Skip to main content

LEO NI SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI, UNANAFASI GANI HAPO ULIPO?

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA:::-

MAZINGIRA ni vitu vyote vinavyotunzunguka vyenye uhai na visivyo na uhai. 

Vitu vyenye uhai, ni pamoja na mimea na wanyama, lakini visivyo na uhai ni pamoja na hewa, maji na ardhi.

 Maisha ya viumbe hai wa kizazi kilichopo na kijacho, hutegemea mahusiano mazuri kati ya watu na mazingira.

KWANINI TUYAHIFADHI MAZINGIRA?

Hifadhi ya mazingira ni juhudi zinazofanywa na binadamu, ili kuhakikisha dunia anamoishi usiharibiwe na utendaji wake, bali uweze kuwafaa watu wa vizazi vijavyo.

Tunatakiwa tutunze mazingira, kwani tukiyachafua tutapata magonjwa ya mlipuko kama vile kipindu pindu na mengine mengi.

SABABU ZA MATOKEO YA UCHAFUZI WA MAZINGIRA

Binadamu ndiye anayehusika na uchafuzi wa mazingira, na maendeleo yake ya viwanda na teknolojia na ukuaji wa idadi ya watu ni sababu zingine, zilizo wazi za kuongezeka kwa uchafuzi wa mazingira.

Katika miaka ya hivi karibuni, kwa njia hii uzalishaji wa gesi zinazochafua mazingira, uzalishaji wa taka, kukata na kuchoma misitu, unyonyaji ovyo wa maliasili, shughuli zote zinazohusiana na tasnia, madini, kilimo, biashara, unyonyaji wa mafuta.

HISTORIA YA SIKU YA MAZINGIRA

Tangu mwaka wa 1974, siku ya mazingira duniani  huadhimishwa kila mwaka tarehe 5 mwezi wa Juni, hushirikisha serikali, mashirika ya biashara, na raia ili kushughulikia masuala nyeti kabisa ya mazingira.

Kongamano la Umoja wa Mataifa la mwaka wa 1972 kuhusu mazingira ya kibinadamu mjini ‘Stockholm’ Uswis, lilikuwa kongamano la kwanza kabisa la Umoja wa Mataifa.

Na hapo neno “mazingira” kwenye anwani yake, kuundwa kwa shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) ni mojawapo ya matokeo makuu ya kongamano hili, lilianzisha mambo mengi.

UNEP iliundwa kwa urahisi kama kitengo cha Umoja wa Mataifa cha kushughulikia mazingira duniani.

Shughuli zitakazoendelezwa katika mwaka wote wa 2022 zitaangazia hatua kuu, zilizopigwa na yatakayojiri katika miongo ijayo. 



Siku ya mazingira dunia, ni sawa na siku kuu ya Umoja wa Mataifa ya kuhamasisha na kuchukua hatua za kushughulikia mazingira duniani.

Kwa miaka mingi, imekuwa jukwaa kubwa zaidi la kimataifa la kuhamasisha umma kuhusu mazingira na huadhimishwa na mamilioni ya watu kote, ulimwenguni.

MAADHIMISHO YA MWAKA 2022

Maadhimisho ya siku ya Mazingira duniani, katika mwaka 2022, yataendeshwa chini ya kaulimbiu ‘dunia moja’ na inatoa wito wa kufanyia marekebisho sera na maamuzi yetu, ili kuwezesha kudumisha usafi.

Kutochafua mazingira na kuishi kwa njia endelevu na mazingira, sayari hii ndiyo makaazi yetu tu, na ni sharti tulinde rasilimali zake zinazoweza kuisha.

‘Dunia moja’ ilikuwa kaulimbiu ya kongamano la Stockholm la mwaka wa 1972, lililopelekea kuanzishwa kwa shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP).

Miaka 50 baadaye, dunia inapoendelea kushuhudia changamoto za aina tatu duniani za mabadiliko ya tabianchi, uharibifu wa mazingira, uchafuzi na taka, mambo yanayoendelea kuhatarisha sayari yetu, kaulimbiu hii bado ina mashiko.

Lengo la 13 la malengo ya maendeleo endeleavu ya dunia mabadiliko ya hali ya hewa, yanaongeza kasi na matukio ya hali ya hewa kali, kama vile mawimbi ya joto, ukame, mafuriko na vimbunga vya tropiki.

Matatizo makubwa ya usimamizi wa maji, kupunguza uzalishaji wa mazao ya kilimo na usalama wa chakula, kuongeza hatari za afya, kuharibu miundombinu muhimu na kukatiza utoaji wa huduma za msingi.



Kuanzia 1880 hadi 2012, wastani wa joto duniani uliongezeka kwa 0.85 senti gredi, na kuwa eneo la dunia kuendelea kuwa na ukame karibu muongo mzima.

Bahari zimepata joto, kiasi cha theluji na barafu kimepungua na usawa wa bahari umeongezeka.

Kuanzia 1901 hadi 2010, kiwango cha wastani cha bahari kiliongezeka kwa sentimita 19, kadiri bahari zinavyoongezeka.

Kiwango cha barafu katika bahari ya aktiki, kimepungua katika kila muongo mfululizo tangu 1979, huku uzalishaji wa hewa ukaa duniani (CO2) umeongezeka kwa karibu asilimia 50 tangu 1990. 

Uzalishaji wa hewa ukaa haraka zaidi kati ya mwaka 2000 na  mwaka 2010, kuliko katika kila miongo mitatu iliyopita.

WADAU WA MAZINGIRA WANASEMAJE

Mohamed Khatib Khamis wa Wamba, anaemiliki mizinga ya nyuki 50, anasema uzalishaji umepungua kufuatia uharibifu na uchafuzi wa mazingira.

‘’Wanaoendesha kilimo cha mihogo na kilimo cha juu cha mpunga, unaotokana na uvunji misitu, umeathiri mfumo wa nyuki wa kupata chakula, na uzalishaji asali,’’anasema.

Mwenyekiti wa jumuiya ya uhifadhi wa mazingira Chake chake Halima Omar Mohamed, anasema kazi ya kuhifadhi mazingira wanayoifanya, imekuwa ikishambuliwa na jamii.

‘’Tukiwa kwenye maadhimisho ya siku ya mazingira duniani, kila ifikapo Juni 5 ya kila mwaka, bado jamii haijaona umuhimu wa kusaidia harakati za uhifadhi mazingira,’’anasema.

Othman Haji Kheir wa kijiji cha Tundaua, wilaya ya Chake chake, anasema hata uoto wa asili kama mikoko (mikandaa) imekuwa nayo ikishambuliwa na jamii, kwa matumizi binafsi.

Sheha wa shehia ya Ndagoni wilaya ya Chake chake Massoud Juma, anasema elimu imekuwa ikitolewa na uhifadhi wa mazingira, changmoto ni kubadili tabia.



‘’Kasi ya kuotesha miti kwa jamii hata iwe kwa siku za kitaifa bado iko chini, hali inayopelekea dunia kuizidi katika uotaji miti na hatimae msitu,’’anasema.

Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (Tanzania Forest Services Agency) ‘TFS’ ulianzishwa kisheria kupitia tangazo la Gazeti la Serikali (GN 269) la Julai 7, mwaka 2010 na kuzinduliwa rasmi mwaka mmoja baadae.

Kuanzishwa kwa wakala wa Huduma za Misitu ni kwa mujibu wa Sheria ya Wakala pamoja na Sera ya Misitu ya mwaka 1998, Sera ya Ufugaji Nyuki ya mwaka 1998, Sheria za Misitu na Nyuki Sura 323 na Sura 224 za mwaka 2002.

Lengo la 11, la kuanzishwa wakala wa Huduma za Misitu Tanzania ni uwepo wa usimamizi madhubuti na wenye ufanisi na tija wa rasilimali za misitu na nyuki.

Lakini hata kuongeza ubora na thamani ya kifedha katika kutoa huduma kwa umma, kuendelea kukuza na kuboresha uwezo wa kutoa huduma kwa umma.

Wakala umepanua wigo kibiashara na kuongeza maeneo ya uzalishaji miti na mazao ya nyuki ili kukidhi mahitaji halisi, shughuli za uwekezaji, kuboresha njia mbadala za mapato na uboreshaji wa hifadhi za misitu na nyuki kwa ujumla.

SMZ

Waziri katika afisi ya Makamu wa Kwanza wa rais Harusi Said Suleiaman, anasema ni wajibu wa kila mmoja kuyatunza na kuyahifadhi mazingira.

‘’Kuhifadhi mazingira na kuacha kuyachafua halihitaji sindikizo la kisheria, iwe ni wajibu wa kiutu kwa kila mmoja, maana faida na athari zake zinamgusa kila mmoja,’’anasema.



Kwa mwaka huu, Makamu wa Kwanza wa rais Zanzibar Othman Massoud Othman, ndie anayetarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya mazingira.

                  Mwisho

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch