Skip to main content

NYUMBA ZA UZUNGUNI WETE KUFANYIWA MATENGENEZO.

 


NA ZUHURA JUMA, PEMBA

WAKAAZI wa nyumba za Serikali zinazosimamiwa na Wakala wa Majengo Pemba, ambazo zipo Uzunguni Wete wametakiwa kuhama, ili kupisha matengenezo ya nyumba hizo.

Akizungumza na baadhi ya wakaazi wa nyumba hizo, Afisa Mdhamini Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Pemba, Bakar Ali Bakar alisema, ni vyema wananchi wakahama katika nyumba hizo, kwani zinahatarisha usalama wa maisha yao.

Alisema kuwa, kutokana na ubovu wa nyumba hizo haistaki tena kuishi wananchi, hivyo ni vyema wakasikiliza maagizo ya Wizara kuhusu kuhama eneo hilo, ili ziweze kufanyiwa matengenezo.

“Tuliwahi kuwapelekea barua ili wahame kwenye nyumba hizi kwa sababu ni mbovu na tayari zimeshafanya mipasuko, hivyo ni hatari kwa maisha yao, lakini baadhi yao bado hawajakubali kuhama”, alisema Mdhamini huyo.

Aliwaomba wakaazi hao kuridhia maagizo ya kuhama kwenye nyumba hizo, huku Wizara ikiandaa utaratibu wa kuzijenga, ili kuepuka maafa yanayoweza kutokea.

“Serikali ina azma nzuri kwenu, haina lengo la kuwafukuza katika nyumba hizi lakini kutokana na majengo yalivyo sasa hakuna haja ya kuishi hapa ni lazima kuhama”, alisema.

Mdhamini huyo alieleza kuwa, ubovu wa nyumba hizo kunaweza kuwaletea athari kubwa wao na Serikali na kusababusha kugharimu maisha ya watu pamoja kukosekana kwa rasilimali watu.

Kwa upande wao wakaazi ambao hawajahama katika nyumba hizo walieleza kuwa, walikuwa wameshaanza kuhama ingawa kuna baadhi ya vitu hawajamaliza na ndio maana muda mkubwa wanakuwepo eneo hilo.

“Hatuishi tena hapa na tumeshahamisha baadhi ya vitu vyetu ingawa kwa vile tumezoea huwa tunakuja na kukaa mara moja tu, lakini sasa tutahamisha kila kitu chetu na kuondoka”, walisema baadhi ya wakaazi hao.

Nae Injinia Said Malik Said kutoka Wakala wa Majengo Pemba alisema kuwa, ni muda wametoa barua ya kuhama kwa wakaazi hao ingawa baadhi yao wamekaidi agizo hilo.

“Tulifikiri tayari wameshahama, lakini nimeshangaa leo kuwaona hapa, nyumba ni mbovu na tunawahamisha kwa usalama wao, ingawa bado baadhi yao hawajalipa umuhimu suala hili”, alisema.

Alisema tangu watoe barua hizo, hawajawahi kudai kodi kwani hawatakiwi tena kuishi hapo mpaka pale nyumba hizo zitakapomalizika kujengwa.

Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi kupitia Wakala wa Majengo Pemba inatayarijia kuzijenga nyumba zilizopo Uzunguni Wete ili ziwe na hadhi ya kisasa.

                                              MWISHO. 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch