Skip to main content

WAZIRI RAHMA ABAINISHA CHANZO CHA MIGOGORO YA ARDHI ZANZIBAR

 






Na Sabiha Keis, Zanzibar

Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar Rahma Kassim Ali amesema ongezeko la migogoro ya Ardhi nchini linasababishwa na baadhi ya wananchi kununua Ardhi kwa kutofuata sheria na taratibu zilizowekwa.

Kauli hiyo ameitoa mara baada ya kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Bajeti kwa kipindi cha Julai hadi Disemba 2022 kwa kamati ya Mawasiliano,Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilishi huko katika ukumbi wa Wizara hiyo Maisara, Unguja.

“Asilimia 80 ya migogoro ya Ardhi inatokana na mauziano ya wananchi kuuziana ardhi kinyume na sheria, na hao wanasheria ndio balaa, kiwanja kimoja kinauzwa mara mbili hata tatu, afadhali hata masheha wakihusishwa wajua kama kiwanja hichi kimeshauzwa “ Alisema Waziri Rahma.

Alieleza kwamba mbali na ununuzi huo wa Ardhi usifuata sheria lakini pia ujenzi holela usiozingatia mipaka halisi ya eneo husika umekua ukichangia kuwepo kwa migogoro hiyo ambapo Wizara yake imejipanga kwa sasa katika kudhibiti hali hiyo.

Waziri Rahma alisema Wizara ya Ardhi tayari imeshakaa vikao mbalimbali na Taasisi zinahusiana  na wizara yake katika masuala ya Ardhi ikiwemo Tawala za Mikoa, Mamlaka ya Uwekezaji (ZIPA) pamoja na Wizara ya Kilimo na kutoka na azimio kuwa vibali vyote vya ujenzi vitolewa katika ofisi moja ili  kuondoa  changamoto iliyopo.

Aidha waziri huyo alisema taasisi yake ya Mahakama ya Ardhi imepokea kesi mpya za migogoro ya ardhi  108 kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2022 ambapo kesi 107 zilitolewa maamuzi huku kesi 183 zinaendelea katika Mahakama hiyo. Kesi hizo ni kwa Unguja na Pemba.

Akizungumzia mikakati ya Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Mngereza Mzee Miraji amefahamisha kwamba licha ya wizara hiyo kukabiliwa na  changamoto ya fedha lakini wamejipanga kutafuta washirika wa maendeleo kwajili ya  kutekeleza miradi mbali mbali ikiwemo upimaji wa ardhi, kujenga nyumba za bei nafuu na usalama wa ardhi.

“Kwanza tulikuwa na jukumu la kuwa indentify partners, kuangalia jinsi ya kujenga nyumba za low cost, land tenure security pamoja na kuangalia tuanzie wapi? ”Alisema Dkt Mngereza.



Aidha Dkt Mngereza amefahamisha kuwa katika kutatua changamoto ya ujenzi holela Wizara yake tayari imeshatiliana saini na Kampuni ya Propertie International kutoka Tanzania Bara kwa ajili ya kushirikiana katika kazi ya kupima na kupanga mji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Mawasiliano,Ardhi na Nishati  Yahya Rashid Abdalla ameipongeza Wizara hiyo kwa namna inavyofanya kazi zake pamoja na kuishauri Wizara  kuhakikisha matumizi ya Ardhi yanalingana  na mahitaji husika.

Wizara ya Ardhi na maendeleo ya Makaazi kwa kipindi cha Julai hadi Septemba 2022 ilikadiriwa kukusanya jumla ya TZS Billioni 1.168 kutoka katika vyanzo mbalimbali vya mapato ndani ya Taasisi zake ambapo hadi kufikia Disemba,2022 jumla ya TZS Millioni 700.550 zimekusanywa ambazo ni wastani wa asilimia 60 ya makadirio.

Kwa upande wa matumizi kwa kipindi julai- Disemba 2022,Wizara ilipangwa kutumia jumla ya TZS Billioni 2.956 kwa ajili ya kazi za kawaida Na mishahara ambapo hadi kufikia Disemba 2022 Wizara imepatiwa jumla ya TZS Billioni 2.718 ambazo ni wastani wa asilimia 91.9 ya fedha zilizopangwa.

Mwisho

 

 

 

 

 

 

 

 

 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch