Skip to main content

TAMAA YA MAHARI, MKAJA WA WAZEE WAKATISHA NDOTO ZA WATOTO WA KIKE MFIKIWA

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANAHARAKATI wa haki za watoto shehia ya Mfikiwa wilaya ya Chake chake, wamesema tamaa ya mahari na haki ya wazee (kilemba cha wazee), ni miongoni mwa sababu, zinazochangia watoto kukatishwa masomo kwa kuozwa waume mapema.

Walisema, baadhi ya wazazi wamekuwa wakikimbilia haki ya wazee na mahari, wakati mtoto wake anapotokezea muume, na hivyo kumkatisha masomo kwa tamaa hiyo.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kijijini hapo, walisema hiyo ni miongoni mwa sababu moja kubwa, ambayo sasa husababisha watoto, kukatishwa masomo.

Mratibu wa wanawake na watoto shehiani humo Kheriyangu Mohamed Ali, alisema pamoja na elimu wanayoitoa, lakini bado wapo wazazi wamekuwa wazito kubadilika.



Alieleza kuwa, na hasa pale inapotokezea kuna mtoto ni mtoro masomoni, ndipo hapo wazazi huchukua nafasi hiyo, kuwakatisha masomo.

‘’Hapa shehiani, wapo wazazi na walezi wamekuwa wakivutiwa mno na yale mahari na fedha za wazazi (kilemba cha wazee), hivyo huwa rahisi kuwaoza watoto wao,’’alieleza.

Kwa upande wake mazazi Masika Mohamed Ali, alikiri kuwepo kwa tamaa hiyo kwa baadhi ya wazazi, bila ya kujali athari yake, hapo baadae.

‘’Watoto wa kike hapa kijijini waliowengi wamekuwa wakivunjiwa ndoto zao, maana huolewa mapema na moja ya sababu ni utoro na wazazi kupenda fedha za mahari,’’alieleza.

Nae Mkubwa Ali Khatib alishauri jamii, kutowakatisha masomo watoto wao wa kike, na wawaache waendelee kutimiza ndoto zao za kielimu.


Sheha wa Mfikiwa Bimkubwa Rajab Tangwi, alisema wamekuwa wakali mno, pale wanapohisi kunaharakati za kufungwa ndoa ya mtoto shehiani mwake.

Alieleza kuwa, wamekuwa wakijitahidi kutoa elimu kwa jamii, ingawa wamekuwa wajanja na wakati mwingine kuzifungisha ndoa hizo nje ya shehia ya Mfikiwa.

‘’Ni kweli tamaa ya mahari imekuwa ikisababisha watoto wengine kukosa kuendelea na masomo, maana wazazi wingine hukimbia aibu ya mimba kabla ya ndoa,’’alifafanua.



Mratibu wa TAMWA-Pemba Fat-ya Mussa Said, alisema lazima jamii iweke mkazo wa kipekee, ili kuhakikisha watoto wa kike wanamaliza masomo ya lazima.

Kwa upande wake Mratibu wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, alisema moja ya changamoto iliyopo ni wazazi kutohudhuria mikutano ya wazi na kujifunza.

‘’Kupitia mikutano ya wazi, huelezwa athari za mtoto kumkatisha masomo na kisha kumuoza, akiwa bado viungo vyake havijakomaa, lakini hawahudhurii,’’alieleza.

Akizungumza hivi karibuni, Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, aliwatahadharisha masheha kutosogelea vikao vya sulhu, kwa kesi za udhalilishaji.

 Matukio ya ubakaji na ulawiti yanayowakumba wanawake na watoto kwa miezi ya February na Machi mwaka 2023/2024 yaonekana kupungua na kufikia 300, upungufu wa matukio 24 kwa mwaka jana.

Kulingana na takwimu zilizoripotiwa kutoka Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa serikali, inaonesha miezi hiyo Febuari na Machi mwaka uliopita, zinaonesha kuwa ndani ya siku 59 ya miezi hiyo miwili, kumeripotiwa matukio sita, kwa kila siku moja.

Taarifa zinaeleza matukio ni 624, yaliyoripotiwa kwa miezi minne kwa Zanzibar, na kuonesha wastani wa matukio 56 kuripotiwa kila wilaya, kati ya 11 za hapa Zanzibar.

                                  Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan