Skip to main content

Afya za Vijana ziko hatarini kukosekana Vipimo vya kupima virusi vya Ukimwi (HIV KITS)

 



NA NAFDA HINDI, ZANZIBAR@@@@

KUKOSEKANA kwa vipimo vya kupimia maambukizi yanayosababisha ukimwi (HIV Kits) Zanzibar ni jambo linalowarejesha nyuma vijana kujitokeza katika vituo vya Afya kupima afya zao.

Hayo yamebainika kufuatia ziara iliofanywa na Chama Cha Waandishi wa habari Tanzania TAMWA,ZNZ wakati wa kutembelea vituo vya Afya na huduma Rafiki kwa vijana vilivyopo Wilaya ya Kati na Magharibi “B”.

 Wakizungumza kwa nyakati tofauti watoa huduma za Afya kutoka vituo mbali mbali wamesema licha ya vijana kuwa na mwamko wa kujitokeza kwa wingi katika vituo vya Afya kupima afya zao kwa sasa imekuwa ni tofauti kwa kukosekana vipimo vya maambukizi ya virusi vya ukimwi ambapo huvikimbia vituo hivyo.

“Idadi ya vijana ilikuwa iko juu na inaongezeka kwa kasi kupima Afya zao katika kituo chetu hasa virusi vinavyosababisha ukimwi ila kwa sasa kila leo idadi inapunguwa kutokana na tatizo la kutokuwepo vipimo vya kupimia maambukizi hayo,(HIV KITS), “ Mtoa huduma kituo cha Afya Mwera.

Tatizo hilo la kukosekana kwa vipimo vya kupimia virusi vya Ukimwi limedhihirika kwa takribani vituo vinne vya Serikali kutoka Magharibi “B” na Kati kwa Unguja ikiwemo Mwera, Fuoni, Tunguu na Magirisi kilichopo Taveta ambapo huduma hiyo hupatikana bila ya malipo.  

“Kwa sasa kuna upungufu wa HIV kits kwa wateja wetu, isipokuwa tunatowa upendeleo kwa mama wajawazito tuu ndo wanaofaidika na huduma hii kwa sasa,”Daktari Kiongozi Kituo cha Afya Fuoni, Sultani Shella.

Kijana amabae alifika katika Kituo cha Afya Magirisi kilichopo Taveta Meli Nnne kufuata huduma Rafiki kwa vijana amesema kukosekana kwa kipimo hicho athari inakuwa kubwa hasa kwa vijana kwa kutokujuwa Afya zao na hatimae kuleta majanga kwa jamii.

“Athari ni kubwa kwa vijana, kwa sababu ukitaka kufunga ndoa lazima upime HIV kama hakuna kipimo tutaumia na kuumiza familia hata Taifa kwa ujumla kwa kutokujuwa nani ni muathirika wa magonjwa hayo na utazidi kusambaza kwa wengine,” Kijana kutoka Meli Nne.

Hata hivyo kituo Afya  Mwera kilichopo Wilaya ya Kati Unguja  kinachohudumia Shehia ya Magharibi “A” na Koani licha ya kutoa huduma Rafiki kwa vijana, kinatowa huduma mbali mbali zikiwemo Uzazi wa mpango,Ushauri Nasihi, na  huduma za mama wajawazito na kwa mwezi huzalisha wajawazito wasiopunguwa mia moja na hamsini.



Mmoja kati ya mteja anaepata huduma kutoka kituo cha Mwera Maryam Abdalla Bakar amesisitiza wanawake kuhudhuria clinic mapema wakati wa kujigunduwa ni wajawazito kwa lengo la kujuwa maendeleo yao na kujikinga na matatizo yanayoweza kujitokeza.

Nae Mratibu wa Mradi wa kuendeleza utetezi kwa vyombo vya habari juu ya Afya ya Uzazi kwa wanawake na wasichana kutoka TAMWA,ZNZ Zaina Abdalla Mzee amesema  ziara hiyo ya kutembelea vituo vya Afya ina lengo la kugundua changamoto na kuziwasilisha kwa wahusika na kupatiwa ufumbuzi.

“Tunafanya ziara hii kwa lengo la kuvijuwa vituo vya Afya na vinavyotoa huduma Rafiki kwa Vijana vilivyopo Wilaya ya Magharibi “B” na Kati kujuwa changamoto zinazovikabili vituo hivyo na kutafutiwa ufumbuzi kwa wahusika,” Zaina Abdalla Mzee, Mratibu wa kuendeleza utetezi kwa vyombo vya habari juu ya Afya ya Uzazi kwa wanawake na wasichana kutoka TAMWA,ZNZ.

 

Afisa muelimishaji na  muhamasishaji kwa vijana kutoka Wizara ya Afya Zanzibar, Kitengo Shirikishi cha Afya ya Uzazi mama na mtoto  Fatma Ussi Yahya anasema wanatoa elimu kupitia vyombo vya habari kwa mama wajawazito kuhudhuria clinic mapema kwa kujuwa maendeleo yao na changamoto zinazowakabili ili kuzitatuwa mapema.

“Sisi tunahamasisha vijana kupima Afya zao na muitikio ni mkubwa, kwa sasa Chanagamoto za uhaba wa vipimo vya kupimia virusi vinavyosababisha Ukimwi (HIV KITS) la muda mrefu kiasi kwa Wilaya zote kwa Pemba na Unguja,” Afisa muelishaji na muhamasishaji vijana kutoka Wizara ya Afya, Fatma Ussi Yahya.  

Mradi wa kuendeleza utetezi kwa vyombo vya habari juu ya Afya ya Uzazi kwa wanawake na wasichana wa mjini na vijijini unafanywa kwa Wilaya ya Kati na Magharibi “B” kwa Uguja na Chake chake kwa Pemba unatekelezwa na TAMWA.ZNZ kwa ufadhili wa Wellspring Philanthropic Fund(WPF) ya Marekani.

                                                   MWISHO  

      

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch