Skip to main content

RC MATTAR: ATAJA SABABU WANANCHI KUITILIA MASHAKA MAHKAMA

 



NA ZUHURA JUMA, PEMBA:

 

MKUU wa Mkoa wa Kusini Pemba Matar Zahor Masoud amesema, wananchi wanashindwa kujua wajibu wao na badala yake wanailalamikia mahakama kwamba haitendi haki.

 

Alisema kuwa, ipo haja ya wananchi kushirikiana na mahakama katika kutoa ushahidi na kuacha tabia ya kulalamika kwamba mahakama hazitendi haki.

 

Akizungumza wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya sheria yaliyofanyika katika Uwanja wa Tenis Chake Chake, alisema kuwa bila ya ushahidi hakimu hawezi kumtia hatiani mshitakiwa, hivyo juhudi zinahitajika katika kutoa ushahidi ili keshi zipate hatia.

 

"Kwanza tuzisimaie kesi zetu vizuri, tuzifiatilie na tutoe ushahidi, hii itasaidia kesi kupata hukumu, lakini ikiwa tunakaa tu hatufiki mahakamani baadae analalamika sio sahihi", alisema.

 

Aidha alisema, mfumo wa huduma ya haki mtandao watakaotumia mahakama utarahisisha usikilizaji wa mashauri, jambo ambalo litasaidia upatikanaji wa haki kwa haraka.

 

Kwa upande wake Jaji kutoka Mahakama Kuu Zanzibar Abdulhakim Ameir Issa alisema kuwa, ukuaji wa tehama duniani unarahisisha ukuaji wa uchumi kwani inasaidia kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato na ndio maana na wao wakaamua kutumia haki mtandao kwa kukuza uchumi na ustawi wa jamii.

 

"Mfumo wa tehama ni mzuri kwani utawaimarishia katika mfumo mzima wa uendeshaji kesi na wananchi watapata haki zao kwani huduma zitaimarika", alisema. 

 

Mwakilishi kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Jecha Vuai Jecha alieleza kuwa, lengo la siku ya sheria ni kuisaidia jamii kupata uelewa wa sheria pamoja na kupata haki stahiki.

 

"Ili kwenda sambamba na mahitaji ya sasa, Serikali imerahisisha huduma za kijamii na upatikanaji wa haki, kujenga mazingira wezeshi kwa wananchi, lengo ni kuona wanapata haki zao", alieleza.

 


Nae Wakili Mbobevu kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka Pemba Ali Haidar Mohamed alifahamisha kuwa, huduma za mtandao zitaweza kujenga imani kwa wananchi, kupata haki, kuongeza mapato na kuimarisha utendaji ambao utaondoa mianya ya rushwa.

 

Akisoma risala ya Chama Cha Wanasheria za Zahran Mohamed Yussuf alisema kuwa, miongoni mwa majukumu yao ni kurekebisha jamii, kusimamia haki na kutekeleza majukumu ya kazi pasi na ubaguzi, jambo ambalo linasaidia upatikanaji wa haki kwa urahisi.

 

Maadhimisho hayo ya siku ya sheria yamefanyika katika Uwaja wa Tenis Chake Chake Pemba, ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni 'HAKI MTANDAO KWA KUKUZA UCHUMI NA USTAWI WA JAMII'.

 

              MWISHO.

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch