Skip to main content

KAMATI: 'MASHINDANI YA TANO YA QUR-AN WAMBAA YALIFANIKIWA'


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

JUMUIYA ya tahafidhi qur-an kanda ya Wambaa na Chumbageni wilaya ya Mkoani, imewashukuru waumini wote na taasisi nyingine, kwa michango yao, iliyofanikisha mashindani yao ya tano ya tahafidh qur-an, yaliyofanyika hivi karibuni.

Akizungumza kwenye kikao cha tathmini, kilichofanyika almdarsaatul- imaniya Chumbageni, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo ustadhi, Hassan Othman Khamis, alisema pamoja na kujipanga kwao, lakini michango ya wadau, ilisaidia kufanikisha shughuli hiyo.

Alisema kuwa, umoja na mshikamano waliopewa na jamii ya Chumbageni na Wambaa, ni vyema ukawa endelevu kwani, wanamalengo ya kuendesha mashindani mingine makubwa, hapo mwakani.

Alieleza kuwa, bila ya wanajamii kufanikisha michango yao, isingekuwa rahisi wao, kufikia malengo na kuendesha mashindani hayo ya tano kwa mwaka huu.

ā€˜ā€™Kwa hakika michango ya fedha, vifaa na zawadi nyingine zilizotolewa na wanajamii, ilisaidia mno kunogesha mashindani yetu, na tunawapa shukran watu wote,ā€™ā€™alifafanua.

Hata hivyo, amwapongeza viongozi wenzake wa Jumuiya, kwa moyo wao wa kujitoa wakati wote wa maandalizi, kuanzia siku ya kwanza hadi kwenye kilele husika.

Kwa upande wake Katibu wa jumuia hiyo ustadhi, Abdalla Haji Ali, alisema kwa mashindani ya mwaka huu, muitikio wa wazazi na walezi, ulikuwa mkubwa, ikilinganishwa na mwaka uliopita.



ā€˜ā€™Hasa wazazi wa kiume, tunawashukuru mno kwa kuhudhuria kwao, maana kwa mwaka jana, walikuwa wachache mno, jambo ambalo lilitukatisha tamaa kama wanajumuia,ā€™ā€™alifafanua.

Hata hivyo, amezikaribisha madrassa nyingine kutoka nje ya shehia za Wambaa na Chumbageni, kujitokeza kushirikiana na jumuiya yao, ili kuongeza idadi ya madrassa hapo mwakani.

ā€˜ā€™Ni kweli kwa awamu tano mfululizo, hatujawahi kupata madrasaa nje ya shehia zetu mbili, lakini kwa mwakani tunazikaribisha madrassa nyingine, ili kuongeza idadi kutoka saba, walau kufikia 10 mwakani,ā€™ā€™alifafanua.



Baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu wa shehia za Wambaa na Chumbageni, walisema mashindani ya mwaka huu, yalikuwa mazuri mno, ikilinganishwa na mwaka jana.

Wakati huo huo Nnaibu Mwenyekiti wa kamati hiyo, ustadhi Awesi Abdalla Ali, amesema wanakusudia kuendesha uchaguzi wa viongozi wapya wa jumuia hiyo, mapema mwezi ujao.

Alieleza kuwa, walikuwa wanasubiria kumalizika kwa mashindani hayo, na kuitisha uchaguzi mwingine, ambao ni takwa la kikatiba.

ā€˜ā€™Mwanzoni mwa mwezi ujao, tutakutana kwa ajili ya kupanga mikakati na kuendesha uchaguzi, ili jumuiya ya tahafidhi qur-an ya kanda ya Wambaa na Chumbageni, ipate viongozi wapya,ā€™ā€™alieleza.

Nao wajumbe wa kamati hiyo, wamewakumbusha viongozi wa jumuia hiyo, kwa mwakani, kuanza maandalizi mapema, ili mashindani hayo yazidi kuwavutia wengi.

Raya Juma Khamis, alisema kama sikuchelewa kuanza maandalizi kwa mwaka huu, wengepata asilimia 100 ya mafanikio, kwa mashindani hayo.

Mashindani ya tano ya tahafidh qur-an kanda ya Wambaa na Chumbageni, yalifanyika mwezi 22 ramadhan, katika msikiti wa ijumaa Chumbageni na mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa wilaya ya Mkoani Dk. Hamad Omar Bakar.

mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ā€˜ Mkapaā€™ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ā€˜ Makababu ā€™ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. ā€œBaada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,ā€™...

ā€¦ā€¦.SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ā€˜SUZAā€™ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...