Skip to main content

'ASI' SECURITY: 'TUTUMIENI TUKO 'FIT' KIULINZI

 




NA HAJI NASSOR, PEMBA:::

UONGOZI wa kampuni ya ulinzi ya Active Security with Integrity ‘ASI’ umeziomba tasisiza serikali na zile za watu binafsi, kuwatumia katika ulinzi wa maeneo yao mbali mbali, kwani vijana wao, wanayo mafunzo ya kutosha ya kazi hiyo.

Ushauri huo umetolewa na Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Salim Khamis Juma, wakati akizungumza hospitali ya Coteji Vitongoji wilaya ya Chake chake, mara baada ya kumalizika kazi ya usafi, iliyofanywa na watendaji wa kampuni hiyo.

Alisema, baada ya kusajiliwa rasmi serikalini na kwenye taasisi zake nyingine, sasa ni wajibu wa tasisi mbali mbali kuwatumia wao katika ulinzi.

Alieleza kuwa, tayari zipo tasisi chache wameshaanza kuwatumia, lakini kwa idadi ya vijana walionao, ni vyema na tasisi nyingine kuona umuhimu huo.







Mkrugenzi huyo alieleza kuwa, ili kufikia azma ya serikali ya ajira 300,000 zilizotangaazwa na rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi, basi ni kuwapatia ajira vijana wa kampuni yao ya ‘ASI’.

‘’Kama tasisi za serikali na zile za watu binafsi watatumia sisi katika ulinzi, ni sehemu ya kuisaidia serikali kuu, katika kuwapatia vijana ajira, kwani za serikali haiwezi kutupata ajira sote,’’alieleza.

Akizungumza suala la zoezi la usafi walilolifanya hospitalini hapo, alisema ni sehemu ya malengo ya kampuni, kushrikiana na serikali kuu katika kuimarisha usafi.

‘’Kampuni ya ‘ASI’ kufanya usafi huu ni sehemu ya kuunga mkono juhudi na mawazo ya rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, ambae ni muumini wa usafi wa mazingira,’’alifafanua.

Aidha Mkurugenzi huyo alisema, zoei kama hilo litakuwa endelevu katika maeneo mbali mbali, kwani pamoja na kazi za ulinzi, lakini suala la usafi ni kipaumbele chengine.

Katibu wa Hospitali hiyo Dk. Nassir Suleiman Hamad, alisema wazo la kampuni hiyo ya ‘ASI’ kufanya usafi katika eneo la wagonjwa, ni jambo jema mno, maana ni njia moja wapo ya kukimbiza maradhi.





‘’Kampuni hii pamoja na kwamba ni ya ulinzi, lakini kumbe inaashiria kuwa, inapenda kulinda kwenye eneo safi, na mmekuwa mabalozi wetu katika kuyakimbia magonjwa mbali mbali,’’alieleza.

Akizungumza kwa niaba ya Afisa Mdhamini wa wizara ya Afya Pemba, Daktari dhamana wa hospitali hiyo, Fahad Ali Khamis, aliiomba kampuni hiyo, kuendelea na kazi za usafi kila baada ya muda.

‘’Kampuni hii ni ya ulinzi, lakini kufanya kwenu usafi sisi hili limetuvutia, na ikitokezea bahati ya kutaka watendaji wa kudumu wa kazi hii, itakuwa rahisi kuwasiliana,’’alieleza.






Mapema mkuu Mafunzo na nidhamu wa wa kampuni hiyo ya ulinzi ya Active Security with Integrity ‘ASI’ Khamis Salim Khamis, alisema kampuni kwa sasa inafanyaka kazi zake kisheria.

Hata hivyo alieleza kuwa, pamoja na kazi hiyo ya ulinzi, imejiegemeza katika kutoa huduma bure kwa jamii, ikiwemo ya usafi, ili kuwa na taifa lenye afya bora.





Nae mlezi wa kampuni hiyo Mussa Salim Nassor, aliwapongeza vijana hao kwa kushiriki katika kazi hiyo ya kujitolea na kuwataka wasisite kila wanapoitwa.

‘’Moja ya jambo ambalo vijana wengi wamelikosa katika miaka ya hivi karibuni ni jambo la uzalendo wa kujitolea, lakini hawa kwa kampuni ya ‘ASI’ naona muko vizuri, hongereni sana,’’alieleza.

Baadhi ya vijana walioshiriki kwenye zoezi hilo la usafi, walipongeza hatua ya uongozi wao, kubuni jambo hilo, ambalo ni kuwasaidia wagonjwa kuishi kwa utulivu.






Kampuni ya ulinzi ya Active Security with Integrity ‘ASI’ ambayo imeanzishwa mwaka 2020, moja ya malengo yake ni kutoa huduma ya ulinzi, na tayari imeshaajiri vijana 12.

                    Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch