Skip to main content

WATU WENYE ULEMAVU WAIPA NENO WIZARA YA AFYA PEMBA

 



NA ZUHURA JUMA, PEMBA:


WATU wenye ulemavu kisiwani Pemba wameiomba Serikali kupitia Wizara ya Afya kuweka kitengo maalumu cha kuwapatia huduma, ili kuepuka usumbufu wanaoupata wakati wanapofika kutaka huduma za matibabu.

Walisema kuwa, wameona kwamba kuna vitengo mbali mbali vimewekwa ikiwemo vya Ukimwi, kitengo cha maradhi ya macho, viungo, kifua kikuu na vyengine, ingawa wao hawajatengewa, jambo ambalo linawapa usumbufu wakati wanapofika hospitali.

Walieleza kuwa, ipo haja kwa Wizara husika kuwawekea kitengo chao maalumu ambacho kitakuwa kina mahitaji yote ya watu wenye ulemavu, ikiwemo kuweka miundombinu imara ya ufikiaji, wakalimani pamoja na madaktari ambao watakuwa wanajua lugha za alama.

Wakizungumza katika kongamano la Watu Wenye Ulemavu ambalo liliwashirikisha wadau mbali mbali, walieleza kuwa wanapoifuata huduma ya afya wanateseka sana, hivyo watakapowekewa kitengo chao wataondokana na usumbufu ambao wanaupata.

“Kitengo ni muhimu kwetu kwa sababu tutakuwa na ‘one stop center’ yetu ambayo itakuwa na huduma mbali mbali zinazoendana na hali yetu tuliyonayo”, walisema.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wenye ulemavu Pemba (JUWAUZA), Hidaya Mjaka Ali alisema, changamoto kwenye huduma za afya bado zipo, ikiwemo za ufikiwaji, ukosefu wa wakalimani pamoja na madaktari kutokujua lugha za alama.

“Tunakumbana na changamoto mbali mbali wakati wa kuitafuta huduma ya Afya ikiwemo huduma ya ufikiaji, ukosefu wa wakalimani pamoja madaktari kutokujua lugha za alama, hivyo tunapofika tunazubaa zubaa”, alisema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wasioona Pemba (ZANAB) Suleiman Mansoor Suleiman alisema kuwa, wasiiona hawana wasimamizi wakati wanapofika hospitalini au vituo vya afya, hivyo huzubaa tu na wakati mwengine hurudi bila kupata huduma.

“Tutakapowekewa kitengo ,tunapofika tutapatiwa huduma kwa urahisi na haraka zaidi, kwani tunaamini kuwa kutakuwa na mambo yote ambayo yanastahiki tuwe nayo”, alieleza.

Nae Ofisa Maendeleo ya Jamii kutoka MECP-Z Pemba, Haji Ali Hamad alisema, wamekuwa wakifanya mikutano na makongamano mbali kwa lengo la kuhakikisha kwamba changangamoto za watu wenye ulemavu zinatatuliwa na wanapata huduma stahiki.

“Madrasa inafanya kila juhudi kuona kwamba watu wenye ulemavu wanapata haki, fursa na huduma sawa na watu wengine, ili wasijisikie unyonge, kwa sababu mpaka sasa bado wanaona wanatengwa na jamii”, alisema Ofisa huyo.

Aliitaka jamii kuacha kuwanyanyapaa watu wenye ulemavu na badala yake wawape mashirikiano ili kuona kwamba wanapata haki zao za msingi na huduma stahiki.

                                                         MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch