Wizara
ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inarajiwa kuwa mdau katika Mkutano wa Kimataifa wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya
Mtoto (MMMAM) unayotarajiwa
kufanyika Mwezi Machi mwaka huu, jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Akizungumza
ofisini kwake Kinazini Unguja na Viongozi kutoka Wizara
ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum bi
Abeida Rashid Abdallah amesema Wizara hiyo
imefanya jambo jema kuishirikisha
Wizara yake kuwa mdau katika mkutano huo unaotarajiwa kufanyika tarehe 11-14
Machi 2024 Katika ukumbi wa Kimataifa ya
Mwalimu Julius Nyerere.
Amesema ni wazi kwamba Serikali zote mbili, Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar (SMZ) na
Jamhuri ya Mungano wa Tanzania (SMT) kwa
pamoja zinalengo la kuisaidia jamii katika Malezi,
Makuzi, na Maendeleo ya Mtoto.
Kwani mtoto ndio tegemeo la taifa la kesho.
Aidha
bi Abeida ameshauri katika mkutano huo ni vyema kuwashirikisha na Wizara
zingine za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ikiwemo Wizara Afya, Elimu na Mafunzo
ya Amali kwani Wizara hizo pia ni wadau katika masula ya mtoto.
Pia
Katibu Mkuu Abeida amemshukuru Wiziri ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi
Maalum Mhe. Dkt. Doroth Gwajima na katibu Mkuu wake Dkt Seif Shekalaghe kwa namna wanavyoshirikiana na
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (SMZ) katika mambo mengi
ya Kiutendaji.
“
Kupitia mashiriano hayo Wizara yetu inapata mambo mengi yakuiga kwani Wizara
yetu imezaliwa upya, yapo mengine hatuwezi kuiga kwasababu hayatekeleziki
kutokana na nature ya mazingira yetu huwa tunaachana nayo, ila tunawashukuru
sana kwa mashirikiano yao kwetu” Alisema Abeida.
Hivyo
bi Abeida amewataka maafisa wa tendaji
wa pande zote mbili kuendeleza vikao vya mashirikiano kwani vikao hivyo ni
muhimu na vinazaa matunda ya maendeleo kwa wananchi.
Naye
Mkurugenzi Idara ya Mtoto kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake
na Makundi Maalum bw. Mathias Mgimbe Haule amesema kupitia mkutano huyo uaotarajiwa kufanyika
Machi kutawasilishwa mada mbali mbali zinazohusiana na Malezi, Makuzi na
Maendeleo ya Mtoto kwani wadau wameshaanza kutuma stakabadhi za kuwasilisha.
Pia
amesema Wizara yake inatarajia kuanzisha Madawati ya Watoto ambapo yamelenga
kutoa elimu kwa Watoto ili wawezi kujilinda pamoja na kutoa taarifa za vitendo
vya ukatili wa kinjisia na udhalilishaji.
Mapema
Mshauri elekezi wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto bw. Godwin
Emil Mongi ameleza kwamba Mkutano wa Kimataifa wa Malezi, Makuzi na Maendeleo
ya Awali ya Mtoto (MMMAM) unayotarajiwa kufanyiaka Mwezi machi mwaka huu ni
mkutano wa kwanza kwa Afrika Mashariki.
Aidha
alifahamishwa kwamba hadi sasa maandalizi ya mkutano huo yanaendelea vizuri na
utarajiwa kuwa washiriki zaidi ya 1500 kwani hadi sasa wadau waliyojisajili
wameshafikia idadi ya 1200. Hivyo ametoa wito kwa wadau wengi kujisajili kabla
ya muda wa usajili kumalizika.
Mwisho
Comments
Post a Comment