Skip to main content

WANANCHI KIDAGONI WAKOSA ELIMU KISA............

 



ZANZIBAR

 

 Na Nafda Hindi, ZANZIBAR @@@@

 WANANCHI wa Shehia ya Kigongoni Wilaya ya Kaskazini 'A' Unguja walalamikia umbali wa masafa marefu kwa watoto wao wakifuata huduma ya Elimu.

wameiomba serikali kuwajengea skuli karibu na makaazi yao ili Watoto wao wapate elimu ipasavyo na kuwaepusha na hali hatarishi.

 

Malalamiko hayo yamekuja kufuatia ziara ya kuibua changamoto za wananchi iliyoandaliwa na Chama cha waandishi wa Habari wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar kupitia mradi wa kuwainua wanawake katika  Uongozi, Strengthen Women In Leadership  (SWIL) unaotekelezwa na chama hicho.

 

Wazazi wa watoto hao wamesema kwa sasa Watoto  wanasoma skuli ya  mbali ambayo wanatembea Zaidi ya saa moja hali inayohatarisha usalama wao na wengine kushindwa  kufika skuli kuendelea na masoma na kuishia vichakani .

 

“Skuli iko mbali na sisi inabidi twende Fukuchani. Kidagoni au Kidoti hali ambayo ina hatarisha usalama wa watoto wetu, na sisi wazazi huwa hatuna Amani mpaka watoto warudi skuli,” Mwananchi, Shehia ya Kidagoni.

 

Mmoja wa wananchi hao Ali Simai Silima amesema shehia hiyo ya kigongoni hakuna skuli na badala yake Watoto wa eneo hilo wanakwenda kusoma skuli ya kidagoni ambayo ni mbali na shehia hiyo.

 

“Vijana wangu wanasoma maeneo ya mbali tumejenga banda la skuli katika maeneo ya karibu lakini baadhi ya Viongozi wa chini  wametwambia tuondoshe baadhi wanafunzi hasa watoto wadogo wamekata kwenda skuli kabisa kutokana na masafa ya mbali,” Mwananchi.

 

Aidha amesema Watoto wake kusoma kwa umbali huo anakosa amani kutokana na dunia kukumbwa na matukio mengi ya kihalifu ikiwemo udhalilishaji.

 


“Mtoto akitoka kwenda skuli hafiki anakwama njiani,unaambiwa wende ukachukuwe mwanao, tunawaambia Viongozi wetu wa Jimbo kama wanatutaka mwakani tuwapigie kura walitazame suala hili kwa umakini, sisi wazee ndio tunaoumia.

 

 Nae Mwalimu Mkuu wa skuli ya Maandalizi na Msingi kidagoni Machano Khamis Machano amesema zaidi ya wanafunzi 30 wa skuli hiyo wanakosa masomo kwa siku kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo masafa marefu ya maeneo wanakoishi.

 

“Suala hili kwa kweli linatuumiza kichwa wanafunzi wanatoka majumbani kwao lakini hawafiki skuli, kuna kijiji kinaitwa Kijini Mbumbwi ni sehemu ambayo iko mbali, watoto wengi wanatoka huko tena wadogo wa Nursery na ni pori tupu, mwendo wa saa moja huko hakuna skuli kwa hiyo wanakosa haki yao ya msingi ya kupata Elimu.” Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Msingi Kidagoni, Machano Khamis Machano.

  

Alisema wanafunzi wa skuli hiyo wanatoka maeneo ya mbali haliambayo inawasababisha kuwavunja moyo na kuwasababisha kuishia njiani.

 

 

Alisema wanafunzi wanaosoma katika skuli hiyo wanatoka shehia ya kigongoni ,Bwereu na kidoti ambapo kutoka maeneo hayo hadi kufika skuli ni Zaidi ya saa moja kutembea huku njia zenyewe zikiwa haziridhishi kwasababu hatarishi.

Mwalimu wa skuli hiyo Zainab Silima Machano aliiomba serikali kuwawekea miundombinu mizuri ambayo itasaidia kufika skuli hapo kwa wakati kwasababu anatoka masafa marefu na akifika skuli huwa kashachoka na kusababisha kushindwa kuvikosa baadhi ya vipindi hususani vya asubuhi.

 

“Tunatoka mbali na changamoto hamna usafiri, watoto wanachelewa na pia wanakuwa watoro na kama kipindi chako ni cha kwanza hata ukifika skuli kushakikosa kwa kuchelewa,” Mwalim wa Skuli ya Kidagoni Zainab Silima Machano.

 

Baadhi ya wanafunzi wa skuli hiyo walisema hali hiyo ya umbali wa skuli inawaathiri hasa kwenye masomo yao ambapo muda mwingi wanautumia njiani badala ya kusoma hivyo wameiomba serikali kuwajengea skuli ya karibu ili kupata haki yao ya elimu bila ya usumbufu.

 

“Tukifika skuli tumechoka tokea kiwiliwili mpaka akili na masomo mengi tunakosa kutokana na kutembea masafa marefu, hivyo tunaomba Serikali itusaidie,” Mwanafunzi kutoka skuli ya Kidagoni.

 

Akizungumzia tatizo hilo Sheha wa shehia hiyo Vuai Mtosho Bure alisema hatua aliochukua ni kushirikiana na wananchi wake kuanza ujenzi wa skuli ya maandalizi katika maeneo hayo ya karibu ili kuwaondoshea usumbufu watoto wadogo kufuata huduma hiyo katika masafa ya mbali.

 

 “Naiomba  Serikali  kuu na wadau wengine wa maendeleo kuwakamilishia ujenzi wa skuli yao kwani wamekwenda katika maeneo mbalimbali ikiwemo uongozi wa Jimbo na halmashauri lakini bado hawajafanikiwa,” Sheha Kidagoni, Vuai Mtosho Bure.

 

Mratibu wa mradi wa kuwainua wanawake katika uongozi SWIL kutoka chama cha waandishi wa Habari wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar Mariam Ame Chum amesema  lengo la ziara hiyo katika maeneo hayo ni kuibua changamoto zinazoikabili jamii ili ziwe kufanyiwa kazi na wananchi waweze kupata huduma bora ambazo ni haki yao ya msingi, ikiwemo elimu , mali na miundombinu ya Barabara.

 

“Viongozi wa majimbo waliochaguliwa na wanachi watimize wajibu wao ipasavyo kuwahudumia wananchi na kupata haki zao za kidemokrasia kwa kutatuwa changamoto mbali mbali zinazowakabili kupitia majimbo yao,” Mariam Ame Choum. Mratibu SWIL, TAMWA,ZNZ.

 

Tamwa Zanzibar inatekeleza mradi huo wa kuwainua wanawake katika uongozi sambamba na kuibu changamoto za wananchi na kuwawezesha kupaza sauti zao kwa kudai haki zao za msingi kwa kushirikiana na ZAFELA na PEGAO chini ya ufadhili wa ubalozi wa Norway.

 

mwisho  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch