Skip to main content

''MSITEGEMEE WANGANGA WA KIENYEJI KUPANDA VYEO, CHAPENI KAZI'

  


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MKURUGENZI Baraza la Manispaa ya Chake chake Maulid Mwalim Ali, amewataka watumishi wapya wa umma kisiwani Pemba, kutotegemea waganga wa kijienyeji, kutafuta vyeo katika ofisi zao, na badala yake wafanye kazi kwa bidii kwani ndio msingi mkuu.

Alisema, huu sio wakati tena wa kuelekea kwa wapigamrali, ili kusaka vyeo, bali mchawi wa hilo ni kuwatumikia wananchi kwa ufanisi zaidi na bila ya ubaguzi.

Mkurugenzi huyo aliyasema hayo jana, ukumbi wa Manispaa hiyo alipokuwa akiyafunga mafunzo ya siku mbili, kwa watumishi wapya wa umma, kuhusu uthibitisho wa kazi baada ya kuajiriwa.



Alisema, nidhamu, utendaji kazi uliotukuka, heshima na kutoa huduma bora, ndio chanzo cha wao kupanda daraja katika maeneo yao ya kazi.

‘’Niwaombe sana watumishi wenzangu wa umma, kuhakikisha mnakwenda kufanyakazi kwa bidii na nidhamu, kwani huo ndio msingi mkuu wa kupanda daraja,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi huyo, amewataka watumishi hao wapya, kujenga umoja na mshikamano miongoni mwao, ili kufanikisha kazi zao.

Hata hivyo, amewakumbusha kuzisoma kwa umakini sheria na kanunuzi za utumishi wa umma, ili wajuwe kwa undani haki na wajibu wao.



Akiwasilisha mada ya maadili kwa watumishi wa umma Mkuu wa Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar ‘IPA’ tawi la Pemba, Juma Haji Juma, alisema msingi mkuu wa maadili ni kujielekeza katika utendaji wa kazi.

Alisema msingi mwingine ni kujielekeza kwa mpewa huduma, tena iwe kwa hali ya juu, kwa wakati na bila ya kujichelewesha wakati uliopangwa.

Aidha Mkuu huyo wa Chuo cha IPA, aliwafahamisha watumishi hao wapya wa umma kuwa, msingine mwingine wa maadili ni wajibu wa kuitumikia mamlaka ya nchi.



‘’Kwa mfano kutii maagizo na miongozo ya serikali iliyopo madarakani ni jambo la lazima, katika kufikia azma ya maadili kwa mtumishi wa umma,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, amewaonya watumishi hao kutotumia lugha za kejeli, matumisi, ubaguzi na watumie lugha za kupembejea.

‘’Mjue kuwa mnaiwakilisha serikali kuu, mkitumia lugha chafu mnaiwakilisha vibaya, lakini lugha laini na nyororo ndio zitawaridhisha wateja hata kama wamekosa huduma husika,’’alifafanua.

Mapema Afisa kutoka Mfuko wa Hifadhi wa Jamii Zanzibar ‘ZSSF’ tawi la Pemba Said Bakar, alisema yapo mafao kadhaa ikiwemo ya kuumia kazini, ulemavu na wanachama waliojifungua kwa kufuata uzazi wa mpango.



Alieleza kuwa, ni wakati sasa kuzifahamu sheria za utumishi na kujua namna ya kudai mafao ya kuumia kazini ikitokezea, jambao ambalo watumishi waliowengi hilo hawalifahamu.

 Kwa upande wake Wakili wa kujitegemea Suleiman Omar Suleiman, aliwataka watumishi wa umma kuzisoma kanuni za utumishi wa umma na sheria zake, ili wajuwe haki na wajibu wao.



‘’Ni vigumu kudai haki zenu hasa zilizojificha, kama mtakuwa wazito wa kuzisoma sheria na kanuni zinazowaongoza, katika kipindi chote cha utumishi wa umma,’’alifafanua.

Mapema washiriki hao walisema mafunzo hayo ni mazuri, ingawa yanahitaji uendelevu kila baada ya muda, ili kuhakikisha wanazielewa.

Mwisho 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...