Skip to main content

MTANGAZAJI ITV AIBUKA MSHINDI WA JUMLA 'EJAT' 2021/2022

 


Masekepa Natisa Asangama  wa  Kituo cha Runinga  cha  ITV ameibuka Mshindi wa Jumla wa Tuzo za Umahiri wa Uandishi Habari Tanzania (EJAT) kwa mwaka 2021.

Aliwashinda wanahabari wengine watatu  – Nusra Kichongapishi  wa runinga ya mtndaoni ya TIFU , Sanula Athanas  wa  Nipashe  Herieth Makweta  wa Mwananchi.

Ansangama  alishinda tuzo mbili  – Tuzo ya Wazi na Utalii na Uhifadhi  kwa runinga.

Alitangazwa Mshindi wa Jumla wa EJAT na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye katika kilele cha tuzo hizo kwenye Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam Mei 28,2021.

Waziri  alimkabidhi  Mshindi huyo wa Jumla Tuzo, cheti  na hundi ya mfano ya kiasi cha sh. Milioni 3.

Fedha hizo zimetolewa na mshiriki kiongozi wa EJAT , Baraza la Habari  Tanzania, kumwezesha  mshindi huyo kujiendeleza kwa masomo.

Kushinda Tuzo ya Wazi  aliwashinda watangazaji wawili wa kituo cha runinga cha Star – Naishook Alais Makaseni  na  Sudi Shaaban  Ally  na kwa Tuzo ya Uhifadhi na Uhifadhi alikuwa mteule pekee.

Nusra  alikuwa mteule pekee  na kushinda Tuzo ya  kilimo na Biashara ya Kilimo kwa  vyombo vya habari vya mtandaoni na piaalishinda Tuzo ya Elimu, ambapo Athanas alishinda Tuzo ya Sayansi na Tuzo ya Haki za Bindamu na Utawala Bora na Herieth  alishindaTuzo za Hedhi Salama na Afya.

Kushinda  Tuzo ya Sayansi  na Teknolojia , Athanas  alimshinda To win  Elizabeth  Edward Kusekwa wa Mwananchi  wakati  Herieth  Makweta  alikua mteule pekee  kwa Tuzo ya Hedhi Salama na alimshinda  Khamisuu Abdallah Ali  wa  Zanzibar Leo  na Christina  Mwangakale  wa The Guardian.

 

Ephrahim Edward Bahemu wa  Mwananchi  alishinda Tuzo ya Uchumi, Biashara na Fedha  akimshinda  Francis Dhamira Kajubi wa The Guardian  na  Mariam Shaban Mbwana  wa Mwananchi.

Michezo na Utawala  Tuzo yake ilitwaliwa na Maryam Salum Habib  wa  Zanzibar Leo  akimshindwa mwandishi mwingine wa gazeti hilo  Hanifa Salim Mohamed.

Kwa Radio Tuzo hiyo imeenda kwa  Said Seleman Lufune  wa City FM  aakimshinda  Adam Gabriel Hhando wa CG FM wakati  Paschal Michael  Buyaga wa TBC1 tuzo hiyo kwa runinga akimbwaga   Amour Khamis Ali  wa Zanzibar Cable TV.

Aurea Simtowe  wa  Mwananchi alishinda Tuzo ya Elimu kwa magazeti akimshinda mwandishi mwenzake  wa Mwananchi  Tumaini Msowoya  na  Abdi Juma Seleman  wa Zanzibar Leo.

Naishhoki Alais Makasemi  wa kituo cha runinga cha Star alishinda Tuzo ya Elimu .

Beatrice Philemon Mkocho  aloshinda Tuzo ya Utalii na Uhifadhi kwa magazeti  wakati Najjat Hajj Omar wa   The Chanzo – online alitwaa Tuzo hiyo kwa vyomvo vya habari vya mtandaoni.

Tuzo ya Uandishi wa Habari za Uchunguzi ilitwaliwa na  Salum Vuai Issa  wa Zanzibar Leo.

Uandishi wa Habari wa Data Tuzo  yake ilitwaliwa na Francis Dhamira Kajubi wa  The Guardian  akimshinda  Ephrahim Edward Bahemu wa Mwananchi.

Isakwisa Njole Mbyale wa Highlands FM Radio alitwaa Tuzo  hiyo kwa   Redio ambapo Khalifa Said Rashid wa  The Chanzo alishinda  tuzo kwa  vyomvo vya habari za mtandaoni akimshinda   Daniel Samson  wa   Nukta Habari Blog.

Joe Beda Rupia  wa Jamhuri alishinda Tuzo ya Utawala Bora na Uwajiobikaji kwa magazeti  ambapo  kwa runinga TRuzo hiy ilitwaliwa na   Sudi Shabaan Ally wa Star TV   na  Lukelo Francis Haule wa  The Chanzo alishinda tuzo  hiyo pia.

 

Halfan Chusi  wa Nipashe   na mwandishi mwingine wa Gazeti hilo   Sanula Athanas waliwashunda  wateule  wengine wawili   –  mfa yakazi mwenzao    Marco Zephania Maduhu  na mwandishi mwingine Hadija Rajabu kushinda tuzo  ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.

Tuzo ya Mpiga Picha Bora  kwa Magazeti  ilitwaliwa na  Sabato Mwafiri Kasika wa Nipashe wakati  Munira Abdillah Hussein  wa BBC Swahili alishinda Tuzo ya Mpiga Picha  Bora Runinga   akiwashinda Festo Charles Lumwe  wa Dar 24  na  Peter Simon Rodgers wa ITV.

Muhidini Ally Msamba  wa  The Guardian  alishinda  Tuzo ya Mchora Katuni Bora kwa  Magazeti.

Amina Ahmed Mohamed wa Zanzibar Leo aliwashinda  wanahabari wawili wa Nipashe  – Mary Geofrey Mashina na Augusta Mathias Njoji kutwaa Tuzo ya Jinsia na Watoto.

Kwa Redio Tuzo  hiyo iliendwa  kwa  Gladness Joseph Msetti wa U FM Radio ya Azam Media  akimshinda Adam Hhando wa CG FM.

Kwa vyombo vya mtandaoni  mshindi wa Tuzo ya  Jinsia na  Watoto ni Harith Jaha Ally .

Tuzo ya  kuripoti Gesi, Mafuta na Uchimbaji Madini imetwaliwa na  Joyce David Joliga  wa The Citizen  akimshinda  Elizaberth Cornery Zaya  wa Nipashe. Kwa vyombo vya habari vya mtandaoni  Tuzo  imeenda kwa  Mariam Ngollo John  wa Nukta Habari Blog.

 

Irene Nicholaus Mwasomola  wa Uhuru  alishinda Tuzo ya Kuripoti Watu Wenye Ulemavu akiwashinda  wateule wengine wawili- Habiba Zarali Rukuni  na Haji Nassor Mohamed wa Zanzibar Leo.

Tuzo ya Afya  kwa Redio imetwaliwa na Adam Gabriel Hhando wa CG FM  akimshinda  Isakwisa Njole Mbyale  Highland FM  Radio.

Jackline  Inyas Silemu wa ITV  alishinda Tuzo  ya Afya na  mtandaoni Tuzo hiyo imeenda kwa  Zuhura Hassan Makuka wa Dar 24.

Tuzo ya Hedhi Salama kwa Redio imeenda kwa Peter Lugendo John  wa  TBC FM  akiwashinda  wateule wengine wawili Jecha Simai Jecha wa  ZBC FM na Lugendo Ibrahim Madege wa UFM Radio.

Kwa  runinga  tuzo  hiyo imeenda kwa  Salma Msichoke Mrisho wa  Star TV akimshinda mfanyakazi mwenzake Omary Hussein Omary.

Baraka Jailos Messa wa  Habari Leo  alishinda Tuzo ya Ushirika  ambapo  kwa Rdio Tuzo hiyo imetwaliwa na won the Reporting Martha Stephen Nalimi wa Shamba FM.

Elizabeth Edward Kusekwa  wa Mwananchi  alishinda Tuzo ya Kundi la Wazi kwa magazeti akimshinda  Marco Zephania Maduhu.

Haji Nassor Mohamed wa  Pemba Today  alishinda  Tuzo ya Kundi la Wazi kwa  vyombo vya mtandaoni.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch