Skip to main content

WANAKAMATI, WAHAMASISHAJI JAMII MRADI WA SWIL WAIBUA MJADALA MZITO KWA WANAWAKE NA UONGOZI

 



 

NA NUSRA SHAABAN

Wahamasishaji jamii(CBs) pamoja na wanakamati walio katika mradi wa Kuongeza Ushiriki wa Wanawake kwenye Masuala ya Uongozi na Demokrasia (SWIL), unaofadhiliwa na Ubalozi wa Norway nchini Tanzania, wameibua mjadala huo kufuatia kikao kilichoandaliwa na  Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA)  katika ukumbi wa Skuli ya Turkey  Mpendae Zanzibar.

Kikao hicho, kimewapa fursa wanakamati hao pamoja na Wahamasishaji jamii  hao, kuwasilisha ripoti zao za ufuatiliaji wa changamoto za kijamii na utendaji kazi wao kuanzia mwezi Januari 2023 mpaka Juni 2023.

Jumla ya ripoti kumi zimewasilishwa  na kuibua mijadala tofauti  inayohusu wanawake na uongozi.

Miongoni mwa maeneo yaliyozua mjadala mkubwa ni suala la wanawake wanaotaka kugombea nafasi za uongozi kuambiwa vyeti vyao ni feki.

Akielezea kwa undani juu ya changamoto hiyo, Bi Sabahi  Bakari Hassan, Mhamasishaji  jamii kutoka Wilaya ya Kati, alisema kwa wanawake waliopo Wilaya ya kati changamoto hiyo ya vyeti inaonesha imewaathiri kwa kiasi kikubwa  kwani  hupata  usumbufu wa kutofikia malengo wanayokusudia hasa ikizingatiwa cheti cha kuzaliwa kina umuhimu wake katika harakati za mwanamke na uongozi.


Uploading: 27306393 of 27306393 bytes uploaded.



“Takriban vyeti vyote vya wanajamii kwa Wilaya ya kati ni  feki, hiyo ni kwasababu, wahusika hawajui taratibu za uhalali wa vyeti, na katika  kipindi cha nyuma ,kuna uzembe ulifanyika! wewe ukienda muda wowote utaandikiwa cheti, lakini utapewa namba ya mtu mwengine, cheti cha mtoto wa kiume mara atapewa mtoto wa kike, kipindi hicho ilikuwa unatozwa kiasi cha Shilingi 15,000, cheti utakiona halali kwa sababu hujui taratibu zake” alisema bi Sabahi.

Bi. Sabahi anaendelea kusema kwamba, baada ya muda mtoto  anafikia hatua ya kwenda Sekondari, unapokwenda Mambo Msije, ndipo unapokuja kugundua kwamba kumbe cheti ni feki.

Aliongeza kwa kusema kwamba,Mratibu aliekuwepo Mambo Msije kwa wakati huo alietambulika kwa jina la Rehema, ameshastaafishwa na mafao yake yote hakupewa kutokana na uzembe alioufanya. Sasa kilichobakia ni kufuata  utaratibu mpya wa kufuatilia vyeti vya watoto .”

“Utashangaa unaambiwa cheti  feki, binafsi huwa najiuliza sasa inakuaje kuwepo na vyeti feki wakati mhusika aliyepatiwa cheti  hicho  alikipata kwa wahusika wa masuala ya  vyeti“? Riziki Msomi Juma kutoka Wilaya ya Kati alihoji .

“Sasa hapo mwanamke mwenye nia ya kuwa kiongozi hata akija kukipata hicho cheti cha kuzaliwa,muda nao si umeshaenda?”.Hili nalo litazamwe linawasumbua wanawake na harakati za kuwania nafasi za uongozi.” Bi Riziki alisema.

Akiongelea suala la vyeti feki, Mkurugenzi Mtendaji wa Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) Bi, Jamila Mahmoud, alisema kwamba ipo haja kwa  jamii kuelimishwa kuhusu utaratibu wa kufuatilia vyeti vya kuzaliwa, kwani wengine hushindwa kufuatilia vyeti hivyo kwa kuona tabu na muhali, huku wengine kufikia hatua ya kugharamika kwa uenyeji na kukwepa kufuata utaratibu maalum uliowekwa na Serikali.

Kwa upande mwengine ripoti hizo, zimeonesha hatua mbalimbali  zilizochukuliwa na wanakamati pamoja na wahamasishaji jamii hao katika kutatua changamoto za mwanamke na uongozi kama nukuu ya  mwanakamati  Abibu Ali Sheha kutoka Kaskazini  “A” inavyojidhihirisha  hapa chini :

“ Ili mama apate muda wa kuingia katika uongozi, tumeona tumsaidie katika malezi kwa kutumia njia ya kudhibiti wimbi la ajira za watoto, tuliungana kulisimamisha janga hilo kwa watoto maeneo ya Nungwi”

ZAFELA inatekeleza mradi huo kwa kushirikiana  na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake TAMWA Zanzibar na PEGAO kwa upande wa Pemba.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch