Skip to main content

DK. MWINYI ATOA RAI KWA WASIO WATANZANIA




 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Hussein Ali Mwinyi amewataka  Wananchi  ambao sio raia halali wa Tanzania kufika katika   Ofisi za Uhamiaji kwa lengo la kujiorodhesha ili waweze kutambulika rasmi katika nchibya Tanzania. 

Aliyasema hayo wakati wa kukabidhi vyeti vya Uraia Tanzania kwa Tajnisi hoko ikulu katika Mkoa wa Mjini Unguja, ambapo alisema baaadhi ya wanachi wanashi  Tanzania bila ya utambulisho wowote .

 "Nawaomba Wananchi  ambao kwa namna moja au nyengine hawajafika kwenye Ofisi za Uhamiaji kujiorodhesha, ni vyema wakaitumia fursa hiyo ili waweze kutambuliwa rasmi. Serikali zetu zimedhamiria kulimaliza tatizo hili kutokana na athari zake." alisema Dk Mwinyi

Pia alisema Jumla  ya wananchi elfu tatu mia tatu na kumi na tisa  3,319 wamekabidhiwa vyeti vya uraia wa Tanzania tajnisi Ikiwemo Msumbiji,Comoro,Burudi na Ruwanda.

"Kwa hakika, nchi, yetu leo inaandika historia mpya ya kulikamilisha jambo hili kubwa la kuwapa uraia ndugu zetu ambao tumekuwa tukiishi nao kwa zaidi ya miaka 50 sasa wakiwa na asili ya mataifa jirani ya Burundi wakiwa raia watano  5 , raia wa Comoro mia moja na aroubaini na saba  147, raia wa Msumbiji thalathini na mmoja elfu miamoja na kumi na sita  3116 na raia wa Rwanda 1". alisema dk Mwinyi

Pia ametoa  shurkan kwa Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi na Jeshi  la uhamiaji  kwa kuhakikisha linasimama na timia  zoezi hilo

" Natoa shukurani kwa Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na Jeshi la Uhamiaji kwa namna walivyolishughulikia na kulisimamia jambo hili hadi leo tumefikia hatua ya kuwakabidhi vyeti vya Uraia ndugu zetu hawa." alisema Dk Mwinyi

" Kwetu sisi Serikali zote mbili tumefurahia sana kuona kuwa hatimae suala hili limekamilika kama ambavyo binafsi nilitoa ahadi ya kulishughulikia baada ya kuingia madarakani mwaka 2020. Leo napata faraja kuona kuwa dhamira njema ya Serikali na ndoto ya muda mrefu waliyokuwa nayo ndugu zetu hawa, imeweza kutimia ambapo kumalizika kwa zoezi hili kuna wafanya tuwatambue kuwa Raia wa Tanzania badala ya Wahamiaji wasiohamishika." aliongezea Dk Mwinyi



.Aidha alisema ni vizuri kushirikiana kwa pamoja katika kuleta amani ya nchi bila kuleta vurugu kwa lengo la kutopoteza hadhira ya serekali.

"Matumaini yangu  kuwa mtaipata heshima inaystahili hadhi ya kuwa raia  raia wema,Kwa hakika ndugu zangu mna wajibu wa kuendeleza utiifu wenu wa sheria na kujiepusha na vitendo viovu ili msipotoshe dhamira njema ya Serikali ya kukupeni uraia wa Tanzania. Kwa pamoja tushirikiane katika kulinda na kudumisha amani tuliyo nayo kwa faida yetu tuliopo sasa na wale watakaokuja baadae." alisema  Dk Mwinyi

"Hivi sasa mataifa mbali mbali duniani yanaendelea kuimarisha sheria zao za uhamiaji na uraia kwa lengo la kudhibiti uingiaji, ukaaji na utokaji wa watu ili kulinda mipaka na kuhakikisha amani na usalama katika mataifa yao." alieleza Dk Mwinyi

Aidha ametoa  wito kwa Idara ya Uhamiaji lenye dhamana ya masuala ya uhamiaji nchini, kuendelea kuziimarisha sheria zilizopo hususan Sheria ya uraia wa Tanzania. Sheria hii haijafanyiwa mapitio kwa kipindi kirefu, hivyo huu ni wakati mwafaka wa kuiangalia upya kwa madhumuni ya kuiwezesha kukabiliana na changamoto mbali mbali zinazowahusu wananchi na wageni wanaofika hapa nchini.



Naye Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Hamad Yussuf Masauni alisema kutokana na busara za viongozi ,Raisi wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Hussein Ali Mwinyi Pamoja na Raisi waJamuhuribya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluh Hassan wameamua kuwasamehe zaidi ya bilioni 6 waliotakiwa kulipa na kupewa uraia bure.

" Serekali ya Mapinduzibya Zanzibar pamoja na Serekali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa msamaha kwa raia hao kwasababu walitakiwa kulipa zaidi ya bilioni sita 6 kwa kukaa hapa bila ya kutambulika na imeamua kuwapa uraia bure bila ya harama yoyote. " alisema Haji yussuf 

 

  Naye Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anne Peter Makakala alisema   jumla ya wahamiaji wasiohamishika elfu tatu na mia tatu na kumi na tisa 3319  wakiwemo wanaume 676, wanawake 968 na watoto 1675 walikizi vigezo vya kupatiwa uraia wa Tanzania wa TAJINISI.

Vilevile amesema serikali zote mbili zimeridhia maombi hayo kwa sharti la kukamilisha taratibu za uraia kwa mujibu wa kanuni ya Tanzania ya 2017.



Pia alisema   wameanzisha mfumo wa kielektronik uliotengenezwa kwa wataalam wa ndani kwa ajili ya kutengeneza vyeti hivyo ili kuepusha udanganyifu na kutunza kumbukumbu za Wahamiaji ao.

Akitoa shukrani kwa niaba ya raia waliopatiwa vyeti hivyo  Dkt.Miraji Issa Saleh wameeahidi watakuwa waaminifu na kutii sheria zilizopo ili kwa lengo la kuleta maendeleo ya nchi amewataka  watu wengine wajitokeze ili watambuliwe.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch