Skip to main content

HATIMAE BARABARA MELI TANO- WETE YAANZA KUTIWA LAMI, WANANCHI HAWAAMINI MACHO YAO

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANANCHI na waendesha vyombo vya moto wanaotumia barabara ya Meli tano- Wete, wamesema zoezi la utiaji wa lami wa barabara hiyo, ndio wameanza kujenga matumiani ya kuitumia barabara hiyo bila ya usumbufu.

Walisema, sasa wanaamini na kuanza kusahau machungu waliyodumu nayo kwa miaka zaidi ya 20, kufuatia kuharibika kwa miundombinu ya barabara hiyo bila ya kufanyiwa matengenezo.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, walisema kwa sasa hawana shaka ten ana nia ya serikali ya kuwatengenezea barabara hiyo, hasa baada ya kuanza kwa zoezi la utiaji wa lami wiki tatu zilizopita.

Walisema, kwa sasa hawana wasi wasi na kuwataka wenzao wanaoitumia kutoa ushirikiano wa karibu na mafundi hao, ili zoezi hili liwe rahisi kwao.

Mmoja katia ya wananchi hao Mwanajuma Haji Nassor ‘anti mwaju’ alisema zaidi ya miaka 30, barabara hiyo ilikuwa ikitajwa kuuanza ujenzi wake bila ya mafanikio.

Alieleza kuwa, walifika pahala walishindwa kuamini nia thabiti ya serikali kwamba barabara hiyo yengenjwa kwa kiwango la lami.

‘’Maana ahadi zilishakuwa nyingi mno kwetu, sasa ilifika pahala hata tukielezwa hakuna anayeamini, maana tulishakula dhiki na usumbufu kwa miaka mingi,’’alieleza.


Nae Khamis Omar Khamis, alisema zoezi linaloendelea la utiaji wa lami ndio limewapa uhakika kwamba, sasa serikali inataka kutimiza ahadai zake kwetu.

Dereva wa gari ya abiria aliyejitambulisha kwa jina la Khamis Haji, anayefanyakazi Chake chake-Wete kupitia barabara hiyo, alisema walishapata usumbufu kwa muda mrefu.

‘’Hata wakati ujenzi unaaza wa kuisafisha barabara hii, mimi na wenzangu hatukuamini kwamba, itafika pahala iwekee lami, maana ahadi zilishakuwa nyingi,’’alieleza.

Hata hivyo, alisema kwa kasi ya uwekaji lami kwa sasa, wanayomatumaini ya kweli, kwamba sasa dhiki inaweza kuandoka wakati wowote.

Dereva wa piki piki ‘boda boda’ anayechukua abiria eneo la Meli tano, alisema sasa wanafurahishwa na kazi ya Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi.

‘’Mwinyi naamini ametumia nguvu nyingi kuhakikisha barabara hii haikuwami tena, na leo zoezi la uwekaji limeshaanza na sasa naamini juu ya kukamilisha ahadi hii,’’alisema.

Mkubwa Haji Kassim mwenye ulemavu wa viungo, alisema sasa wataisahau dhiki ya kupita kwa dhiki na baiskeli zao za magaurudumu matatu.

Mkuu wa wilaya ya Wete Dk. Hamad Omar Bakar, alisema kasi ya Dk. Mwinyi ndio iliyosababisha barabara hiyo na nyingine kuendelea kwa kasi ujenzi wake.

Akitembelea ujenzi wa barabara hiyo, Julai 30, mwaka huu Makamu wa Pili war ais Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla, aliitaka kampuni ya Mecoo inayojenga barabara hiyo kuongeza kasi zaid.

Alisema, anajua kuwa kwa mujibu wa mkataba wake, ilitakiwa barabara hiyo ikamilike tokea mwezi Augost mwaka huu, ingawa kutokana na sababu mbali, wakaongezewa tena miezi mitano mbele.

Akizungumzia kusua sua kwa ujenzi wa barabara hiyo Mkandarasi wa kampuni hiyo Nassor Kolowa, alisema moja ni kucheleweshewa kwa malipo na kuondoa udongo mwingi usiohitajika kwenye barabara hiyo.

Hata hivyo, Afisa Mdhamini wa wizara ya Ujenzi, Usafirishaji na Uchukuzi Pemba Ibrahim Saleh Juma, alisema hadi juzi, tayari kilomita 2.2 zimeshaweka lami moto.

Alieleza kuwa, zipo kilomita 7.3 nazo tayari zimeshawekea rojo ‘primer’ tayari kwa maandalizi ya uwekaji wa lami moto, ambapo zoezi hilo halitarajiwei kusita tena tokea lilipoanza wiki tatu zilizopita.

Barabara hiyo ya Chake chake -Wete yenye urefu wa kilomita 22, ujenzi wake unatarajiwa kugharimu shilingi bilioni 26.6, ambapo mkataba wa ujenzi ulisainiwa mwaka 2022 na ilitakiwa kukamilika Agosti 2024.

                      mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...