtoto ndio tegemeo la taifa la kesho.

Aidha bi Abeida ameshauri katika mkutano huo ni vyema kuwashirikisha na Wizara zingine za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ikiwemo Wizara Afya, Elimu na Mafunzo ya Amali kwani Wizara hizo pia ni wadau katika masula ya mtoto.

Pia Katibu Mkuu Abeida amemshukuru  Wiziri ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Doroth Gwajima na katibu Mkuu wake Dkt Seif  Shekalaghe kwa namna wanavyoshirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (SMZ) katika mambo mengi ya Kiutendaji.

“ Kupitia mashiriano hayo Wizara yetu inapata mambo mengi yakuiga kwani Wizara yetu imezaliwa upya, yapo mengine hatuwezi kuiga kwasababu hayatekeleziki kutokana na nature ya mazingira yetu huwa tunaachana nayo, ila tunawashukuru sana kwa mashirikiano yao kwetu” Alisema Abeida.

Hivyo  bi Abeida amewataka maafisa wa tendaji wa pande zote mbili kuendeleza vikao vya mashirikiano kwani vikao hivyo ni muhimu na vinazaa matunda ya maendeleo kwa wananchi.

Naye Mkurugenzi Idara ya Mtoto kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum bw. Mathias Mgimbe Haule amesema  kupitia mkutano huyo uaotarajiwa kufanyika Machi kutawasilishwa mada mbali mbali zinazohusiana na Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Mtoto kwani wadau wameshaanza kutuma stakabadhi za kuwasilisha.

Pia amesema Wizara yake inatarajia kuanzisha Madawati ya Watoto ambapo yamelenga kutoa elimu kwa Watoto ili wawezi kujilinda pamoja na kutoa taarifa za vitendo vya ukatili wa kinjisia na udhalilishaji.

Mapema Mshauri elekezi wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto bw. Godwin Emil Mongi ameleza kwamba Mkutano wa Kimataifa wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (MMMAM) unayotarajiwa kufanyiaka Mwezi machi mwaka huu ni mkutano wa kwanza kwa Afrika Mashariki.

Aidha alifahamishwa kwamba hadi sasa maandalizi ya mkutano huo yanaendelea vizuri na utarajiwa kuwa washiriki zaidi ya 1500 kwani hadi sasa wadau waliyojisajili wameshafikia idadi ya 1200. Hivyo ametoa wito kwa wadau wengi kujisajili kabla ya muda wa usajili kumalizika.

 

Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch