Skip to main content

INTERNEWS, TAMWA- ZANZIBAR ZAUNGANA KUSAKA SHERIA MPYA YA HABARI ZANZIBAR

 




NA HAJI NASSOR, PEMBA::

KUMBE masuala ya haki za binadamu, yalianza kuingizwa katika mikataba mbalimbali ya kitaifa mwaka 1950.

Na kwenye Azimio la kulinda Haki za Binadamu Ulimwenguni lilifikiwa mwaka 1984 na Afrika mwaka 1981.

Baada ya hapo, mikataba ya kikanda ilipitishwa, kwa dhamira ya kutoa ulinzi wa haki za kiraia na kisiasa, haki za kiuchumi, kijamii na kiutamaduni, kwa ufanisi zaidi.

Maazimio mbali mbali, yaligusia juu ya suala la uhuru wa maoni na kujieleza, likiwemo azimio la ‘UDHR, katiba ya Zanzibar ya  mwaka kifungu cha 18 (1) na (2) kama nayo imeeleza:

“Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta kupokea na kutoa habari na dhana kupitia chombo chochote, bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati”

Hata kifungu cha (2) ‘’kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbali mbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shuhuli za wananchi, na pia juu ya masuala muhimu kwa jamii”

Zipo sheria nyingi kwa namna moja ama nyingine, zinaathiri uhuru wa habari na haki ya kujieleza kwa mfano sheria ya Usalama wa Taifa, Sheria ya Baraza la Wawakilishi, Sheria ya Takwimu, Sheria ya Makosa ya Mtandaoni.

SHERIA YA MAGAZETI ZANZIBAR

Sheria ya Usajili wa Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu namba 5 ya mwaka 1988 kama ilivyorekebishwa na sheria namba 8 ya mwaka 1997, ambapo sheria hii imekua na mapungufu mengi, yanayokwamisha haki ya uhuru wa vyombo vya habari na uandishi wa habari Zanzibar.

 

Kwa mfano kifungu cha 27(1),(2) na (4) kinachoelezea uwezo wa kukamata magazeti na kupekua majengo.

 

Kifungu kidogo (1) ofisa yeyete wa Polisi anaweza kukamata gazeti lolote, popote litakapoonekana, lililochapwa au kuchapishwa, au ambalo kwa maoni yake atalituhumu kwamba limechapwa au kuchapishwa, kinyume na sheria hii.

 

Kifungu kidogo(2) hakimu yoyote anaweza kwa hati, kumruhusu ofisa yoyote wa polisi wa cheo cha mkaguzi au cheo cha juu yake, akiwa na msaada au bila ya msaada, kuingia na kuepuka sehemu yoyote ambayo kwa maoni yake anadhani kwamba limo gazeti lililochapwa kinyume na sheria hii.

 

Aidha kifungu kidogo (4) gazeti lolote lililokamatwa chini ya kifungu litapelekwa haraka iwezekanavyo kwa hakimu, ambaye anaweza, ikiwa atajitosheleza kwamba gazeti lilichapwa au kuchapishwa kinyume na sheria hii.

 

INTENEWS/ TAMWA –ZANZIBAR ZINAFANYA NINI?

Chama cha Waandishi wa habari Wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar kwa ufadhili wa Shirika la Internews, kwa sasa wapo katika kufanyia uchechemuzi wa sheria hiyo, katika vifungu mbali mbali ambavyo ni kandamizi, ili kuweze kupatikana kwa sheria mpya.

 

Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, anasema kuna baadhi ya vifungu katika sheria ya hiyo vimekua sio rafiki kwa waandishi wa habari, hali inayopelekea baadhi ya waandishi kufanya kazi kwa woga.

“TAMWA imekua ikikutana na wadau mbali mbali wa habari kujadili, mapungufu yaliyomo ndani ya sheria hiyo na kutoa maoni yao, ili mwisho wasiku maoni hayo yawasilishwe na kuwa na sheria rafiki kwa waandishi,”amesema.



Mratibu wa Internews Tanzania ofisi ya Zanzibar Zaina Mzee, anasema wameamua kuunga za pamoja na TAMWA-Zanzibar ili kuhakikisha Zazibar inakuwa na sheria bora.

Anasema, mwelekeo hasa ni kutaka kufutwa kwa sheria hiyo Magazeti pamoja na ile ya Tume ya Utangaazaji nambari 7 ya mwaka 1997, ili Zanzibar kuwe na sheria moja.

‘’Ndio maana Internews hailali, iko huku na kule, kuhakikisha sekta ya habari Zanzibar inaongezewa thamani kwa kuwepo kwa sheria rafiki,’’anasema Mratibu huyo.

Hapa akaongeza kuwa, anawategemea sana waandishi wa habari na wadu wao, ili kuona wanaviibua na kuvisemea vifungu kandamizi kwa uhuru wa habari.

‘’Suala la kupata, kusambaaza habari lipo kikatiba zaidi, sasa kama sheria imetungwa inakinzana na haki hiyo, haina nafasi kwa sasa,’’anasema.

WAANDISHI WA HABARI WENYEWE

Berema Suleiman Nassor, wa Zenj Fm redio Unguja, anasema kifungu hicho kinapaswa kufanyiwa marekebisho ya haraka, kwani kinampa mamlaka makubwa polisi wakati zipo taasisi za kihabari zinazopaswa kusimamia kitu hicho.

 

Kuwepo kwa mamlaka hayo kutapelekea waandishi, wauzaji, wasambazaji na makampuni kuwatia hofu kila wakati kuhofia kukamatwa.

 

Jabiri Idrissa kutoka Mwanahalisi mtandaoni, anasema tasnia ya habari, inaenda kuwa mhimili wa nne usio rasmi, kumpa mamlaka polisi au chombo chengine sheria kwenda kufanya upekuzi au kuwadhalilisha waandishi.

 

“Kama kuna mamlaka inahisi gazeti limeaandika vibaya au limekwenda kinyume na sheria za habari, vizuri kufuata taratibu za kisheria na sio kuwakamata moja kwa moja au kuwavamia.

 

Mwandishi wa habari kutoka Gazeti la Zanzibarleo Pemba Habiba Zarali Rukuni, anasema mamlaka hayo kwa ofisa wa Polisi, anaweza kukamata gazeti atakapojisikia tu kukamata na sio kwa kufanya kosa.

 

Meneja wa radio Jamii Mkoani Said Omar Said, anasema sio sahihi kwa ofisa Polisi kupewa mamlaka hayo, kwani uhuru wa habari utakuwa bado haujakuwepo nchini.

 

“Kama mwandishi amegombana na afisa wa polisi, mitaani na ubarabarani si anaweza kuutumia ugomvi huo kuja kufanya upekuzi na kusababisha sito fahamu kwa waandishi na chombo cha habari.”amesema.

 


WADAU WA HABARI

Katibu wa Jumuiya ya Waandishi wa Habari Pemba PPC Ali Mbarouk Omar, aliwahi kusema kuwa, vifungu vya sheria hiyo haviko sawa na vinakandamizi mno tasnia ya habari, kwa kutoa mamlaka ya moja kwa moja kwa vyombo vya ulinzi.

 

Mkurugenzi wa KUKHAWA Pemba Hafidh Abid Saidn, anasema uwezo uliopo katika kifungu ni mkubwa na unanyima uhuru wa waandishi wa habari na taasisi zao kufanya kazi zao ipasavyo.

 

“Hii sheria inaonekana ni kongwe sana na imeshapitwa na wakati, sasa ni wakati wa maendeleo lazima sheria hii ifanyiwe mabadiliko makubwa ili iweze kuendana na mabadiliko yaliyopo,”amefahamisha.

 

Mratibu wa TAMWA Pemba Fat-hiya Mussa Said, anasema Mamlaka ya Polisi ni kulinda raia na mali zao na amani ya nchi, hivyo mamlaka yaliomo katika kifungu 27 kifungu kidogo (1)(2) na (4) yanapaswa kufanyiwa maboresho.

 

“Kitakapoboreshwa kifungu hicho, waandishi watakuwa huru kufanya kazi zao za kihabari na wananchi watapata habari, uhuru wa kutoa maoni na kujieleza", anasema.

 

Khalfan Amour Mohamed ambae ni mwanasheria, anasema kifungu cha 27 kifungu kidogo (1) hakipo sawa na kinanyima uhuru wa habari kwa waandishi na taasisi ya kihabari.

 

“Kichekesho zaidi anaposema ‘kwa maoni yake’ neno hili halitakiwi liwepo kisheria na kupewa mamlaka makubwa Polisi,’’alieleza.

 

Anasema kifungu kidogo (2) kinaenda kinyume na vifungu vya sheria nyengine, ambazo zinaelekeza namna ya kufanya upekuzi na ukamataji wa vitu vinavyodhaniwa kuwa ni makossa.

 

Anafafanua kuwa, sheria ya Mwenendo wa makosa ya jinai Zanzibar namba 7 ya mwaka 2018, na Sheria ya Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na madawa ya kulevya Zanzibar, zimeweka utaratibu wa kufanyika upekuzi.

 

Naye Afisa Sheria kutoka Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar Ofisi ya Pemba Bakar Omar Ali, anasema kifungu hicho hakipo sawa na kinahitaji kufanyiwa marekebisho.

Mhariri Mtendaji wa Shirika la Magazeti ya Serikali Zanzibar Ali Haji Mwadini, anasema sheria inayonyima uhuru wa waandishi wa habari kufanya kazi zao vizuri na kikamilifu, haijengi.

 

Mjumbe wa Kamati tendaji kutoka Pemba Press Club Gaspary Charles, amesema sheria kumpa nguvu ofisa wa polisi uwezo wa kukamata na kufanya upekuzi, ni kipimo kikubwa cha ukiukwaji wa uhuru wa habari nchini.

 

Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania(MCT) Kajubi Mukajanga, anasema waandishi wasipozieleweka sheria zao, mchakato wa kupitisha utakuwa kwenye mikono ya wanasheria na wanasiasa na hivyo watapendekeza wanavyotaka.

 

Asha Khamis Juma na mwenzake Tatu Abdalla Msellem, wanasema jamii kwa kiasi kikubwa inavitegemea vyombo vya habari kuweko huru na kuwaibulia mambo wasiyoyaona.

 


Mchambuzi wa sheria za habari Zanzibar Imane Duwe, anasema wakati wa Zanzibar sasa kuachana na sheria kandamizi umekwisha.

MWISHO

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch