Skip to main content

WADAU WA ELIMU PEMBA: WATAKA SERA IJAYO YA ELIMU IKIREJESHEE HADHI CHUO CHA UALIMU NKURUMAH

 




NA HAJI NASSOR, PEMBA

WADAU wa elimu kisiwani Pemba, wamependekeza kua sera mpya ijayo ya elimu, ilazimishe kukirejeshea hadhi na uasili wake Chuo cha uwalimu Nkurumah, ili kupata waalimu wenye sifa na uwezo zaidi wa kufundisha.

Walisema kwa sasa kuna waalimu waliosoma sana na na sio waliosomea, jambo linalochangia kushuka kwa hadhi ya elimu Zanzibar, ikilinganishwa na muongo mmoja uliopita.

Wakizungumza na waandishi wa habari katika miji ya Chake chake, Wete na Micheweni wadau hao walisema, ni vyema sera ikatambua na kukirejeshea hadhi hicho hicho cha waalimu.

Walisema, chuo hicho kilitoa mafunzo ya kina kwa waalimu na kuwajenga kiuwezo hata kama hawakua na elimu ya juu mfano wa shahada na uzamilivu.

Mmoja kati ya wadau hao mwalimu mstaafu skuli ya Uweleni, Mohamed Ussi Shaame, alisema chuo hichoo kilikuwa mwarubaini wa kuipandisha hadhi elimu ya Zanzibar.

“Kwenye sere mpya ya elimu ijayo ni vyema ikatamka wazi wazi, suala la kukifufua kimafunzo na kimasomo chuo cha ualimu cha Nkurumah, ili tuzalishe wanmafunzi bora,’’alipendekeza.

Mkuu wa shirika la Maktba kisiwani Pemba, Mwache Mohamed Bakar, alisema moja ya eneo muhimu la kulirekebisha ni uwepo wa mafunzo bora ya waalimu.




Aidha alisema jengine linalofaa kuingizwa kwenye sera mpya ijayo ni kulazimisha kwa kila skuli iwe na maktaba yake na yenye vitabu vyote husika.

“Lakini hata sera itamke na ilazimishe kusijengwe wala kufunguliwa skuli yoyote pasi na kuwepo kwa matundu ya vyoo yanayokwenda samba mba uwiyano wa wanafunzi,’’alipendekeza.

Nae Mzazi Bimkubwa Juma Abass wa Chumbageni Mkoani, alipendekeza suala la ujenzi wa skuli lazima uzingatie mahitaji na matakwa ya wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Nae Siti Makame Ali ambae ni mjumbe wa PACSO alipendekeza kuwa, vyumba vya madarasa yawe na vifaa kamili ikiwa ni pamoja na meza na viti.

Kuhusu urejeshaji wa viboko (bakora), alipendekeza viwepo lakini kama adabu mbadala kwa wanafunzi, na iwe baada ya kupewa maonyo na maelekezo na waalimu.

Akizungumza kwenye mkutano wa siku mbili kwa wadau wa elimu wa Mkoa wa kusini Pemba, Mwenyekiti wa PACSO Mohamed Ali Khamis, alisema wameamua kufanya uchechemuzi wa sera ya elimu, ili wananchi watoe maoni yao.




Alieleza kuwa, PACSO imekuwa na utamaduni ya kuisadia serikali katika kuifikia jamii iliyokubwa zaidi, ili kuona maona yao wanayatoa kuelekea kupata sera mpya.

Mratibu wa miradi kutoka PACSO Mohamed Najim Omar, alisema mara watakapokamilisha ukusanyaji maoni, watayafikisha wizara ya elimu, kama sehemu ya maoni yao.

“Moja ya jukumu kubwa la asasi za kiraia, ni kuisaidia kazi serikali kuu, kwani nasisi tunakundi kubwa la jamii, na ndio maana tumeshafanya mikutano kadhaa ya kupokea maoni,’’alieleza.

Kaimu Mratibu wa Idara ya Mpingo, sera na utafiti wa wizara ya elimu Pemba Adam Kombo Nassor, alisema wanachokifanya PACSO kwao ni msaada mkubwa, katika uandaaji wa sera mpya ya elimu.

“Ni kweli sera inayotumika sasa ya mwaka 2006, imeshajaa changamoto, sasa wizara iko mbioni kukusanya maoni ili kisha baadae  kuwa na sera ambayo ndio muongozo wa elimu,’’alieleza.

Utafiti mdogo uliofanywa hivi karibuni na PACSO juu ya sera ya elimu inayotumika sasa ya mwaka 2006, ambapo waliwahoji watu 50 kwa kila wilaya kisiwani Pemba, ilibaina watu 162 kati ya 200  waliotakiwa kueleza nini maana ya sera hawakuwa na uwelewa.

Aidha utafiti huo ukabaini kuwa, watu 183 kati ya 200 waliohojiwa hawajui taratib za kuanzia mwanzo hadi mwisho za upatikanaji sera.

Watu wengine 138 walisema ushirikishwaji wao katika sera ya mwaka 2006 ni katika mikutano na ujenzi wa vyumba vya madarasa pekee.

                          Mwisho        

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch