Skip to main content

WASIADIZI WA SHERIA, SHEHA WAWI WAFUMUA MIPANGO KUOZESHWA MWANAFUNZI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

UONGOZI wa shehia ya Wawi, wasaidizi wa sheria na askari wa shehia hiyo, wametiribua mpango unaosukwa na familia, ya kijiji cha Vikutani shehiani humo, wa kutaka kumuozesha mtoto wao, anaesoma darasa la saba, ambae anadaiwa kuwa na ujuzito.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka shehiani humo, iliyopatikana Juni 11, 2024 familia hiyo baada ya kupewa taarifa na wasamaria wema, juu ya mabadiliko ya mtoto wao, waliamua kumfikisha hospitali kumfanyia vipimo.

Ilielezwa kuwa, baada familia kugundua kuwa mtoto wao anaujauzito unaokisiwa wa miezi sita, waliamua kumfuatilia kijana anaesadikiwa kuwa amempa ujauzito huo, ili kumfungisha ndoa.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, sheha wa shehia ya Wawi Sharifa Waziri Abdalla, alisema baada ya kugundua mpango huo, sasa wameshaifuata familia hiyo, na kuitahadharisha juu ya uamuzi wao huo.

Alieleza kuwa, kwa sasa wamekuwa karibu mno kumfuatilia mtoto huyo, ili kuhakikisha kwanza anarejshwa skuli, kuendelea na masomo na kuona hafungishwi ndoa kabla ya wakati.

Alifahamisha kuwa, juzi Juni 6, 2024 aliiandikia familia hiyo barua, ili kukutana nayo na kuiekeleza namna ya kufungua lalamiko Polisi, ingawa ilishinwa kutii agizo hilo.

''Taarifa tulizinazo kwa sasa, wapo watu wakiwemo wa upande wa kijana wa kiume, wanasuka mipango ili kuhakikisha mtoto huyo anaolewa, ingawa tunapokea taarifa kila kinachoendelea,’’alieleza.

Sheha huyo alieleza kuwa, wamekuwa wakishirikiana kwa karibu kati yake na wasaidizi wa sheria na Askari wao shehia, ili kuona wanaifuatilia haki ya mtoto huyo.

Katika hatua nyingine, Msaidizi wa sheria wa shehia ya Wawi Fatma Hilali Salim, alisema hakuna namna ya kesi hiyo kuimaliza kienyeji, bali ni kwa wazazi kufungua lalamiko la ubakaji.

‘’Tumekuwa tukiwaelimisha wananchi kila siku, kwamba kesi za udhalilishaji hazitakiwi kumalizwa kienyeji, na ndio maana tunashirikiana na uongozi wa shehia, ili kulifikisha Polisi,’’alieleza.

Katib wa sheha wa shehia hiyo Sham Haroub Said, alisema awali aliwapelekea wito wazazi hao, ingawa walishindwa kutii agizo na badala yake walikimbilia kijiji jirani.

‘’Juzi tulipokwenda usiku, mama na mtoto wake ameshakimbilia kijiji jirani, ingawa tukilimkuta kaka na baba mzazi, na tuliwaarifu juu ya kufika Polisi na kutoa maelezo ya utuhma za ubakaji kwa mtoto wao,’’alieleza.

Baba mazazi wa mtoto huyo (jina limehifadhiwa), alisema hana taarifa zozote za mtoto wake kuwa ni mjamzito na anahudhuria masomo ya skuli na madarassa, kama kawaida.

Kaka wa mtoto huyo, anayesoma darasa la 12, alikiri kuwa mdogo wake ana miezi mitano sasa, hajahudhuria masomoni, ingawa hajaelezwa lolote juu ya tuhma hizo.

‘’Ni kweli mdogo wangu anayesoma darasa la saba kwenye moja skuli za Jimbo la Wawi, hahudhurii masomoni, sasa ni miezi mitano na nusu, lakini sijui kwamba amebakwa ama amejiuzia mwenyewe,’’alifafanua.

Baadahi ya wananchi wa kijiji cha Vikutani shehia ya Wawi, walisema, mtoto huyo amekatisha masomo kwa miezi mitano sasa, na familia inazotaarifa za uhakika, juu ya ujauzito wake.

Mwananchi huyo aliyekataa kutaja jina lake, alisema waliogundua mabadiliko ya afya yake, ni waalimu wake, na ndipo taarifa hiyo ikafikishwa kwa wazazi na kuamua kumfanyia vipimo.

Daktari aliyekataa kutaja jina lake wa hospitali binafsi ya Dira Machomanne Chake chake, aliyemfanyia uchunguuzi mtoto huyo, alisema amemgudua ana ujauzito wa miezi sita.

‘’Huyu kwa mwaka huu ni mwanafunzi tisa, kuja kuchunguuzwa na kubainika akiwa na ujauzito, ingawa wa mwisho alionekana na ujauzito wa miezi nane, bila ya familia kugundua,’’alieleza.

Mratibu wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba, Fat-hya Mussa Said, alisema bado jamii, imekuwa ikizifanyia sulhu kesi hizo, na kuviza mapambano ya kutokomeza udhalilishaji.

Mkurugenzi wa Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Nassor Bilali Ali, aliitaka familia hiyo haraka kukimbilia Polisi na kufungua shauri la ubakaji, na kuacha mpango wao wa ndoa.

Matukio ya ubakaji na ulawiti yanayowakumba wanawake na watoto kwa miezi ya February na Machi mwaka 2023/2024 yaonekana kupungua na kufikia 300, pungufu ya matukio 24 kwa mwaka jana.

Kulingana na takwimu zilizoripotiwa kutoka Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa serikali, inaonesha miezi hiyo Febuari na Machi mwaka uliopita, zinaonesha kuwa ndani ya siku 59 ya miezi hiyo miwili kumeripotiwa matukio sita, kwa kila siku moja.

Taarifa zinaeleza matukio ni 624, yaliyoripotiwa kwa miezi minne kwa Zanzibar, na kuonesha wastani wa matukio 56 kuripotiwa kila wilaya, kati ya 11 za hapa Zanzibar.

Mtoto huyo mwaka 2022, aliwahi kutuhumiwa kubakwa na kijana wa miaka 20 ambae ni jirani yake, na baada lalamiko hilo kufikishwa Polisi, akimbia hadi sasa hajarudi kwao.

Mwisho

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan