Skip to main content

MAKAMU WA PILI AWAPA NENO WASAIDIZI WA SHERIA ZANZIBAR AKIFUNGUA JUKWAA LA PILI

 

 


NA HAJI NASSOR, UNGUJA

MAKAMU wa Pili wa Rais Zanzibar Hemed Suleiman Abdullah, amewataka wasaidizi wa sheria na watoa msaada wa kisheria kuendelea kufanya kazi zao kwa uweledi, na hasa kuelekeza nguvu zao, katika mapambano ya udhalilishaji, rushwa na dawa za kulevya.

Alisema, bado jamii inakabiliwa na changamoto hizo, hivyo ni wajibu wao kuendelea kutumia weledi wao, ili wananchi waishi kwa salama, bila ya kuwa na changamoto hizo.

Makamu huyo wa Pili, ameyasema hayo leo Disemba 13, 2022 ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi mjini Unguja, kwenye jukwaa la pili la msaada wa kisheria Zanzibar, lililoandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar.

Alisema, serikali inayoongozwa na Dk. Mwinyi inaelewa kazi inayofanywa na wasaidizi wa sheria, hivyo lazima wazidishe kasi na juhudi za kuhakikisha wanaifikisha elimu hiyo kwa jamii.



Makamu huyo wa Pili alisema, serikali itaendelea kuwa karibu mno na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, ili kuona wanafanikisha malengo yao, ya kuifikia jamii.

‘’Muelewe kuwa kazi hii ya utoaji wa masaada wa kisheria ni kazi ya kujitolea, na malipo yenu ni kwa Muumba zaidi, hivyo endeleeni kuwasaidia wananchi wanyonge, ili wapate haki zao kisheria,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Makamu huyo wa Pili, alisema yuko tayari kuusaidia mfuko wa msaada wa kisheria, mara utakapoanzishwa, ili kuhakikisha unasaidia kusukuma mbele utoaji wa msaada wa kisheria.

‘’Mheshimiwa Waziri, mimi naunga mkono uanzishwaji wa mfuko huo,  na niko tayari hata mshahara wangu mmoja kuweka, na naamini na wengine watasaidia,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Makamu huyo wa Pili ameipongeza Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, kwa juhudi zake za kuhakikisha, wanaielewesha jamii, wajibu na haki zao kisheria.

‘’Juzi nilitembelewa na mwananchi mmoja, ambae ni mnyonge na ameelezea kupata haki zake, akisema waliomsaidia ni wasaidizi wa sheria, tena bila ya malipo, hongereni kwa hili,’’alieleza.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi Afisi ya Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Zanzibar Haroun Ali Suleiman, ameiagiza Tume ya Kurekebisha sheria Zanzibar, kuifanyia marekebisho sheria y msaada wa kisheria Zanzibar no 13 ya mwaka 2018.



‘’Ushauri wa wenzetu wa tasisi ya LSF kuwa sasa sheria yetu tuifanyie marekebisho, ili itambuwe uwepo wa mfuko wa maalum wa msaada wa kisheria, kama ilivyo kwa wenzetu wa Tanzani bara kwenye sheria yao,’’alifafanua.

Hata hivyo alisema, ni wazo zuri kuwa wasaidizi wa sheria wapatiwe ofisi ndani ya ofisi za wilaya, ili waendesha shughuli zao kwa ufanisi.

Akisoma maazimio yatokanayo na jukwaa la kwanza, Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, Zanzibar Hanifa Ramadhan Said, amesema sasa wasaidizi wa sheria wanashirikiana vyema na vyombo vya habari.

Alisema, hata wakati wa shamra shamra za siku 16 za kupinga ukatili, wasaidizi wa sheria, walivitumia vyombo vya habari kufikisha ujumbe wa kupambana na unadhalilishaji.



Alieleza kuwa, Idara pia imefanikiwa kuwaptia mafunzo ya kuwakumbushia sheria mpya, wasaidizi wa sheria, ili waendane na kasi ya utoaji huduma.

Nae Afisa Mtendaji Mkuu wa taasisi ya ‘LSF’ Lulu Mwanakilala amesema kutakuwa na mfuko wa msaada wa kisheria, ambapo serikali na wadau, ndio wenye jukumu la kuutunisha.

‘’Kwa mfano Tanzania bara, kwenye sheria yao jambo hilo limo, hivyo ni wakati wa Zanzibar, kufanya marekebisho ya sheria msaada wa kisheria namba 13 ya mwaka 2018, ili kuingiza kipengele hicho,’’alisema.

Hata hivyo alisema, kwa mwaka wa fedha ujao, watazidisha kasi ya kushirikiana na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar.



Aidha LSF imeshafanya mazungumzo na wizara husika, ili kuona wasaidizi wa sheri,a wanakuwa na ofisi kwenye majengo ya TAMISEMI, ili kupunguza gharamza kukodi.

Aidha tunataka kuona kuwa, mahakama zinatenga ofisi za wasaidizi wa sheria, kwenye vitengo jumuishi kama ilivyo kwa wenzao wa Tanzania bara.

‘’Tunaahidi kuendelea kuwa bega kwa bega katika kuwajenga uwezo watoa huduma za msaada wa kisheria, ili kutimiza matakwa ya wananchi, yanayoongezeka kwa kasi,’’alieleza  

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Zanzibar Omar Haji Gora, alisema jukwaa hilo ni utekelezaji wa sera ya mwaka 2017 na sheria ya msaada wa kisheria no 13 ya mwaka 2018.

Alieleza kuwa, LSF imekuwa karibu mno na Idara ya Katiba, Msaada wa Kisheria, katika kufanikisha majukumu yake hasa ya kuhakikisha, wananchi wanapata haki zao na ufumbuzi wa mambo ya kisheria.



Katika jukwaa hilo la siku mbili mada kadhaa zitajadiliwa ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa wa msaada wa kisheria kwa kwa watu wenye ulemvu, uimarishaji wa vituo vya msaada wa kisheria, katika vyuo vikuu, saikolojia ya jamii na upatikanaji wa msaada wa kisheria ambapo ujumbe wa mwaka huu ni ‘’Uimarishaji wa Huduma Bora na endelevu za utoaji wa msaada wa kisheria Zanzibar ‘’.

                              Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch