Skip to main content

WIZARA YA AFYA KUIMARISHA UTOAJI HUDUMA KWA WATU WENYE ULEMAVU




NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

WIZARA ya Afya Pemba imesema, itaendelea kuboresha mifumo ya utoaji huduma na upatikanaji wa huduma za afya kwa watu wenye ulemavu, kama sheria zinavyo elekeza.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Afisa mdhamini wa wizara hiyo Pemba Khamis Bilali Ali alisema, ili kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata huduma bora kama ilivyo kwa wengine, wizara itahakikisha hospitali zinawekwa njia za kupitia watu wenye ulemavu (Ramp) ili kupita kwa urahisi  pale wanapofika kufuata huduma.

Alisema jambo jengine linalotekelezwa ni kutoa maelekezo kwa watoa huduma za afya kuhakikisha wanatoa kipaombele kwa watu wenye ulemavu wanapofika hospitalini, kama kanuni zinavyo eleza ili kuhakikisha watu hao wanapata haki yao ya msingi ya afya bila ya usumbufu.

“Tumeweka (Ramp) pia kuna kanuni zinazo wataka watoa huduma kutoa kipaombele kwa wenye ulemavu na wizara inasimamia kwakaribu suala hili na linafanyika”, alieleza.

Alisema ingawa kuna changamoto ya wakalimani wa lugha ya alama kwa ajili ya wenye ulemavu wa uziwi hospitalini, wizara huwashauri watu hao kutumia wakalimani wa lugha ya alama waliomo katika jumuiya zao au watu wao wakaribu, ili kurahisisha mawasiliano na upatikanaji huduma bora.

Aliongeza kua katika kulizingatia hilo watoa huduma huweka umakini mkubwa wa kimawasiliano bainabaina yao na wagonjwa wenye uziwi, ambao wanaweza kujieleza wenyewe ili kuhakikisha wanapata huduma stahiki.

“Miundombinu ya utoaji huduma inaridhisha kwa watu wenye ulemavu wa aina mbalimbali, lakini bado changamoto ipo kwa wenye ulemavu wa uziwi, wakalimani hatuna bali tuna shauri wafike hospitali na wakalimani wao au watu wao wa karibu”, alieleza.

Alifafanua wizara imeona upungufu mkubwa katika eneo hili la wakalimani wa lugha ya alama hospitalini, na imeona ipo haja ya kuweka wakalimani hao ili kurahisisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wenye ulemavu wauziwi, hivyo wanaendelea kuishauri serikali kuu umuhimu wa jambo hili.

Alisema wizara ya afya itaendelea kuweka miundombinu rafiki ya utoaji huduma bora kwa watu wenyeulemavu, kwani ni haki ya msingi ya kila mmoja kama sheria zinavyo eleza.

Aidha aliwataka watu wenye ulemavu kuendelea kutumia vituo vya afya na hospitali ili kutatua changamoto zao za kiafya na kwamba serikali inawazingatia ipasavyo ili kuhakikisha wananufaika na huduma zote za msingi .

Kwa upande wao watu wenye ulemavu wamesema kwakiasi kikubwa serikali kupitia wizara ya afya  imefanikiwa katika utoaji huduma kwao, na upungufu zaidi unakuwepo  kwa wenye ulemavu wa uziwi, hivyo wameiomba serikali kuwazingatia watu hao ili wapate huduma bora kama ilivyo kwa wengine.


Sheria ya Zanzibar ya watu wenye ulemavu (2022) kifungu cha 28, kinaeleza kua watu wenye ulemavu wanastahiki  kupata haki zote za msingi ikiwemo ya afya.

MWISHO

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...