Skip to main content

Uzazi wa mpango ni haki inayopaswa kufurahiwa na wote

 



Na Mwandishi wetu, @@@@

Dhana ya kupanga uzazi kama haki ya binadamu ni muhimu. Inapinga maoni yoyote potofu kwamba ni aina ya udhibiti wa idadi ya watu na itahakikisha kwamba vizazi vijavyo kamwe havichukui haki hii ya kibinadamu iliyopatikana kwa bidii kuwa ya kawaida.

Katika kuhakikisha huduma za afya ya uzazi zinafikiwa kwa urahisi, mafunzo ya siku tatu kuhusu SRHR yalifanyika kwa waandishi wa habari, uhamasishaji ulifanywa kwa siku mbili, na vyombo vya habari vilijengewa uelewa kuhusu SRHR ikiwa ni pamoja na uzazi wa mpango.

Hata hivyo, pamoja na mafanikio yaliyopatikana, bado kuna changamoto katika upatikanaji wa huduma za afya ya uzazi.

Kwa mfano, ingawa upatikanaji wa uzazi wa mpango ni haki ambayo inapaswa kufurahiwa na wote, lakini sio wote wanaofaidika na haki hiyo.

Na ingawa ni wazi kuwa uzazi wa mpango unachangia katika kupunguza vifo vya uzazi na kuhakikisha kuwa akina mama na watoto wachanga wanakuwa na afya njema, wanandoa wengi bado wananyimwa haki ya kupanga uzazi na wapenzi wao.

Wanaume wamekuwa kikwazo cha kufikia malengo ya kitaifa kwa sababu wanasitasita kuwaruhusu wake zao kutumia njia za kupanga uzazi na hata kutishia talaka.

Hata hivyo, kama elimu ya uzazi wa mpango itawafikia wanaume wengi zaidi basi lengo la  kupunguza vifo vya uzazi na watoto wachanga ungekuwa na mafanikio makubwa zaidi.

Tunapaswa kujua kwamba kwa kila shilingi inayotumika kupanga uzazi serikali inaweza kuokoa maisha ya mama na mtoto na kufanya uzazi wa mpango  kuwa mojawapo ya uwekezaji wa gharama nafuu nchini.

Uzazi wa mpango unatoa fursa kwa wanawake na vijana kuchagua lini na mara ngapi kupata watoto lakini pia wasichana wengi zaidi wanaweza kubaki shuleni na wanawake wengi wanaweza kuamua kuingia au kubaki katika uchumi.

Mashirikia ya kimataifa kama UNFPA yameendelea kuongeza uwekezaji wa kitaifa katika huduma za uzazi wa mpango na huduma za afya ya uzazi, ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa huduma za kupanga uzazi, huku ikiunga mkono juhudi za kupanua wigo wa vituo vinavyotoa huduma za kisasa za uzazi wa mpango na kuimarisha ubora wa huduma hizo.

Lengo la UNFPA, miongoni mwa mengine, ni kupanua upatikanaji wa taarifa na huduma kwa vijana na makundi mengine yaliyo hatarini.

Kufikia malengo ya maendeleo endelevu ifikapo 2030, kunategemea ni kwa kiasi gani haki za afya ya uzazi zinazingatiwa.

Utimilifu wa mahitaji ya wanawake na wasichana ya kupanga uzazi ni mojawapo ya uwekezaji wenye faida zaidi kwa Zanzibar.

Dk Ali Omar Ali kutoka wizara ya afya, anasema uzazi wa mpango ni haki ya binadamu wote na ni muhimu huduma bora uzazi wa mpango  zipatikane na kufikiwa kwa urahisi.

Sheikh Abdullah Talib, Katibu Mtendaji wa Wakfu na Maliamana, anasema kuwa uzazi wa mpango unakubalika katika uislamu na unaruhusu familia kujitengenezea mazingira bora ya kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni na kiafya pamoja na kuweka mazingira bora zaidi ya elimu kwa watoto wao.

Anatoa wito kwa jamii kushikamana na ukweli/mafundisho ya kidini na kutosikiliza imani potofu.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch