Skip to main content

USHIRIKI WA WANAWAKE MAPAMBANO YA MABADILIKO YA TABIANCHI WAZAA MATUNDA@@@@

 





NA KHAULAT SULEIMAN,PEMBA

 KATIKA harakati za kupambana na mabadiliko ya tabia ya nchi, jitihada za akina mama zinazidi kwa kuandaa mbinu,  ambazo zitasaidia katika  kukabiliana na janga la mabadiko ya tabia ya nchi.

Mabadiliko ya tabia ya nchi yanazidi kujitokeza siku hadi siku, kiasi ambacho husababishwa na  shughuli  za kibindamu, ikiwemo ukatwaji wa miti ya juu na ile ya pembezoni mwa bahari.

Ambayo kisayansi yametajwa kuwa, husaidia kuzuiya upandaji wa maji juu ama kufika katika sehemu za makazi ya wanachi.

Mabadiliko ya tabia ya nchi (climate change) ni  mwenendo wa hali ya hewa yakiwemo majira, wastani na vizio vya juu na chini kabisa vya joto, utokeaji  na mtawanyiko wa mawingu, mvua na theluji.

Zipo athari kadhaa ambazo zinasababishwa na hali hiyo, ambayo huathiri jamii na nchi kwa ujumla.

Moja wapo ni ongezeko la nyuzijoto, na kasi ya matukio mabaya mno ya hali ya hewa kuanzia kwa mawimbi na joto, ukame, mafuriko, dhuruba za msimu wa baridi, vimbunga na mioto ya mwituni.

Mnamo mwaka 2019, shirika la hali ya hewa ulimwnguni (WMO), linasema joto la wastani ulimwenguni  lilikua 1.1, juu kuliko kipindi cha kabla ya ujenzi wa viwanda.

Linasema mwaka huo huo ilihitimishwa muongo wa joto la kipekee ulimwenguni, kupungua kwa barafu na uswa wa bahari, kutokana na gesi za ukaa zinazozalishwa na shughuli za binadamu.

WMO likaenda mbali na kufafanua kuwa, watu 30 kila 100 ulimwenguni kote, wanakabiliwa na wimbi baya la joto yanayotokezea zaidi ya siku 202 kwa mwaka.

 




Mkufunzi wa kilimo msitu chini ya mradi wa mabadiliko tabia nchi Zanzibar ZANZADPT, unaoendeshwa na Jumuima ya uhifadhi wa misitu CFP, Fatma Ali Mgwali wa shehia Kiuyu Minungwini, anasema kilimo hicho ni himilivu.

Kilimo msitu  ni kilimo ambacho ni mchanganyiko wa mazao mbali mbali, kama minanasi, michikichi migomba, njugu, mahindi, mbazi na miembe,   kinasaidia kuhimili na kulinda upotevu wa hali ya hewa.

Mkufunzi na mkulima wa shehia Mjini kiuyu Ridhiki Ali Juma, anategemea kupata mvuno mfululizo, wakati wa msimu wa mavuno ukianza.

ā€˜Baada ya kupewa elimu na CFP, ili niwape na wenzangu, nilianza kuotesha shamba la kilimo msitu na sasa nna minanasi, michikichi, migomba pamoja na mboga mboga kwenye eneo dogo,ā€™ā€™anasema.

Wanasema faida nyingine ya kilimo msitu ni kupata miti kwajili ya kuni, mbao matunda, kurutubisha undogo, malisho ya mifugo dawa za asili na usindikaji wa bidhaa zinazotokana na mazao ya misitu

WANUFAIKA WA MRADI

Fatma Shaban Mohamed ni mkulima wa kilimo msitu  mkaazi wa Kiuyu minungwini ambaye alihamasika katika kilimo hicho.

ā€˜Mradi huu ulitufikia mwezi wa tatu , tulianza mafunzo  na kulima minanasi 1625 ,miche ya miparachi ambapo awamu ya kwanza ilikua sita  kwa kupiga matuta umwagiliaji wa maji ā€˜ā€™anasema.

Hidaya Khatib Hamad mkaazi wa Kambini bandani  anaeleza kuwa, kupitia kilimo msitu kinaweza kusaidai  wanawake  kujikwamua kimaisha.

ā€˜Mwanzo niliona kilomo hichi kitanikwamisha katika shughuli zangu nyingine na kukatishwa tamaa kua hakina faida yoyote na ipo miradi mbali mbali ambayo inakuja, ingawa hatupati faida, kupitia kilimo msitu tunaona faida na tutaweza kufikia malengo yetu.



WANAUME WANASEMAJE

Khatibu Suleiman Juma Katibu wa kamati ya uhifadhi wa shehia ya Kambini, amesema kamati imezingatia kuweka idadi kubwa ya wanawake kwenye kamati kuliko wanaume ili kuwapa kipaumbele.

ā€˜Katika kutoa mchangao kwa wanawake kushiriki na kutoa mamuzi kwa kupaza sauti zao, ili kuweza kusikika,ā€™ā€™anasema .

Khatib Omar , mjasiriamali mkazi wa Mjini kiuyu aliwashauri wanaume ambao bado wapo nyuma katika uwelewa wa kuwashirikisha, kuwapa nafasi uhuru wa kufanya shughuli za kujikwamua kimaisha.

TAMWA  

Chama cha wandishi wa habari  wanawake TAMWA Zanzibar, nao husimama kidete  katika tetea haki za upatikanaji wa usawa wa kijinsia, na kuwashirikisha wanawake.

Kaimu Mratibu wa chama hicho, ofisi ya Pemba, Amina Ahmed amesema ,wameona  bado kuna  nafasi kwa wandishi wa habari kupaza sauti zao kwenye mabadiliko ya tabia nchi.

ā€˜ā€™Tulishirikiana na CFP na CFI lakini tutahakikisha sauti za wanawake zinasikika katika zote shehia nne ambazo zimefika mradi  kwa kupaza sauti zao, kwenye mabadiliko tabia nchi,ā€™ā€™anaeleza.

CFP

Mkurugenzi wa Jumuiya ya uhifadhi ya misitu Pemba, Mbarouk Mussa amesema, athari mbali mbali za ukataji wa miti ya mikoko kwa shughuli mbali mbali za kijamii, zimekuwa zikijitokeza katika maeneo tofauti huku jumuiya hiyo ikiendelea kutoa elimu.

Nae Saada Juma Afisa kilimo kutoka CPF, amesema mradi umelenga watu wote hauja  bagua na lengo ni kuwainua wanawake  katika shughuli za  kujitafutia kipato.

ā€˜ā€™Shughuli za ugawaji wa mbegu za kilimo msitu katika shehia( 4 ) hufanyika kika baada ya miezi minne, ili kuondoa changamoto ya ukosefu wa mbegu hizo kwa walengwa,ā€™ā€™anaeleza.

 Afisa Mdhamini  Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Pemba, Mhandishi  Idris Hassan Abdulla amefafanua kuwa ,wameanda mpango maalum wa kuhakikisha, wanazalisha kupitia kilimo msitu kwa kuchanganyisha miti tofauti.

Uharibifu wa mazingira na rasilimali zilizopo pamoja na kushauriana na wadau kuona ni kwa namna gani tatizo hilo linaondoka

                    MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ā€˜ Mkapaā€™ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ā€˜ Makababu ā€™ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. ā€œBaada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,ā€™...

ā€¦ā€¦.SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ā€˜SUZAā€™ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...