Skip to main content

'WORLD VEGETABLE CENTER ' ’ ZEEA WASUKA MPANGO KWA WAJASIRIAMALI

 

 NA ASHA ABDALLA, PEMBA@@@@

 

MRADI wa ‘world vegetable center’ kwa kushirikiana  na wakala wa uwezesha wananchi kiuchumi (ZEEA),  wameweka mpango mkakati wa kuwapa taaluma wajasiramali wadogo, kwa lengo la kuhakikisha wanapata soko la bidhaa zao ndani nan je ya Pemba.

 

Aliyasema hayo Mtaalamu wa kilimo cha mbogamboga Renatha Edgar, kutoka mradi huo,  kwenye kiwanda cha usindikaji cha wajasiriamali kilichoko Pujini Wilaya ya Chake chake, mara baada ya kukagua na kufanya tathmini, kwa wajasiriamali ambao wamepatiwa mafunzo ya kuzalisha na kusarifu mchicha lishe.

 

Alisema, lengo la kutoa taaluma kwa wajasiriamali hao ni kuweza kujipatia fursa mbali mbali, ambazo zitawaongezea thamani ya bidhaa zao, na kupata soko ambalo, litawaongezea kipato.

 


“Kwa sasa tumepiga hatua kwa kufanya mafunzo kwa wajasiriamali zaidi ya 200, ambao kati yao wameshaanza kufanya hii kazi, ya kuongeza thamani za bidhaa zao kwa kutengeneza unga wa mchicha lishe,’’alifafanuwa.

 

Hata hivyo, alitoa wito kwa jamii kuwa na mwamko wa kuutumia unga huo (wa mchicha lishe) ,ili kuimarisha afya zao, huku akiwaomba wajasiriamali hao kujitokeza kwa wingi kupata mafunzo  hayo ili yawasaidie katika kutengeneza bidhaa hizo.

 

Naye Kaimu Mratibu Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (ZEEA) Haji Mohamed Haji, alisema kuwa wajasiriamali hao, wamenufaika kupitia mafunzo hayo, na wamefikia hatua kubwa katika kuzalisha bidhaa hiyo na kuongeza pato lao.

 

Aidha aliwataka wajasiriamali hao kuyatumia mafunzo hayo, kwa kuzalisha bidhaa zilizobora ambazo zitaongeza thamani na ubora wa kuuzika.

 

Kwa upande wake Msimamizi wa wajasiriamali kutoka mradi wa ‘World Vegetable Center’ Nadra Suleiman Haji, alisema kuwa matumaini ya mafunzo hayo ni kuendelea kuwafikia wajasiriamali wengi zaidi, ili kufikisha taaluma ya kujikomboa kimaisha, inasambaa kwa walio wengi.

 



Naye mjasiriamali ambaye amenufaika na mafunzo kupitia mradi huo, Amina Adam Makame, alisema ameyapokea mafunzo hayo na ameshawajiisha watu wengine, ili kuzalisha mbegu za mchicha lishe, na kusarifu unga wenye virutubisho kadhaa.

 

Mradi wa ‘World Vegetable Center’ ukishirikiana na (ZEEA) chini ya ufadhili ‘USAID’ kupitia Mradi wa AID- I, kwa sasa unaendelea kuwapatia mafunzo wajasiamali ya kuendeleza biashara zao, jambo ambalo litaweza kuinuwa vipato vyao.

 

                                     MWISHO.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan