Skip to main content

'MADEO' AIBAKISHA WAWI STAR MSIMU WA LIGI UJAO


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

TIMU ya Wawi star, imejihakikishia kubakia ligi daraja la kwanza kanda ya Pemba msimu ujao, baada ya jana kuichakaza Azimio SC kwa mabao 3-2, kwenye mchezo uliopigwa uwanja wa Ngere ngere Jeshini, majira saa 10:30 jioni.

Kwa timu ya Wawi star, mchezo huo kwao ulikuwa na maana pana, ili wajihakikishie kubakia kwenye daraja hilo, hasa kwa vile mchezo unaofuata wataumana na Junguni anayesaka alama za lazima za kuongoza ligi hiyo.

Katika mchezo wa jana, ambao uliohudhuriwa na watazamaji wengi, ulianza kwa kasi, huku kila timu ikiangalia ulipo udhaifu wa mwenzake, ili aondoke na alama tatu muhimu.

Katika kuhalalisho hilo, Wawi star ilianza kuwafurahisha washabiki wake, mnamo dakika ya 15, pale mshambuliaji wao hatari Suleiman Seif ‘Madeo’ alipotikisa nyavu kwa bao la kwanza.

Lakini Azimio SC, kwa vile walishaazimia ushindi, walisawazisha bao hilo, mnamo dakika ya 34, kwa shuti la mbali lililopigwa na mlinzi wao Salum Kazumar, na kujaa wavuni.

Ingawa ‘Madeo’ wa Wawi star, aliwanyamazisha washabiki wa Azimio, baada ya mkwaju wake alioujaribu wa umabli mita kama 25, nao kufanikiwa kuja wavuni, kabla ya Azimio kuweka mambo sawa, kwa bao la pili, mnamo dakika 42 kwa shuti zito la mchezaji wao Ali Rashid.

Wanaume hao, walioonekana kukamiana, huku wakiacha shangwe na wakati mwingine manung’uniko kwa wapenzi na washabiki wao, walizimaliza dakika 45 za awali, wakitoka uwanjani wakiwa nguvu sawa.

Dakika 45 za mwsiho, ndizo zilizokuwa za kasi zaidi, huku Wawi Star wakizitaka alama tatu kama ilivyo hamu ya Azimio, ambao wako hatarini kuungana na timu sita zitakazoshuka daraja la kwanza kanda ya Pemba.

Dakika mbili kabla ya mchezo huo kumalizika, Suleiman Seif ‘Madeo’ ndie aliyeihakikishia alama tatu Wawi star, safari hii akiukwamisha mpira wavuni kwa mkwaju wa penalti, baada ya mlinzi wa Azimio, kuunawa mpira ndani ya eneo la hatari.

Hivyo mwamuzi wa mchezo huo Suleiman Khatib Kisauti, aliamuru adhabu kubwa, na ‘Madeo’ bila ya ajizi, aliipa alama tatu, na kujikusanyia alama 43 zinazowabakisha kwenye lgi hiyo.

Mchezo unaofuata wa Wawi Star, wataumana na Junguni United yenye alama 71 inayoongoza ligi, inayopuliwa kwa karibu na Tekeleza FC yenye alama 70, wote wakiwa na michezo sawa 31.

Timu inayoshika nafasi ya tatu ni Mwenge SC, yenye alama 65, wakati News stone town na Konde star zikiwa na alama sawa 46 kila mmoja.

Timu sita ambazo zinapigiwa mnada wa kushuka daraja la kwanza mwakani, ni Tibirinzi star FC yenye alama 21 kwa michezo 30, Dynamoo na Mkoroshoni United zina alama 25 kila mmoja.

Timu nyingine zinazojitarisha kushuka ni Kifumbi Kai FC na Mila FC zikiwa na alama 33, huku timu ya Yosso boys ikiwa na alama 33, juu ya Alazzar FC yenya alama 36.

                                     MWISHO  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan