Skip to main content

WANAWAKE WALIMA MWANI PEMBA WADADAVUA MACHUNGU, SERIKALI YAJA NA NEEMA KWAO

 

  

NA ABUU BAKAR, ZU@@@@

MWANI ‘sea weeds’ ni aina ya zao, lenye mnasaba na kiumbe hai, kinachopatikana baharini pekee.

Kwa uasili wake viumbe hawa, huota na kukua kwenye fukwe zenye asili ya mawe au mchanga mzito, nyasi za baharini na kwenye matumbawe.

 Kwa karne mbili na nusu zilizopita, zao la mwani, halikubeba thamani yake, na lilionekana kama vile ni bustani ya habarini yenye lengo la kuwapendezesha viumbe kama samaki.

Kwa kule kucheza cheza kwao, kufanya mazalio, nyumba, sehemu za mapunziko na chakula kwa baadhi ya viumbe.

Ilionekana, kama vile mwani ni viumbe vinayoota na kufa kila baada ya muda, na hakuna aliyefikiria kuwa, iko siku zao hilo linaweza kuwa sehemu ya kukuza pato la mtu au taifa.

Baada ya kuonekana kuwa na thamani, sasa wataalamu wanatueleza kuwa, ziko aina mbali mbali za mwani, ambazo hutofautiana kutoka ukanda mmoja wa bahari na mwingine.

Kwa mfano Tanzania, kuna aina mbili kuu za mwani, ule unaoitwa “Eucheuma denticulatum” au kwa jina jingine hujulikana kama “Eucheuma spinosum” na aina ya pili inaitwa “Kappaphycus alvarezii”.

 Kwa kwaida mwani huwa na rangi ya kijani, kahawia na nyekundu, ambapo rangi hizo zinasababishwa na kuongezeka au kupungua kwa kina cha maji ya bahari.

Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, imeanisha kuwa, uzalishaji wa zao la mwani umeongezeka kutoka, tani 10,531 kwa mwaka 2021 hadi tani 12,594 kwa mwaka 2022 sawa na ongezeko la asilimia 20.

Taarifa ikafafanua kuwa, usafirishaji wa mwani nje ya nchi umeongezeka kutoka tani 12,124 kwa mwaka 2021 hadi tani 13,972 mwaka 2022 sawa na ongezeko la asilimia 15.



CHANGAMOTO ZIPI WANAZOZIPATIA WA KULIMA WA MWANI?

Mkulima wa zao hilo kutoka shehia ya Sizini Salma Khamis Juma, anasema hulazimika kufanya jitihada binafsi, ili kuupata mwani, ikiwemo kutembea kwa miguu kwa kuvuuka sehemu zenye hatari.

Changamoto nyingine anasema, sehemu wanazopita kutafuta mwani zina kuwa na tope na visiki vinavyochoma mithili ya misumiri, ambapo huwakumba wao, wasio na viatu vya kinga.

‘’Mwani hata ukifika nao juu kwa ajili ya kuuwanika, umeshapitia kadhia kadhaa, na wakati mwengine unaweza kushindwa kurudia siku nyingine kwa miguu kupata majeraha,’’anaeleza.

Haisau siku aliyongia kwenye dimbwi lenye tope, na kuzama mpaka magoti, wakati anarudi kuvuna mwani shambani kwake, na kuokolewa na mwenzake.

Mkulima Raya Ali Bakar wa Shehia hiyo ya Sizini wilaya ya Micheweni, anaeleza kuwa, kama sio shujaa wa kweli, ni vigumu kwa mwanamke kujiingiza kwenye kilimo cha mwani.



Anaona kuwa machungu, shida, kadhia ya kuuza roho inayowakabili wakulima wa mwani, ni vyema ikaenda samba mba na bei husika.

‘’Sisi wanawake ambao tumejiingiza kwenye kilimo cha mwani, ni sawa na kuuza maisha yetu kila siku, na huku ukiangalia bei nayo inaumiza kama matayarisho ya kilimo chenyewe,’’anaeleza.

Ali Salim Bakar, anaeleza kuwa kilimo cha mwani hawezi kukifafanisha na kilimo chochote chenye tija na taifa, kutokana na ugumu uliopo wakati wa matarisho yake.

Kule kulimwa ndani maji, kushughulikiwa ndani ya maji na hata kuvunjwa ndani ya maji ni ishara kuwa, kilimo hicho kinaishi pamoja na changamoto zake.

‘’Kila mmoja anasema kama akipata kazi nyingine anaweza kukihama kilimo cha mwani, maana machungu ni makubwa ingawa bei haiendani na kazi zake,’’anaeleza.

Zainab Ali Bakar, anasema ukosefu wa vifaa kinga, vidau vya kusafirishia mwani, bei na wizi unawakosesha furaha katika kazi yao ya kilimo cha mwani.

 UONGOZI WA SHEHIA YA SIZINI

Sheha wa shehia ya Sizini Suleiman Shaame Hamad, anasema wakulima wengi wanaoendesha kilimo hicho ni wanawake, hivyo ni vyema wakaangaliwa kwa jicho la huruma.

‘’Naelewa kuwa, kwa sasa serikali inayomikakati kabambe ya kuhakikisha, wakulima wa mwani wanasahau machungu wanayopata kwenye kilimo hicho,’’anaeleza.

Sheha anawakumbusha wakulima wa zao hilo, kuwa nao watakuwa juu kama walivyowakulima wa zao la karafuu, hasa baada ya uwepo wa kiwanda cha kusarifia mwani Chamanangwe.

Afisa Uvuvi Wilaya ya Micheweni Abdalla Issa Nassor, anasema kuwa wakulima wanakabiliwa na changamoto nyingine inayowakabili wakulima hao ni ya maradhi kwa mwani wao.

Jambo hilo hufanya mwani kuharibika, na kuwafanya wakulima wa zao hilo, kutokufikia malengo yao waliyojiwekea.

Kutokana na changamoto hizo miradi mbali mbali  imeanzishwa kuwasaidia vikundi tofauti, ikiwemo mradi wa IUCN ambao makao makuu yake yapo Dar es Salam, ambapo mradi huo husaidia sehemu mbili kwa Pemba, Mkoani na Micheweni.

Kwa upande wa Micheweni Umesaidia kikundi cha Mikoko, kinachoitwa Shirikani Coparetive Society, kikundi cha Ufugaji wa samaki kinachoitwa Mapambano Coparetive Society na kikundi cha mwani Tuelewane kilichopo kinowe.

SERIKALI KUU INASEMAJE

Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Suleiman Massoud Makame anasema kwa mwaka huu wa fedha, mkazo zaidi umewekwa kwenye maendeleo ya viwanda vya kusarifu samaki, mwani na mazao mengine ya bahari.

 Aidha anasema machungu wanayoyapata wakulima wa mwani wa Unguja na Pemba, yataondoka karibuni kuwatafutia mikakati ya vitendo iliyowekwa na serikali ya awamu ya nane, ikiwemo ujenzi wa kiwanda cha kusarifia mwani.

Akisoma taarifa ya kitaalamu wakati mwenge wa uhuru ulipotembelea Juni mwaka 2023, Mkurugenzi mkuu Kampuni ya mwani Zanzibar Massoud Mohamed Rashid, anasema ujenzi wa kiwanda hicho umefikia hatua nzuri.

Alieleza kuwa, ujenzi huo ambao unajengwa na Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo Zanzibar ‘KMKM’ uko katika awamu ya kwanza, kati ya zile tatu hadi kukamilika kwake.

Alieleza kuwa, awamu ya kwanza inajumuisha ujenzi wa jengo kuu la kiwanda, ujenzi wa ghala pamoja na uzio maalum kwa ajili ya kulihifadhi eneo hilo.

‘’Awamu ya pili utajumuisha ujenzi wa maeneo ya bustani, ufungaji wa mitambo husika na awamu ya tatu ni kuanza uzalishaji bidhaa zitokanazo na mwani,’’aliwaeleza wakimbiza mwenge kitaifa.

Kwa wakati huo, tayari ujenzi huo wa awamu ya kwanza umeshafikia asilimia 86, na ukitarajiwa kutumika shilingi bilioni 8.2 ingawa wameshatumia shilingi bilioni 4.024 na utakapomalizika wote, utagharimu shilingi bilioni 13.

‘’Mradi huu wa kiwanda, utakapomalizika utakuwa na uwezo wa kusarifu mwani tani 30,000 kwa mwaka, ambapo umiliki wake kwa asilimia 55 utakuwa serikalini na asilimi 45 utakuwa wa kampuni ya Nutri-san.  

Taarifa kutoka wizara ya Uchumu wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, zinaeleza kuwa, usafirishaji wa mazao ya baharini ikiwemo matango bahari, mwani, dagaa, kaa na pweza umeongezeka kutoka tani 19,063 mwaka 2021 hadi tani 23,158 mwaka 2022 sawa na ongezeko la asilimia 21.



Uzalishaji wa zao la mwani nao umeongezeka kutoka tani 10,531 mwaka 2021 hadi tani 12,594 kwa mwaka 2022 sawa na ongezeko la asilimia 20.

Huku pia ikianishwa kuwa, usafirishaji wa mwani nje ya nchi umeongezeka kutoka tani 12,124 mwaka 2021 hadi tani 13,972 mwaka 2022 sawa na ongezeko la asilimia 15.

                                  Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch