Skip to main content

KIJALABU iSAVE ZANZIBAR WAWANOA VIONGOZI UCHUKUAJI MIKOPO


                                                                            
 


NA MARYAM SALUM,PEMBA@@@@

VIONGOZI na wanachama wa vikundi vya kuweka na kukopa  Pemba,  wametakiwa kuondokana na woga na badala yake kuchukua mikopo kwa ajili ya  kuendeleza biashara zao. 

Akifungua mafunzo ya siku mbili juu ya ushirikishwaji kwa viongozi wa vikundi vya maendeleo katika ukumbi wa mikutano Ofisi ya TAMWA Pemba, Mratibu wa Chama cha Waandishi wa habari TAMWA, Fat-hiya Mussa Said
alisema kuwa lengo la mradi wa Kijaluba iSave Zanzibar ni kuwainua kiuchumi wanavikundi hasa watu wenye ulemavu. 

Alisema kuwa fedha zilizopo kwenye Hisa zinatakiwa kukopwa kwa ajili ya kuendeleza biashara na sio kutazamwa tu.

"Mradi wa Kijaluba iSave Zanzibar unakusudia kuwatoa woga,ili kuona fedha zilizopo kwenye hisa munazichukua kwa mkopo kwa ajili ya kuboreshea biashara zenu kwa maendeleo zaidi," alisema mratibu huyo.

Alieleza kuwa fedha zilizopo zinatakiwa zitumiwe, na matumizi yenyewe ni kwa ajili ya kuendeleza na kuanzisha biashara nyengine za maendeleo.

Alisema Mradi wa Kijaluba iSave ni mradi unaolenga kuwawezesha watu wenye ulemavu kiuchumi,kuwajengea uwezo kuhusu maisha yao wenyewe na jamii zao.

"Lengo kuu ni kukuza uwezo wa watu wenye ulemavu kiuchumi kwa kujenga mitazamo chanya juu ya ushiriki wao, na kujiingiza katika shughuli za kujipatia kipato kupitia vikundi vya kuweka na kukopa ", alisema.

Alifahamisha kuwa Mradi huo unatekelezwa kwa mashirikiano kati ya Shirikisho la Jumuia za watu wenye ulemavu Zanzibar (SHIJUWAZA) na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania,(TAMWA Zanzibar) kwa ufadhili wa Chama cha watu wenye Ulemavu Nchini Norway (NAD).

Mratibu huyo  aliwataka viongozi hao wa vikundi ambao wamepatiwa mafunzo hayo ya biashara kuhakikisha wanakuwa walimu kwa wenzao, ili kuona lengo linafikiwa.

Alieleza kuwa mradi huo unatekelezwa katika Wilaya mbili Unguja na Pemba,ambapo  kwa Unguja ni wilaya ya Kusini na Wilaya ya Chake Chake Kusini Pemba.

Kwa upande wake Ofisa Muwezeshaji kutoka katika Mradi huo Muhidin Ramadhani Muhidin wakati akiwasilisha mada ya kuchagua,kupanga, usimamizi, kwa viongozi hao alisema kuwa Mradi unajukumu kubwa la
kuhakikisha wanawabadilisha wanavikundi kiuchumi. 

"Mradi wa Kijaluba utahakikisha unawatoa hofu na woga viongozi na wanachama wao kwenye vikundi vya maendeleo ili kuona wanafika mbali kiuchumi " , alisema Afisa huyo.

Alieleza kuwa lengo la Mradi ni kuwawezesha wanavikundi hasa watu wenye ulemavu, ili wawe na uwezo wakuchagua zile biashara zitakazoleta faida.

Aidha aliwataka wanavikundi hao kuyafanyia kazi mafunzo waliyopatiwa na kuwa mabalozi kwa wanachama wa vikundi vyengine, ili kuhakikisha miradi itakayokuja kuanzishwa wanafuata mfumo wa biashara yenye tija
kwa nia ya  kuondokana na umasikini.

Mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo kutoka katika kikundi cha Jembe kazi kilichopo Ole kwa niaba ya wenzake alisema mafunzo hayo yatakuwa chachu yakuleta mabadiliko kutokana na shughuli zao wanazozifanya za
kujipatia kipato.

Jumla ya vikundi 43  vimebahatika kwenye Mradi huo  ambapo Wilaya ya Kusini Unguja vipo vikundi 20 na Pemba 23, Mradi huo ni wa majaribio na unatekelezwa katika kipindi cha miaka miwili kutoka Novemba 2022 hadi Disemba 2024.



                               MWISHO.


Comments

Post a Comment

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch