Skip to main content

ELIMU YA AFYA YA UZAZI KWA VIZIWI IKO NJIA PANDA, WIZARA YASEMA NENO

 











NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

KUANZIA mwaka 1983 hadi 1992, hatua mbali mbali zilichukuliwa, ikiwani pamoja na maamuzi ya mwisho ya Umoja wa Mataifa, kuitangaza Disemba 3 ya kila mwaka, kuwa siku ya kimataifa ya watu wenye ulemavu.

Siku hiyo, pamoja na mambo mengine, kundi la watu wenye ulemavu hujadili, mafanikio na changamoto zao, zikiwemo za huduma za afya.

Kisha serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, iliunda Mkakati wa Kitaifa wa Ujumuishi wa mwaka 2010 hadi 2015, na sera ya taifa ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2004, ukitaja ulazima wa huduma za afya kwa watu wenye ulemavu.

Ipo sera ya kitaifa ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2018 kwa upande wa Zanzibar, ambayo Ibara ya 20, inasisitiza uimarishwaji wa upatikanaji huduma bora na endelevu kwa kundi hilo.

Serikali ilitunga sheria ya Watu wenye Ulemavu ya mwaka 2010, ambapo ilikuja kuharakisha huduma bora na endelevu za afya kwao.

Kwa Zanzibar, ilikuwa na sheria ya watu wenye ulemavu, nambari 9 ya mwaka 2006, ambayo imefutwa na sasa kuwa na sheria mpya nambari 8 ya mwaka 2022.

Kifungu cha 28 (1) (c) cha sheria hiyo, kimeainisha haki ya kupata huduma na elimu ya afya, kwa watu wenye ulemavu, ikiwemo matibabu, matengenezo au marekebisho yanayohusiana na aina ya ulemavu wao.

Kulikuwa na Mpango Mkakati wa sekta ya afya wa miaka tisa, ambao uliishia mwaka 2019, nao ulitaja hatua za kuchukuliwa, ili kuwakinga na utapiamlo wanawake, watoto na watu wenye ulemavu.

Kimataifa upo Mkataba wa haki za watu wenye ulemavu, ambao Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliusaini mwaka 2007, na kuthibithisha mwaka 2009, ambao unalazimisha huduma za afya, kwa watu wenye ulemavu.

Ibara ya 25, inasisitiza nchi wanawachama, zitumbue kuwa, watu wenye ulemavu, wanayo haki ya kunufaika kwa kiwango cha juu, cha huduma na elimu ya afya.

 ‘’Nchi wanachama zitatoa huduma za afya, zinazohitajika kwa watu wenye ulemavu, hasa kutokana na aina ya ulemavu wao, yakiwemo maeneo ya vijijini,’’umefafanua Mkataba huo.

Ukaongeza kuwa, nchi hizo zitawataka wataalamu wa afya, kutoa huduma za kiwango sawa, kwa watu wenye ulemavu, kama wengine.

HALI IKOJE KWA VIZIWI NA ELIMU YA AFYA YA UZAZI?



Omar Haji Omar wa Mtambile wilaya ya Mkoani mwenye watoto sita, akizungumza na wandishi wa makala hii, chini ya mkalimani wake, anasema hajapata elimu ya afya ya uzazi kwa aina ya miundombinu yake.

‘’Mimi nishahudhuria kliniki mara tatu, lakini sijawahi kupata elimu ya afya uzazi, hasa kwa aina yangu ya ulemavu,’’anasema.

 Khamis Massoud Khamis mwenye watoto wawili, mkaazi wa Kilamatinde anasema, hata yeye na mke wake wameshahudhuria klikini mara mbili, lakini hawapati elimu ya afya ya uzazi.

‘’Mara ya kwanza nilipokwenda tunawasiliana na daktari kwa njia ya maandishi, mpaka nikifahamu, lakini kwa kutumia mkalimani sijawahi,’’anasema.

Mkewake Khamisi, Aisha Muhidin Kombo, anasema njia anayotumia kupata elimu ya afya ya uzazi ni kujisomea vipeperushi, lakini sio kupitia madaktari.

‘’Ni kweli mimi nimezaa mtoto kila baada ya miaka mitatu, lakini elimu hii ni ya mazoea tu, sio kama nimefundishwa na madaktari,’’anasema.

Fatma Juma Mohamed (50) mwenye watoto 10, mkaazi wa Mchanga mdogo Wete, anasema mimba moja baada ya kuonekana na tatizo, alikwenda hospitali na mkalimani.

Maimuna Issa Haji na mwenzake Husna Kombo Omar wa Micheweni wanasema, wanapokwenda kliniki, hakuna mkalimani wa lugha ya alama na kukosa taarifa sahihi.

‘’Natamani hasa nipate elimu ya afya ya uzazi kwa kina, ili nijue mambo kadhaa, lakini inakuwa vigumu maana, wale ni wataalamu wa afya tu, sio wa lugha ya alama,’’anasema.

Mkalimani wa lugha ya alama Pemba Asha Suleiman, anasema hajawahi kualikwa na wizara ya Afya, ili kuwa makalimani wakati elimu ya afya uzazi ikisomeshwa.

Mwenyeikiti wa Chama cha Viziwi wilaya ya Chake chake Mohamed Khamis Shehe, anasema hakuna hata mkutano mmoja wao peke yao, waliowahi kualikwa wa utoaji elimu ya afya ya uzazi.

Mjumbe wa Umoja wa Watu wenye Ulemavu Zanzibar, Hidaya Mjaka Ali, anakiri kuwa, elimu ya afya ya uzazi bado ni changamoto kwao.

‘’Ni kweli wizara ya Afya, imeyafikia makundi yote, lakini kwa wenzetu wenye uziwi kwa mkutano wao peke yao, hilo halijafanyika,’’anasema.

Mratibu wa Baraza la Taifa la watu wenye Ulemavu Zanzibar ofisi ya Pemba, Mashavu Juma Mabrouk, anakiri kuwa wizara ya Afya, haijawahi kuliita kundi la watu wenye uziwi, kuwapa elimu hiyo.     

‘’Mbinu tunayoitumia kwa watu wenye uziwi, ili wafikiwe na elimu ya afya ya uzazi, ni kuwatumia maafisa wa Baraza, ambao wameshapata elimu na kukutana na viziwi,’’anasema.

Changamoto inayojitokeza kuwa ni uwepo wa viziwi zaidi ya 400 kisiwani Pemba, ingawa yupo mkalimani mmoja anayetambulika rasmi.

Muhudumu wa afya shehiani Kisiwani panza, ‘CHV’ Haroub Makame Bakar, anasema kwao ni changamoto kuwafikishia elimu viziwi, kutokana na wao, kukosa mafunzo ya lugha ya alama.

‘’Sisi ‘CHV’ tupo watano kwenye shehia hii, lakini hakuna hata mmoja ambae anaelimu, japo ndogo ya lugha ya alama, inakuwa vigumu kuwasiliana nao,’’anasema.

WIZARA YA AFYA INASEMAJE?



Afisa Mdhamini wizara ya Afya Pemba Khamis Bilali Ali, anasema anapotokezea mjamzito mwenye uziwi, huwasiliana na mamlaka husika, kwa ajili ya kupatiwa mkalimani.

‘’Ni kweli wataalamu wetu wa afya hawana utaalamu wa ukalimani, lakini akitokezea mjamzito na mwenzawake wanahitaji ukalimani, tunawasiliana na wenzetu katika hilo,’’anasema.

Eneo jingine, anasema wapo wajawazito ambao ni viziwi, lakini panakokua na shida ya kupata elimu zaidi, huhudhuria kliniki na waume zao.

‘’Wakati mwengine hufuatana na ndugu au jamaa zao wanaoelewa lugha ya alama, ili madaktari wanapowasiliana, iwe rahisi kupata majibu,’’anaeleza.

Anaona bado ipo fursa kwa wale viongozi wa jumuia za watu wenye ulemavu, kuwasilisha maombi kwao, ikiwa wanahitaji elimu ya afya uzazi, chini ya mkalimani wao.

Mtaalamu wa afya ya uzazi kutoka hospitali ya Chake chake Rahila Salim Omar, anasema haki ya afya ya uzazi ndio msingii wa kuwa na afya njema.

Anaona, bado baadhi ya wanaume, wamekuwa wazito kuwasindikiza wenza wao, kuhudhuria kliniki, jambo ambalo husababisha matatizo kadhaa wakati wa kujifungua.


NINI ATHARI YAKE?

Aisha Hussein Khamis, anasema kama wao wataendelea kutengwa kwenye elimu ya afya uzazi, kunaweza kukalizwa matatizo kadhaa, ikiwemo kifo kwa mama na mtoto.

Mwanajuma Majid Ibrahim, anasema athari nyingine ni kukosekana kwa mfumo wa lihse husika kwa mjamzito, kunakotishia kuzaliwa mtoto mwenye utapiamlo.

Mbarouk Juma Daudi wa Kengeja, anasema athari nyingine ni kuongezeka kwa uzazi wa papokwa papo, kunachochangiwa na ukosefu wa elimu ya afya ya uzazi.

Afisa Mdhamini wizara ya Afya Khamis Bilali Ali, anasema moja ni kuongezekwa kwa wimbi la wanaojifungulia majumbani.

Afisa wa Chama cha Viziwi wilaya ya Chake chake Mohamed Khamis Shehe, anasema ni kuwaweka wao katika msingi wa kukumbwa na magonjwa nyemelezi.

NINI KIFANYIKE?

Mratibu wa Baraza la Taifa la watu wenye ulemavu Zanzibar ofisi ya Pemba, Mashavu Juma Mabrouk, anasema ni wizara ya Afya, kurudi kwa kundi la watu wenye ulemavu, ili kuliemisha kwa mujibu wa miundombinu yao.

Mkalimani wa lugha ya alama Asha Suleiman, anashauri vipindi na taarifa zote za kwenye tv zinapoendeshwa, kuwepo kwa mkalimani.

Mzazi mweye kijana mwenye uziwi, anasema ni kutekelezwa kwa sheria kama zilivyo, ili kundi hilo lipate haki zao.

TAMWA ZANZIBAR INAFANYA NINI?

Chama cha Waandishi wa habari Wanawake Tanzania TAMWA- Zanzibar na Tanzania bara wanashirikiana, katika kuendesha mradi wa mwaka mmoja, wa kuwajengea uwezo waandishi wa habari kuandika, habari za afya ya uzazi.

Kwenye mafunzo yaliofanyika Pemba, Mratibu wa mradi huo Zaina Abdalla Mzee, anasema tafiti zilionesha, kuna vipindi na habari kidogo, katika vyombo vya habari, juu ya haki ya afya ya uzazi.

Mradi huu wa majaribio, ambao unafadhiliwa na Shirika la Wellspring Philonthropic fund la Marekani, unaendeshwa katika wilaya za Chake chake, Magharibi ‘B’ na Kati.



Moja ya shabaha kuu, ni kuhakikisha wanawake na wasichana walioko mjini na vijijini, wanakuwa na elimu sahihi ya afya uzazi, kupitia vyombo vya habari.

TAKWIMU

Wakati hayo yakifanyika, Wizara ya Afya Zanzibar, imebainisha kuwa, katika kipindi cha mwezi Julai, 2022 hadi Machi, 2023, kuna vifo vya mama 46 na vya watoto wachanga chini ya siku saba 1,567 viliripotiwa.

Vifo hivyo ni sawa na kila wilaya moja ya Zanzibar kati ya 11, kuwepo wa vifo vya mama watano, sawa na 142 nao kufariki katika wilaya hizo, katika kipindi hicho.

Aidha mwaka huo huo, wapo wajawazito 52,891, sawa 4,808 kutoka kila wilaya moja ya Zanzibar, waliohudhuria kliniki ya upimaji mimba, angalau mara moja.

Kati yao, wajawazito 9,017 walihudhuria kliniki wakiwa na ujauzito chini ya wiki 12, huku kukiripotiwa wajawazito 38,097, Unguja 26,405 na Pemba 11,692 kujifungulia hospitali.

 

                              Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch