Skip to main content

ZAFELA: TAKWIMU ZA UDHALILISHAJI MUHIMU KATIKA MAPAMBANO

 



MKURUGENZI wa Jumuiya ya  Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA), Jamila Mahmoud Juma, amesema mfumo wa  ukusanyaji wa taarifa za udhalilishaji (database), unasaidia kutambua kasi ya ongezeko au kupungua kwa matukio hayo.

 

Jamila alieleza hayo huko ofisini kwake Mpendae Mjini Zanzibar, wakati alipozungumza na mwandishi wa habari hizi, ambapo alisema mfumo huo unasaidia kuweka kumbukumbuku za matukio hayo.

 

Mkurugenzi alisema mfumo huo unarahisisha upatikanaji wa taarifa sahihi za matukio ya vitendo vya udhalilishaji kuanzaia hatua za ufuatiliaji wa kesi mpaka kufikia mahakamani kwa mashirikano na mashirika ya serikali na taasisi mbalimbali.

 

Jamila alisema tangu kuzinduliwa kwa mfumo huo mwaka 2021 na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, mfumo huo umekuwa msaada mkubwa wa kujua taarifa kwa taasisi zilizomstari wa mbele kwenye mapambano dhidi ya vitendo vya udhalilishaji.

 

“Mfumo huu ni muhimu na una faida kwa jamii katika kupata taarifa sahihi dhidi ya kesi za matukio ya vitendo vya udhalilishaji ambapo kesi hizo huripotiwa  na taasisi  zilizomo  katika mfumo huo  kama vile kituo cha huduma za sheria, wasaidizi wa sheria, Polisi na Mahakama, kwani kila mmoja kwa nafasi yake ana nafasi ya kushiriki katika uwekaji wa taarifa za matukio ya vitendo vya udhalilishaji”, alisema.

 


Akizungumzia takwimu za vitendo hivyo kupitia  mfumo huo alisema kwa upande wa ZAFELA peke yake wastani kila mwezi matukio 40 ya kesi tofauti  zikiwemo kesi za udhalilishaji,madai ya mahari,talaka na ukaazi wa mtoto  huorosheshwa kwa kuingizwa kwenye mfumo huo ingawa alisema changamoto  iliyopo  kwa  sasa, ni kwa taasisi nyengine kutoingiza taarifa za takwimu zao hali ambayo inarudisha nyuma lengo walilojipangia la kuwa na mfumo wa pamoja wa ukusanyaji wa taarifa.

 

Alielezea  sababu  zinazopelekea taasisi  hizo  kutoweka taarifa za vitendo hivyo katika mfumo huo ni  kutokana na  hofu ya usalama kutokana na unyeti wa taarifa hizo kwa kuhofia nani anazipokea? na wapi zinakwenda? Sambamba  na uhaba wa fedha kwa baadhi ya taasisi kushindwa kuingiza taarifa zao kwasababu mfumo huo unatumia gharama za kimtandao.

 

Fatma Khamis Ame ambae ni msaidizi wa sheria kutoka Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria Zanzibar (ZAPAO), alisema mfumo huo  unasaidia kurahisisha shughuli zao za kisheria kwa kutambua wajipange vipi kulingana na kesi  tofauti  za vitendo vya udhalilishaji  zinazoendelea kutokezea.

 


Kutokana na  changamoto ya mfumo huo iliyopo hivi sasa, Alitoa ushauri kwa ZAFELA kuitisha kikao cha pamoja cha  wadau wote  wanaopinga vitendo hivyo ili  kuja na Suluhisho la changamoto zinazojitokeza  kupitia mfumo huo ikiwemo changamoto ya  mfumo kudai kitambulisho  hali ambayo imekua ikiwarudisha nyuma.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch