Skip to main content

HUDUMA ZA AFYA KWA WATU WENYE ULEMAVU SIO NGUMU WALA LAINI

 



NA MOZA SHAABAN, PEMBA

DUNIA inapaswa ielewe kuwa, watu wenye ulemavu ni sawa na watu  wingine katika jamii.

Wana haki ya kunufaika na kupata haki zote za msingi ikiwemo ya afya.

Haki ya afya kwa watu wenye ulemavu imetamkwa na kuelezwa kwenye sera na sheria za kimataifa, kikanda na kitaifa.

Hapa Mkataba wa Kimataifa wa Haki za watu wenye ulemavu wa mwaka 2006, ibara ya 25, imesisitiza watu wenye ulemavu wana haki ya kupata huduma za afya bila ubaguzi.

Huku Sheria ya Watu wenye Ulemavu ya Zanzibar nambari 8 ya mwaka 2022 nayo kwenye kifungu cha 28, kikisisitiza watu wenye ulemavu wanastahiki kupata haki zote za msingi ikiwemo ya afya.

“Watu wenye ulemavu wanastahiki kupata huduma za afya kama matibabu, matengenezo na marekebisho yanayohusiana na ulemavu,” kinafafanua kifungu hicho.

Hii inaonyesha, jinsi gani ulimwengu umewazingatia  watu wenye ulemavu katika upatikanaji wa haki zote za msingi ambao ndio haki za kibinaadamu.

Kwani watu wenye ulemavu ni kundi kubwa na muhimu, ambalo halipaswi kudharauliwa kwa namna yeyote.

 Izingatiwe kwamba matokeo ya sensa ya watu na makaazi ya mwaka 2022, yameweka wazi kua asilimia 11.4 ya wazanzibari wote ni wenye ulemavu.

Kwa muktadha huu wanastahili kupata haki zote za msingi ikiwemo huduma za afya, kama ilivyoainishwa.

Na haya yote yanaweza kufikiwa iwapo kila aina ya ulemavu itazingatiwa kwa kuwekewa namana bora ya kuzifikia na kuzipata huduma za afya.



WATU WENYE ULEMAVU WANASEMAJE?

Mmoja wa watu wenye ulemavu wa viungo Said Saleh Sultan wa Mtambile anasema, miundombinu wezeshi  ya ufikiaji huduma iliopo, ndio ujumuishi wao.

Anasema asilimia kubwa ya vituo vya Afya vinawawezesha wenye ulemavu wa viungo kuzifikia huduma, bila au wakiwa na viti mwendo.

Rehema Juma wa Kukuu Kangaani Mkoani, mwenye ulemavu wa uoni anasema, wamekua wakipata  kipaumbele kupata huduma katika vituo vya afya na hospitalini.

Anaona jambo hilo ni hatua muhimu, katika ujumuishi wao kwenye haki hiyo ya msingi ya kiafya.

“Tunapofika vituo vya afya au hospitali tunapewa kipaumbele, ni utaratibu mzuri kwetu, kwani unahakikisha upatikanaji wa haki zetu,”anaeleza.

Pamoja na jitihada hizi bado changamoto zipo kwa watu wenye ulemavu wa uziwi, kutokana na kutokuwepo kwa wataalamu wa lugha ya alama.

Wenyewe wanasema, wasisahauliwe wazingatiwe na watiliwe maanani kama ilivyo kwa wingine.

Nuru Faki Kombo mkaazi wa Kangani mwenye ulemavu wa uziwi anaeleza, mawasiliano baina yao na watoa huduma za afya ni changamoto.

Anasema wakati mwingine hulazimu kuwepo mtu wa tatu wanapotaka huduma za afya, ili waipate ipasavyo haki yao hiyo ya msingi.

Anafafanua kua, mara nyingi kunakua na kutofahamiana baina yao na watoa huduma, kwani wengi wao hawana uwelewa wa lugha ya alama.

Adinani Khamis wa Chake chake anasema, mara nyingine hutumiza dawa madukani na kutumia, bila kuonana na wataalamu.

Anasema ni vyema Wizara ya Afya kuimarisha mifumo ya mawasiliano, kwa kuweka wakalimani wa lugha ya alama hospitalini na vituo vya afya.



“Sisi wenye ulemavu wa uziwi tunapata shida sana kuwasiliana na watoa huduma wa afya, kwani hua hatuelewani, hivyo tunaomba tuzingatiwe,”anasisitiza.

Wafanya kazi wa vituo vya afya na hospitali wakiwemo madaktari na wauguzi, kazi yao kuhakikisha mtu anaefika hospitali anapata huduma stahili, bila kujali hali ya mtu.

WATOA HUDUMA ZA AFYA

Abdullah Ali Juma Daktari wa kituo cha afya Michenzani Mkoani Pemba anasema, utoaji huduma za kitabibu  kituoni hapo, unatoa kipaumbele kwa watu wenye ulemavu.

Anasema huweka umakini wa hali ya juu zaidi kwa wenye ulemavu wa uziwi, ili mawasiliano baina yao yasiwe kikwazo.

Kwa kuepusha hili, Afisa watu wenye ulemavu kutoka Umoja wa watu wenye Ulemavu ‘UWZ’ Pemba Maryam Mohamed Salum anasema, watu wenye ulemavu wanapaswa kuzingatiwa, katika utoaji wa huduma za afya.

Anaeleza changamoto yeyote ile katika vituo vya utoaji huduma hizo, inaweza kuzorotesha ustawi wa watu wenye ulemavu.

 Mratibu Baraza la taifa la watu wenye ulemavu Pemba Mashavu Juma Mabrouk anasema, kuna haja ya kuboresha mawasiliano kwa watoa huduma za afya.

Anaeleza kua, hili litasaidia kuimarisha upatikanaji wa huduma bora kwa watu wenye ulemavu, hasa wale wa uziwi.

Anasisitiza wataalamu wa afya wanapaswa kupewa mafunzo maalum ya kushughulikia mahitaji ya kundi hili.



 Anaongeza kua watu wenye ulemavu wanapaswa kushirikishwa katika kutathmini mipango na bajeti za afya, kama ilivyoelekezwa kwenye sera na miongozo ya nchi kwa ujumla.

Kwa kuona umuhimu wa afya kwa watu wenye ulemavu jitahada mbali mbali zinafanyika kutoka  serikalini na  asasi za kiraia.

Huku lengo likiwa ni kuhakikisha ujumuishi wao na upatikanaji wa haki hii ya msingi ya afya.

Moja ya asasi ni Chama cha waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar, ambao wanatoa mafunzo kuwajengea uwezo waandishi wa habari, juu ya utetezi wa  haki za watu wenye ulemavu.

Masaidizi mkuu wa kitengo cha  elimu ya afya Ghalib Hassan Hamad  anasema, watoa huduma za afya wameshajengewa uwezo ili kutoa huduma bora kwa watu wenye ulemavu.

Afisa Mdhamini wizara ya Afya Pemba Khamis Bilali Ali anasema, wizara inaendelea kuboresha mifumo ya utoaji huduma na upatikanaji wake kwa watu wenye ulemavu.

Anaongeza kuna kanuni zinazowataka watoa huduma  kutoa kipaumbele kwa wenye ulemavu, katika utoaji wao wa huduma na wizara, inasimamia kwa karibu suala hilo.

Anasisitiza ingawa suala la wakalimani wa lugha ya alama hospitalini ni changamoto, lakini kuna umakini mkubwa wa kimawasiliano baina ya watoa huduma na watu wenye ulemavu wa uziwi.

“Ili wenye ulemavu kupata huduma stahili za afya, wizara inajenga miundombinu yenye kufikika kwa kila mmoja, wahudumu wetu wanatoa kipaumbele kwa wenye ulemavu na wanaumakini mkubwa wa kuwasiliana nao,”anaeleza.

Wizara ya Afya itaendelea kuweka miundombinu rafiki ya utoaji huduma bora kwa watu wenye ulemavu, kwani ni haki ya msingi ya kila mmoja.

Aidha Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi katika hutuba yake ya ufunguzi wa baraza la wawakilishi Zanzibar Novemba 10 mwaka huu, aliahidi kulinda na kuimarisha haki za watu wenye ulemavu.

MWISHO

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...