Skip to main content

WAZIRI HAROUN AIPA KAZI IDARA YA KATIBA KUSIMAMIA MAAZIMIO 16 YA JUKWAA

 



NA HAJI NASSOR, UNGUJA:::

WAZIRI wa Nchi Afisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Zanzibar Haroun Ali Suleman, ameiagiza Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria kwa kushirikiana na tasisi ya LSF, kukutana kila baada ya miezi mitatu, ili kuona maazimio 16 yaliobuliwa kwenye jukwaa la msaada wa kisheria yanafanyiwa kazi.

Alisema, Zanzibar imekuwa hodari wa kuanzisha mambo na kisha kuyaweka kwenye karatasi bila ya kufanyiwakazi, lakini kwa hayo maazimioa 16, lazima wajitahidi kuhakikisha wanayatekeleza.

Waziri Haroun ameyasema hayo Disemba 14, 2022 wakati akilifunga jukwaa la pili la Msaada wa Kisheria Zanzibar, lililoandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar kwa ufadhili wa LSF na kufanyika Chuo cha Utalii Maruhubi Unguja.

Alieleza kuwa, kila baada ya miezi mitatu anahitaji kupata ripoti ya utekelezaji wa maazimio hayo, ili kuona waliolengwa wanufaika nayo.

‘’Mhakikishe Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria kwa kushirikiana na wadau wenu LSF, na mimi nitawaita kuanzia mwezi Machi 2023 kujua mliyofanya,’’alieleza.

Aidha waziri Haroun, alipendekeza kuwa jukwaa la tatu la Msaada wa kisheria ni vyema likafanyika kisiwani Pemba, ili washiriki kutoka Unguj,a wapate kujifunza mambo mbali mbali kisiwani humo.

Alieleza kuwa, anaamini Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria kwa kushirikiana na LSF, wakikaa pamoja, wanaweza kufanikisha suala la jukwaa hilo, kufanyika kisiwani humo.

Kwa upnde wke Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar Hanifa Ramadhan Said, alieleza kuwa, katika kongamano hilo, kumeibuliwa maazimio 16.

Alieleza kuwa, moja kati ya hayo LSF kuendelea kusadiana kuwajengea uwezo watendaji wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, pamoja na kufunguliwa kwa ofisi za wasaidizi wa sheria katika ofisi ya wilaya.

‘’Kuhakikisha kuandika ripoti za utendaji kazi, kwa kugusia malengo 17 endelevu ya dunia, ili kuonesha muitikio wa jamii pamoja na kuimarisha mifumo itayohakikisha taifa linakuwa na raia wema,’’alifafanua.

Azimio jengine ni kwa Idara hiyo, kuhakikisha inachukua juhudi za kuratibu na kufanya marekesbisho ya sheria ya Msaada wa Kisheria, ili kuweka mfuko wa taifa wa Msaada wa kisheria.

Aidha Mkurugenzi huyo alisema azimio la 15 ni kuongeza kasi ya mafunzo ya usuluhishi na utatuzi wa migogoro kwa wasaidizi wa sheria.

‘’Natarajia tukikutana tena kwenye jukwaa la tatu la msaada wa kisheria hapo mwaka 2023, yawe tayari haya yameshatekelezwa kwa kadiri itakavyoamuliwa,’’alieleza.



Afisa Mtendaji mkuu wa taasisi la LSF Deogratus Bwire, alisema wamefarajika kuona kuwa, bado Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria inaendelea kushirikiana kwa karibu.

Awali wakichangia mada kwenye jukwaa hilo, Msaidizi wa sheria wilaya ya kusini Unguja Ahmed Haji Mkema, alisema wanafunzi wa sheria, baada ya kumaliza chuo, wamekuwa na uwelewa mdogo.

Hata hivyo alisema lazima kituo cha msaada wa kisheria ‘legal aid clinic’ kilichopo ndani ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kizidi kujitangaaza, ili wanafunzi wakifahamu.

Mapema akiwasilisha mada ya elimu ya saikolojia kwa wahanga wa matendo ya udhalilishaji, wakili Ali Rajab, alisema lazima wasaidizi wa sheria, wajifunze elimu hiyo.

‘’Inawezekana kuna mtoto ameshadhalilishwa na hakuna hata kesi yake moja iliyopata hatia, sasa saikoloji yake ni mtu wa kudhalilishwa, na hasikii tena elimu, ushauri wala msaada wa kisheria,’’alifafanua.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ Harusi Miraji Mpatani, akichangia mada alisema, vyama vya wanasheria, lazima viongeze nguvu, ili jamii ipate msaada.

Alieleza kuwa, msaada wa kisheria umewalenga wale watu maskini zaidi, hivyo lazima viongozi wa vyama na wale wanasheria, wanawasaidie wananchi.





‘’Hapa mawakili wa kujitegemea, lazima sasa tujitolee kuzisimamia kesi bila ya kujali malipo ‘probono cases’ na huo ndio mchango wetu kwa jamii,’’alishauri.

Nae mdau wa sheria Sabaha Bakar Hassan, amesema bado elimu inahitajika kwa jamii, ili kufahamu vyema, dhana ya msaada wa kisheria.  

Nae sheha wa shehia ya Chumbuni Hassan Juma Juma, aliwataka mawakili kuanzisha utamaduni kama wa kukutana na wananchi ngazi ya kijiji, ili kutoa elimu kwao.

Hata hivyo Afisa sheria wa Vyuo vya mafunzo Zanzibar, Seif Maabad Makungu, amewshauri mawakili wasiziache kesi njiani, ambazo wameshalipwa na watuhumiwa.


Hili ni jukwaa la pili la msaada wa kisheria Zanzibar, kuandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria kwa kushirikiana na LSF, ambapo ujmbe wa mwaka huu ni uimarishaji wa huduma bora na endelevu za utoaji wa msaada wa kisheria Zanzibar.

                        Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch