Skip to main content

MAKTABA ZA SKULI ZIWE CHEM CHEM YA UFAULU KWA WANAFUNZI

 

          


NA TATU NAHODA, ZU@@@@

……………fuata nyuki ule asali…………….

Ndivyo walivyosema wahenga, wakimaanisha kuwa, unapaswa kufuata vitu, watu au sehemu zenye ujuzi, ili kufanikiwa katika malengo yako.

 Msemo huu unatumika katika nyanja nyingi ikiwemo ya wanafunzi wanaofuta elimu, hasa kwa mfumo wa kupitia maktaba ziwe na skulini au maeneo mingine.

Maktaba ni hazina pekee inayomtajirisha mwenye kuhitaji utajiri wa kitaaluma na kimaarifa, kwani mtumiaji hapitwi na wakati, na hupata taarifa muhimu juu ya mambo mbali mbali.

Kwa wanafunzi na walimu wao, maktaba imekuwa ni hazina yao ya thamani, kama alivyosema mtaalamu Marcus Tallus Cicore "if you have a garden and library you have everything you need " ukiwa na tafsiri  isiyorasmi kuwa, kama una bustani na maktaba basi tayari una kila kitu.

KWANINI MAKTABA NI MUHIMU SKULINI?

Ahmed Khamis Ahmed mwanafunzi wa kidato cha pili skuli ya Madrasatul-Ahbaab Kisauni Unguja anasema, maktaba kwake ni suluhisho la ufumbuzi wa kielimu na maarifa.

Kwani, anaona ni chanzo cha upatikanaji wa vifaa vya kujifunzia, kama vile vitabu, majarida na vifaa vyengine vinavyohusiana na tasnia ya elimu na masomo yao kwa ujumla.

"Maktaba ni hazina isiyochakaa, ambayo utajiri wake unajitokeza kwa kila mmoja wetu, na kwa kadri ya kila mmoja wetu anavyoitafuta elimu na kujifunza,”anasimulia.

Wanakuwa wanajifunza vitu vipya, ambavyo hawakupata kufundishwa kwa upana madarasani na walimu wao, na hivyo huamua kwenda zao maktaba na kujisomea, ili kuongeza maarifa zaidi.

Salum Issa Salum na mwenzake Aziza Hassan Mzee wanaosoma kidato cha nne skuli ya Mtambile Mkoani, wanasema wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, imefanya jambo jema, kujenga kituo cha maktaba skulini kwao.

"Kwa sasa ni tofauti na zamani, ambapo tulilazimika kuzifata huduma za maktaba mji wa Chake Chake, jambo lililotuwiya vigumu kutokana na masafa yalivyo,’anasema Salum.

Asia Kassim Daru mwanafunzi wa kidato cha sita skuli ya Dk. Salmin Amour ya Chumbuni Unguja, anasema maktaba huhimiza utamaduni wa kujifunzia stadi za maisha na kuwatia moyo, ili waendelee kutafuta maarifa zaidi ya masomo yao.

"Kupitia Maktaba hasa wanafunzi tunaotarajia kufanya mitihani yetu ya taifa, maarifa huongezeka, mithili ya chem chem jangwani, kwani tunapata weledi wa kujibia mitihani hiyo," anaeleza.

Kwake Maktaba ni msaada mkubwa, kwani ni sehemu inayoleta amani, utulivu na umakini, ambao unafaa katika mazingira ya kujisomea, na hata kumpa uwezo mzuri wa kufikiria, juu ya masomo yake.

 Mwanafunzi Makame Nahoda Juma, wa kidato cha tano skuli ya Mwanakwerekwe ‘C’ iliyopo wilaya ya Magharibi ‘B’ Unguja, anaeleza kuwa, Maktaba ni fursa pekee ya kupata taarifa za kielimu na kijamii bila ya kujali hali ya kijamii na kiuchumi.

"Wanafunzi walio wengi hali zao za kiuchumi ni ndogo, hivyo hawamudu baadhi ya mahitaji ya skulini, kama vile ununuzi wa vitabu ambavyo wanapaswa kuwa navyo, katika masomo yao,"anafanua.



WAALIMU

Kama maneno ya wahenga walivyosema,"mwalimu ni mwanga wa maarifa katika giza la ujinga, hii ikiwa na maana walimu hutoa muongozo na elimu kwa wanafunzi wao.

Mwalimu mkuu wa skuli ya Mtambile Mkoani Pemba, Abrahman Hassan Bakar, anasema kuwepo kwa vituo vya maktaba katika skuli huchochea ongezeko la ufaulu.

Mwalimu huyo anafafanua kwa kutoa mfano kuwa, kati ya wanafunzi 200, hivyo wastani wa wanafunzi 150, huingia maktaba kufanya kutafuta maarifa zaidi ya kielimu.

Anaeleza kuwa, ujio wa maktaba hasa skulini kwake, kama vile umekuja kuwaamsha na kuchochea wanafunzi, kwanza kujisomea zaidi, kupata maarifa na mbinu za kujibia mitihani ya taifa.

Akaeleza kwa mfano kuwa, kwa mwaka 2022 skuli hiyo ilifaulisha wanafunzi 26, kuingia kidato cha tano, na kuvunja rikodi ya historia ya skulini hapo.

"Kwa mara ya kwanza, skuli imeongeza ufaulu wa wanafunzi, ikiwa miongoni mwa kichocheo kikubwani  ni uwepo wa Maktaba skulini hapa,"anasimulia.

Hivyo, akawagawageukia wanafunzi wa skuli mbali mbali, kutumia maktaba zilizomo skuli mwao, ili ziwasaidie kupata ufahamu na ujuzi wa mada mbali mbali, zilizomo kwenye mtaala.

Mwalimu Hafidh Said Ali na mwenzake Zakia Ali Abdallah, wanasema maktaba za skuli hazisaidii wanafunzi pekee, bali na wao kwani, huingia maktaba kupata maarifa zaidi kabla kuingia madarasani.

"Maktaba skulini zimezaa matunda ya elimu, sio tu kwa wanafunzi wetu lakini hata kwa sisi walimu wao, maana tunazitumia kabla na hata baada ya kusomesha masomo yetu,"wanaeleza.

Hapa Msimamizi wa Maktaba skuli ya Mtambile Amina Said Salum, anaeleza kuwa, kuwepo kwa maktaba, kumesaidia kuinua kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi, katika masomo yao mbali mbali.



Mkutubu Sabra Abdallah Nassor, katika maktaba ya skuli ya Almadrastul-ahbaab ya ya Kisauni Unguja, anaeleza kuwa, muamko wa wanafunzi katika skuli hiyo, kuhudhuria maktaba ni mkubwa.

Anasemea kwani wanafunzi wanaohudhuria ni zaidi ya 30, kwa kila wanafunzi 40, kutoka madarasa tofauti tofauti yakiwemo yale wanaojitayarisha na mitihani ya taifa.

Katibu wa Jumuiya za kukuza Maktaba za skuli Zanzibar Abbas Mohamed Omar, anaeleza kuwa, kuwepo kwa maktaba skulini ni suala zuri, kwani husaidia wanafunzi, kuondoa changamoto zao za kielimu na maarifa.

Anaeleza kuwa, skuli nyingi za sekondari za Zanzibar, zimekuwa na maktaba, ingawa suali la kujiuliza je, maktaba hizi zinakidhi haja za watumiaji wake?.

Anaona kuwa, Maktaba nyingi za skuli za sekondari, hazikidhi haja za watumiaji wake, kutokana na kukabiliwa na changamoto kadhaa ikiwa ni pamoja na baadhi zao, kukosa wakutubi wenye sifa.

‘’Kwa kweli wizara ya Elimu, imejitahidi kuhakikisha kuwa, kila skuli ya sekondari inakuwa na Maktaba, lakini bado vifaa vya kutosha ni changamoto mpya,’’anaeleza.

HALI YA MAKTABA ZA SKULINI

Kwa mujibu wa Shirika la Huduma za Maktaba Zanzibar, linaeleza kuwa, ni skuli 40 pekee kati ya kila skuli 100, ndizo ambazo zina maktaba na 60 hazina.

Ingawa kwa upande wa skuli za sekondari za Zanzibar, imebainika kuwa, kila skuli 100, basi 70 zinahuduma ya maktaba na 30 pekee, bado hazijafaidika na huduma hiyo.

Takwimu hizi zinaonesha kuwa, suala la maktaba bado halijapewa umuhimu wake, unaostahili katika skuli za msingi, skuli ambazo kama jina lake lilivyo, zinatarajiwa kumjengea msingi madhubuti wa mwanafunzi.

                                           MWISHO.

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch