Skip to main content

WATU WENYE ULEMAVU NA USHIRIKI WA MICHEZO, BADO KIZUNGUMKUTI, WIZARA YAJITUTUMUA

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

‘’WATU wenye ulemavu wanastahiki haki zote za msingi za binaadamu, sawa na watu wingine, ikiwemo michezo na burudani,’’inaeleza sheria yao.

Sheria hiyo nambari 8 ya mwaka 2022, ikazidi kufafanua kwenye kifungu cha 28 (1) (f), kwamba kundi hilo linastahiki haki zote za msingi, bila ya ubaguzi.  

Tena uzuri zaidi kifungu cha 29 (1), kikamtamka kuwa, Baraza la Taifa la Watu wenye ulemavu, katika kuiendea haki hiyo, litahakikisha ufikiaji wa maeneo hayo.

Kikafafanua kuwa, lazima pawepo na miundombinu rafiki ya kuyafikia majengo ama maeneo kwa watu wenye ulemevu, wanapoziendea haki zao michezo na burudani.

Kifungu cha 30, kikasisitiza kuwa, kila mmoja anawajibu wa kutekeleza, kulinda na kutetea haki za watu wenye ulemavu, kwa kutoa taarifa za uvujifu wa haki hizo.

Eneo jingine sera ya maendeleo ya taifa ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2004, Ibara yake 3.15 ikazitaka nchi, kuhakikisha wanawekewa utaratibu utakaohakikisha watu wenye ulemavu, wanashiriki kikamilifu, michezo na burudani.

Sera, ikataka kuaandaliwe utaratibu utakaoshirikisha vyama vya michezo na wadau wingine, kuhakikisha sehemu za michezo kwa watu wenye ulemavu, zinakuwa mpango wa kuendeleza michezo kitaifa.

Mkataba wa kimataifa wa haki za watu ulemavu wa mwaka 2006, Ibara ya 30, ikazitaka nchi, zinachukua hatua kadhaa, ili kuhakikisha watu wenye ulemavu, wanaushiriki sawa kwenye michezo.


Kwenye kifungu cha 30 (b) ukafafanua kuwa, kundi hilo linaakuwa na fursa ya kuandaa, kuendeleza na kushiriki kwenye riadha na burudani, mahsusi kwa ajili yao.

 ‘’Kuhakikisha kuwa, kundi hilo linapata huduma sawa kutoka kwa wanaoandaa shughuli za michezo na burudani, bila ya vikawazo,’’ulifafanua mkatana huo.

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kifungu cha 20, kinatoa kinga kwa uhuru wa watu kujikusanya na kujiunga, kupitia vikundi mbali mbali.

Hapa mikataba, sheria, kanuni, katiba na maandiko, haijawabagua watu wenye ulemavu, kushiriki michezo na burudani.

HALI HALISI IKOJE?

Hidaya Mjaka Ali, kutoka Umoja wa Watu wenye ulemavu Zanzibar ‘UWZ’ Pemba, anasema bado ni kaa la moto, kwao kushirikishwa kwenye michezo.

Anasema, kuanzia viwanja, gharama, vifaa na ushajiishaji, umekuwa haupo, kama ilivyo kwenye mikata na sheria ilivyoelekeza.

‘’Kwa sasa tunayosheria mpya ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2022, lakini bado vifungu vinavyolazimisha sisi kushiriki michezo, havijatekelezwa,’’analalamikia.

Omar Shaibu Omar wa Wawi, mwenye ulemavu wa viungo, anasema hakumbuki hata shindano moja la michezo, kwa ajili ya watu wenye ulemavu, lililowahi kuandaliwa Pemba.

‘’Kwa hakika kwenye michezo sisi hatujatekelezewa hata kidogo, na tunatamani sana kama mpira wa miguu tuwe na ligi yetu, lakini wapi,’’anasikitika.

Ali Ussi Hakim wa Mwambe mwenye ulemavu wa usikivu, anasema vipaji vyao vinazidi kudidimizwa, maana hata timu za mitaani hawashirikishi.

‘’Nilikuwa na rafiki yangu alikuwa akicheza mpira vizuri, lakini kwa vile alikuwa kiziwi, timu ya Mtambile ilimkataa, na kwa vile hakuna ligi yetu maalum, aliachana na michezo,’’anasema.

Mohamed Haji Khamis wa Makoongwe Mkoani, anasema hakuna ligi iliyoandaliwa na wizara ya michezo, iwe ya mpira wa miguu, mikono, kikapo, pete, kuogelea na riadha, kwa ajili yao.

Massoud Khamis Haji wa Mchanga mdogo na Aisha Omar Othmna, wanasema wanamebakia kuwaangalia timu za wenzao, kwao wakikosa haki hiyo.

Bahati Khamis Haji, anasema kwa mara ya mwisho alishiriki kwenye michezo ya kuruka juu, Disemba 3, mwaka 2020 kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya watu wenye ulemavu Wete.

‘Kwa hakika sheria na mikataba haijatekelezwa kwenye michezo, imekuwa maadhimisho hadi sherehe, ndio pingine tunaweza kuigusa michezo,’’analalamika.

ZFF

Khamis Hamad, Katibu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar 'ZFF' ofisi ya Pemba, anakiri kuwa, hakujawahi kuandaliwa ligi ya mpira wa miguu wala michezo mingine, kwa ajili ya watu wenye ulemavu.


Anasema, hilo linachangiwa na mambo kadhaa, ikiwemo miundombinu ya viwanja kwao sio rafiki, mifumo ya mpira wa miguu kwa Pemba, bado ni changamoto.

‘’Huwa nasikia tu huko Tanzania bara, ipo timu ya mpira wa miguu ya watu wenye ulemavu, na imefanya vizuri, lakini kwa Pemba bado sana,’’anasema.


JUMUIAYA ZA WATU WENYE ULEMAVU

Mwenyekiti wa Jumuiya ya wasioona Zanzibar ‘ZANAB’ Ofisi ya Pemba Suleiman Mansour, anasema watu wa kundi lao, bado halijazingatiwa kwenye michezo.

‘’Inawezekana kwa sababu anaeshughulikia michezo hana ulemavu, na ndio maana hata sisi wenye ulemavu hautuna ligi ya michezo wowote,’’anasema.

Maratibu wa Baraza la Taifa la Watu wenye ulemavu Pemba Mashavu Juma Mabrouk, anasema lazima jitahada za kupaza sauti zifanywe, ili kundi la watu wenye ulemavu, lishirikishwe michezo.


‘’Tunataka michezo jumuishwi, viwanja jumuishi, ili kusiwe na mtu kwa sababu ya ulemavu wake, anakosa kushiriki michezo, hii itakuwa sio sahihi,’’analalamika.

WIZARA INAYOSHUGHULIKIA WATU WENYE ULEMAVU INAFANYA NINI?

Aliyekuwa Waziri wa Afisi ya Makamu wa Kwanza Harusi Said Suleiman, anasema kwa mwaka 2024/2025, waliandaa bonanza la michezo kwa watoto 100 wenye ulemavu na wasiokuwa na ulemavu, wakiwemo wanawake 51 na wanaume 49.

Anasema ilikuwa ni sehemu ya shamrashamra za kilele cha maadhimisho ya siku ya kimataifa ya watu wenye ulemavu duniani Disemba 3.

Akafafanua kuwa, kwenye kilele cha siku hiyo, michezo kadhaa ilifanyika, ukiwemo wa kuruka kamba, mbio za magunia, kuvuta kamba, kukalia viti na mchezo wa kuvuka vikwazo.

 Eneo jingine ilifahamika kuwa, hakuna shabaha ya moja kwa moja, inayozungumzia uimarishaji wa michezo, kwa mwaka wa fedha 2025/2026, kati ya shabaha kadhaa.



MITANDAO YA KIJAMII IMERIPOTI NINI?

Disemba 2021, blog ya Idara ya Habari Maelezo ya Tanzania bara, imeripoti, aliyekuuwa waziri wa Michezo, Innocent Bashungwa, aliwaongoza watanzania kuishangilia timu ya Tanzania ‘Tembo Warriors’ baada ya kufuzu nusu fainali ya soka ya bara la Afrika, kwa wenye ulemavu ‘CANAF’.

Hivyo, kukata tiketi ya kushiriki mashindano ya dunia ya mchezo huo yaliyofanyika Uturuki mwaka 2022, ni baada ya kuichapa timu ya Cameroon mabao 5-0. 

Tena timu hiyo baada ya kuingia kwenye michuano hiyo, ilipata ushindi wake wa kwanza, kwa kuifunga Uzbekistan mabao 2-0.

Nayo Dost Media, iliripoti kuwa, Emmanuel Mrefu kijana mtanzania mwenye ulemavu wa viungo, anacheza soka la kulipwa kwa sasa.

Kulingana na kituo cha kudhibiti magonjwa, mmoja kati ya watu wazima wanne wa Marekani, wana ulemavu unaoathiri, shughuli kuu za maisha yao.

Kwa Tanzania sensa ya mwaka 2022 imebaini asilimia 11.2 ya watanzania ni walemavu na wanaohitaji mahitaji muhimu, ili waweze kuendesha maisha yao.

NINI ATHARI YAKE?

Katibu Mtendaji Baraza la Taifa la Watu weye ulemavu Zanzibar Ussi Salim Debe, amenukuliwa akisema, ni kukosa kuwaendeleza watu wenye ulemavu.

‘’Michezo ni afya, na wakiwanayo watu wenye ulemavu hupunguza ukakasi na ufinyu wa kiakili na mwili, na wakiiokosa huzidi kudumaa,’’anasema.

Khamis Hamad kutoka ‘ZFF’ anasema, ni kuwanyima haki zao za kushiriki michezo, kama walivyo watu wingine.

NINI KIFANYIKE?

Maulid Ali Hamad mwenye ulemavu wa Viungo, anasema ni kutekelezwa kwa sheria yao, ambayo inalazimisha michezo kama walivyo makundi mingine.

Aliyekuwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar Tabia Maulid Mwita, akayomba mashirika kuungana na serikali, katika kuanzisha ligi maalum kwa watu wenye ulemavu.

Mwanaharakati wa haki za watu wenye ulemavu Khalfan Amour Mohamed, anasema ni kuhakikisha, wizara inayosimamia michezo, inaweka bajeti maalumm kwa ajili ya kundi hilo.

                       Mwisho  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...