Skip to main content

WANAOKULA DAWA KWA KUJIKADIRIA WENYEWE WAJICHIMBIA KABURI TARATIBU

 

 


NA MOZA SHAABAN, ZU@@@@

KILA siku mwanadamu amekuwa akihangaikia afya yake na ustawi wake.

Kwa karne zilizopita, mwanadamu alitumia mimea, mboga mboga na wanyama, ili kuponya magonjwa na maradhi mbali mbali yaliokua yakimsibu.

Kwa vile wakati haugandi, sayansi inayochunguza faida na athari za vitu vya kemikali, kwa matibabu au kuzuia magonjwa, kupunguza maumivu na nyenginezo ilizuka.

Na hapa dawa mbali mbali ambazo ni muhimu kwa matumizi ya binaadamu, zilianza kutengenezwa hususan zile za kemikali, ili kurekebisha au kuboresha hali ya afya ya mtu.

DAWA NI NINI ?

Dawa za binaadamu ni kitu chochote, ambacho binaadamu anatumia kwa lengo la kutibu au kukinga maradhi yasishambulie kinga za mwili.

Zinaweza kuwa katika aina tofauti, kama vile vidonge, sindano, matone, creams au loshan pamoja na za unga unga.

Kwa mfano, dawa za antibiotics hutumiwa kutibu maambukizi ya bakteria, za antiviras hutumiwa kutibu maambukizi ya virusi, na dawa za analgesic hutumiwa kupunguza maumivu.

Kitaalamu dawa haziliwi tu kama njugu, bali kuna matumizi sahihi ambayo mugonja, anatakiwa kuyajua, na sio rahisi kujua bila kupata maelekezo kutoka mtaalamu wa afya.

 Kwa lugha nyepesi, Ili dawa ifanye kazi mwilini, ina kiwango maalumu (dozi) na muda wa matumizi yake, iliyoandikiwa mgonjwa kutumia baada ya daktari kuthibitisha ugonjwa uliopo.

Lakini kwa sababu moja au nyingine wapo watu hutumia dawa  bila maelekezo ya daktari, na hili limekua kama jambo la kawaida tu,kwani  watu wengi humeza dawa  bila kuzingatia vipimo.

JE JAMII INAMTAZAMO GANI ?

Hamdu Hassan Bakari (65) wa Mjimbini, anasema udhibiti mdogo wa dawa, ni miongoni mwa sababu zinazo pelekea watu kutumia dawa bila maelekezo ya daktari.

Anasema hakuna udhibiti wa kutosha juu ya upatikanaji wa dawa, na kwa sasa mtu anapojisikia kuumwa, hubisha hodi kwenye maduka ya kuuzia dawa na kununua atakayo.

‘’Baadhi ya maduka ya vyakula yanajihusisha na uuzaji wa dawa kama za antibayotiki (panadoli), ambapo wao hawana usajili rasmi wa kufanya biashara hiyo,’’anaeleza.

Abdull-hamid Shaabani Haji mkaazi wa Vitongoji Chake chake Pemba  anasema, kutokumudu gharama za matibabu, ni moja kati sababu zinazo pelekea, watu wengi  kutumia dawa bila kupata maelekezo ya daktari.

Rehema Mohamed Makame (45), mkaazi wa Mtambile Mkoani, anaeleza kuwa, usumbufu wanaopata wagonjwa katika baadhi ya hospitali na vituo vya afya, unapelekea watu kutofika hospitalini, ili kueleza magonjwa yanayowasibu, na kasha kujikadiria dawa.



 ‘’Utamaduni mbovu wa kila mgonjwa kujikadiria dawa, umekuwa ukiathiri kinga za mwili, na kusababisha baadhi ya wakati, dawa nyingine kutofanyakazi mwilini,’’anaeleza.

Hata Sada Mohamed Amour, wa Mjimbini anafafanua kuwa,  waliowengi wamekuwa wakitumia dawa kiholela kwa kule kutokujua madhara ndani ya miili yao.

‘’Watu wengi hawana uwelewa wa kutosha kuhusu madhara yanayoweza kujitokeza, iwapo watatumia dawa kiholela bila yakupata maelekezo kutoka kwa wahudumu wa afya,’’anaeleza.

WATAALAMU WA AFYA YA BINADAMU WANASEMAJE?

Rashid Suleiman Ali ambae ni Afisa tabibu kutoka kituo cha afya Kangani Mkoani nasema, athari moja wapo anayoweza kuipata mtu, anaetumia dawa kiholela ni kusababisha usugu wa dawa mwilini mwake ‘Resistance of Drugs’ hapo baadae.

Yussuf Omar Masoud daktari  kutoka kituo cha afya Kangani anafafanua kuwa, utumiaji dawa kiholela uaweza kusababisha madhara ya muda mrefu, ikiwemo viungo kupoteza nguvu

‘’Kwa mfano, matumizi ya dawa za usingizi ‘sleeping pills’ ukivitumia bila kufuata maelekezo ya mtaalamu, mwisho wa siku, unaweza kupata ulemavu usiotarajiwa,’’anafafanua.

Nae Maryam Said Abdallah Mfamasia kutoka kituo cha afya cha Buguruni Dar-es-salaam anasema, kutumia dawa bila kufuata maelekezo ya daktari kunaweza kusababisha kuongeza sumu mwilini.

Kwani anabainisha kuwa, dawa hutengenezwa kwa kutumia chembe chembe za kemikali, ambazo kimsingi ni sumu zinazoua vimelea vya ugonjwa, ingawa kwa utaratibu maalum kutoka kwa mtaalamu.

‘’Dawa ni sumu, iliyotengenezwa maalum kwa ajili ya kuua vimelea vya maradhi, ingawa ukiitumia kiholela, inaua hata mtu mwenyewe kwa kule kukosa mpangilio wa kitaalamu,’’anafafanua.

BARAZA LA FAMASIA LINASEMAJE?

Elizabeth Shekalage ambae ni Msajili wa Baraza la Famasia nchini , anaeleza kuwa, madhara ya kutumia dawa kiholela ni pamoja na kuleta ulemavu wa kudumu na hata kusababisha kifo.

Kwani ili dawa ifanyekazi mwilini, inakiwango maalumu (dozi) na muda wa matumizi wa dawa, aliyoandikiwa mgonjwa, kutumia baada ya daktari kuthibitisha ugonjwa uliopo.

Aidha mtaalamu huyo, anasema kuwa, kwa dozi ikiwa kubwa, kunasababisha kuongeza kiwango cha dawa, ambacho hakitakiwi kwenye mwili na huleta madhara ya figo, ulemavu na hata kifo.

MITANDAO YA KIJAMII

 Shirika la Afya Duniani (WHO) limetahadharisha kua, ipo hatari ya idadi kubwa zaidi ya watu kupoteza maisha, kutokana na usugu wa vimelea vya magonjwa aliyetumia dawa holela.

 WHO kwenye utafiti wake wa mwaka 2019, limekugundua kuwa, magonjwa sugu dhidi ya dawa, husababisha vifo laki 7 duniani kote kila mwaka.

Ambapo kwa idadi ya vifo hivyo, ni sawa na wastani wa vifo 58,333 kwa mwezi, sawa na vifo 1,944 kwa siku, huku WHO, likiendelea kutahadharisha juu ya ulaji wa dawa kiholela.

 Aidha WHO, limeonya kuwa, ikiwa mikakati haitochukuliwa ya kudhibiti watu kujilia dawa ovyo, huwenda ifikapo mwaka 2050, watu milioni 10, ikawa wanapoteza uhai kila mwaka duniani kote.

NINI KIFANYIKE?

Hemed Nassor Mbarouk mkaazi wa Mjimbini Mkoani, anasema ni vyema kwa wizara ya Afya Zanzibar, kutoa elimu kwa wananchi, juu ya athari za matumizi ya dawa kiholela.



 Ali Mohamed Makame mkaazi wa Mtambile, anashauri ni vyema kwa wataalamu wa afya, kuimarisha huduma za afya vituoni na hospitalini ili kupunguza tatizo hilo.

Salama Omar Ali mkaazi wa Mchanga mdogo, anashauri kuwa, wizara ya afya Zanzibar, idhibiti uuzwaji dawa kiholela madukani, ili kuhakikisha matumizi ya dawa yanakuwa sahihi kwa mgonjwa.

Rashid Suleiman Ali Afisa tabibu wa kituo cha afya Kangani alisema, ni vyema kwa wagonjwa kufika katika vituo vya afya, ili kupata vipimo na maelekezo sahihi ya madaktari namna ya utumiaji wa dawa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Wazee na Watoto Tanzania bara Dk. Seif Shekalage alisema, ili kudhibiti athari zinazoweza kujitokeza, ni vyema kwa wamiliki wa maduka ya dawa, wafuate utaratibu sahihi wa utowaji wa dawa kwa wagonjwa.

Afisa Mdhamini wizara ya Afya Pemba, Khamis Bilali Ali, anasema ni kosa la kitabibu mgonjwa kujikadiria dawa mwenyewe.

‘’Chakufanya ili kudhibiti hali hiyo, hata wauzaji dawa katika maduka yanayotambulika, wasitowe dawa pasi na buku la mtaalamu wa afya alivyoelekeza,’’anaushauri.

                                        MWISHO

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch