Skip to main content

WANAFUNZI, WAALIMU SKULI YA UWELENI KUSAHAU SHIDA YA MAJI

 



HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@

WANAFUNZI 771 wakiwemo wanawake 354 na wanaume 417 pamoja na walimu skuli ya sekondari ya Uweleni wameondokana na huduma ya maji isiyokuwa ya uhakika, baada ya kukamilishiwa ndoto yao ya kuchimbiwa kisima.

Kisima hicho chenye urefu wa mita 70 ambacho kitakuwa na uwezo wa kujaza 22,000 kwa saa mbili kimechimbwa na shirika la usaidizi wa moja kwa moja  Afrika ‘Direct Aid Association’.

Kisima hicho pamoja na kuwanufaisha wanafunzi, tayari huduma hiyo imeshawanufaisha wanafunzi 768 wakiwemo 205 wa skuli ya maandalizi ya Uweleni na 563 wa madarasatul Nurudhalami pamoja na wanajamii wa shehia ya Uweleni.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhiwa kisima hicho Msaidizi Mwalimu mkuu wa skuli hiyo Khamis Mohamed Ussi alisema, kuwepo kwa huduma hiyo ya kudumu skulini hapo, ni tunu haikuwepo kwa zaidi ya miaka 90 tokea kuanzishwa kwa skuli hiyo.

Alisema skuli hiyo, tokea kuanzishwa kwake mwaka 1931 haikuwa na huduma ya uhakika ya maji, kutokana na kutegemea huduma inayozalishwa na Mamlaka ya maji ZAWA, ambayo hayakuwa yakiwatosheleza.

 “Wakati mwengine  wanafunzi wetu walishindwa hata kujifunza kwa ufasha, kutokana na kukosa kwa huduma ya maji ya uhakika na leo( jana), kupatikana kwa kisima hiki kimetimiza ndoto zetu skulini hapa,’’alifafanua.

 Aidha Mwalimu huyo alisema kuwa, watatimiza malengo ya mradi huo, ikiwemo kusaidia upatikanaji wa maji kwa jamii inayowazunguka.



 Kwa upande wake Mwalimu mkuu skuli hiyo Othman Khamis Amour na Mwenyekiti wa skuli hiyo waliwataka walimu, wanafunzi na jamii iliyozunguka skuli hiyo, kuithamini na  kuilinda miundombinu hiyo, ili waweze kutumia wao na vizazi vijavyo.

Walisema, iwapo watafanya uharibifu wa aina yoyote ile, hawatoitendea  haki miundombinu hiyo, pamoja na waliotowa msaada huo, jambo ambalo litakwenda kinyume na malengo yaliyokusudiwa.

“Maji ni uhai na ndio maana tulikuwa na shida pale ilipofikia hatua ya maji ya ZAWA hayatoshelezi, sasa basi kisima hichi ni cha kwenu mnapaswa kukienzi,’’walisema.

Akikabidhi kisima hicho Mkurugenzi wa Shirika la Afrika Direct Aid Association’ upande wa Zanzibar Mohamed Said Othman, alihimiza kutoa sadaka kwa wenye uwezo, kwani kutawatatulia changamoto zinazowakabili maskini.

Alifahamisha kuwa utowaji wa sadaka haumnufaishi mpokeaji pekee, kama wengi wanavyofikiria, bali hata mtowaji, nae ana malipo yake.

Hata hivyo aliutaka uongozi wa skuli hiyo, kuandaa mikakati thabiti na endelevu, ili kuhakikisha kisima hicho kinatoa huduma kama ilivyokusudiwa.



Akisoma taarifa ya kitaalamu mkandarasi wa ujenzi huo kutoka kampuni ya Takdir Drilling Patnaship Salum Mbarouk Salum alisema, kisima hicho kina urefu wa mita 70 kwenda chini, ambacho kina uwezo wa kujaza lita 22,000 kwa masaa mawili.

Mradi wa uchimbaji wa kisima hicho, ambao umegharimu shilingi milioni 35, unakusudia kuwaondoshea shida ya huduma ya maji safi na salama, wanafunzi, waalimu na wanajamii wa shehia ya Uweleni wilaya ya Mkoani.  

             Mwisho.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch