Skip to main content

WAZAZI CHANZO KUZIMA NDOTO ZA WASICHANA KUWA WANAMICHEZO

 



NA NIHIFADHI ABDULLA, ZANZIBAR@@@@

“SIKUJUA kinachoendela nilimuona tu baba kavimba nikamsalimia hakutikia vizuri mimi nikaingia ndani kukoga na mambo mengine”

 Amesimulia  Wafaa akiwa kwenye upenu wa Nyumba na kuwacha kumlisha mtoto kwa muda wa sekunde 5 huku akionesha    huzuni usoni mwake.

Jina lake halisi Wafaa Makame Hassan miaka 26 anakumbuka yaliyomtokea na namna alivyokatishwa ndoto za kuwa mwanamichezo miaka 12 iliyopita wakati anasoma skuli ya Muyuni iliyopo Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja.

Amesema alikuwa na ndoto za kuwa mchezaji mkubwa wa mpira wa Nyavu (Net Ball) na tayari alishaanza mashindano ya Skuli kwa skuli ya Elimu bila ya malipo.

Ameendelea kusema baada ya kupumzika alipata habari kutoka kwa Shangazi yake ambae kwa sasa ameshatangulia mbele ya haki  kwamba baba yake kapiga marufuku kwenda kwenye michezo kwa madai kufanyika  uhuni.

“Kuna mtu kampigia simu baba yako kuwa mnachanganyika na wanaume na kushikana hivyo amekasirika na lazima ukubaliane nae” alielezea Wafaa akimnukuu shangazi yake.

Wafaa amesema siku hiyo ilikuwa nzito kwake kwani hakutarajia kukutana na   hali hiyo na mwisho wa siku akukubaliana  mzazi wake na hivyo ndoto zake zikaishia hapo.

“Sikuwa na furaha nilikasirika sana nikaingia ndani karibia siku  nzima niliwanunia watu wote wa nyumbani lakini mwishowe nikawa sawa nitakasirika mpaka lini anabaki kuwa mzazi wangu tu na zile ndoto zikafikia tamati siku ile” 

Juma Hassan baba mdogo na mlezi wa Wafaa amesema ameamua kumkataza kushiriki michezo kutokana na lawama na maneno ya watu wengine kwa kuambiwa wanafanya uhuni.

“Najua kama lile jambo halikumfurahisha mwanangu lakini sifa ya mtoto wa kike ni kujiheshimu na kujilinda kwenye michezo yao ilo halikuwepo na ndio maana nikapewa salamu ili nimchunge na mimi sikuona vibaya kwani mtoto halelewi na mmoja,

“Wafaa ni mtoto wa marehemu kaka yangu aliniachia akiwa mdogo na kusisitiza nimlee kwa misingi mizuri angeharibika huko michezoni mm ningekuwa mgeni wa nani nikaona la maana asiende michozoni na sio yeye tu hata wanangu wengine wakike hatoenda  kule  hakuna maadili

Salama ali haji mama mzazi wa Wafaa amesema kiupande wake haoni tatizo mtoto wa kike kushiriki michezo kwani anaona wanawake mbalimbali ambao wameajiriwa kupitia sekta hiyo na wanaendesha Maisha yao bila tabu.

“Mimi sikusikilizwa na wala sikufurahi lakini mtoto akiwa ulezini mzazi huna kauli, dada ake alikuwa anashiriki michezo skuli kutwa hakai nyumbani na siku mzuia mpaka kachoka mwenyewe kwasababu sikuona tatizo kuna wanawake wangapi wameajiriwa kwa michezo hayo ndo maendeleo yenyewe” alimalizia Bi Salama.

 

Wafaa kwa sasa ni mke na mama wa watoto wawili amesema baada ya kusitishwa kushiriki michezo hata nguvu ya kusoma masomo mengine nayo ikayeyuka “baada ya hapo maendeleo yangu ya kusoma yakapungua na kusababisha kidato cha nne kufanya vibaya kwenye mtihani wangu wa Taifa  na hivyo nikaolewa na sasa nalea wanangu” alimalizia Wafaa huku akimnywesha mwanawe maji.

Taasisi ya wanawake kwenye  michezo nchini marekani (womens  sport  foundation inaonesha kwamba wasichana ambao wana umri wa miaka 14 huacha kuendelea na michezo ikiwa tofauti na wavulana wenye umri huohuo

 


Kwa hapa Zanzibar moja ya vikwazo hivyo ni wazazi kutowaruhusu watoto wao kwa madai ni kinyume na maadili silka na utamaduni

Kutokana  na changamoto hizo lukuki zilizopo   zinazomkwamisha mwanamkke na msichana kufikia ndoto  zake za kimichezo jitihada mbalimbali zinachukuliwa kuhakikisha linapatiwa ufumbuzi na kuona kiwango cha wanawake kwenye sekta hiyo kinaongezeka

 Afisa mradi wa kukuza  usawa wa kijinsia  na ujumuishi kwenye michezo  Khairat Haji  amesema  Chama cha  Waandishi wa habari Wanawake TAMWA Zanzibar kimeona haja ya kushirikiana Waandishi wa habari juu ya kuandika masuala ya michezo kwa wanawake na wasichana ili iwe rahisi kufikisha ujumbe kwa jamii kuondoa mifume dume ambayo ni vikwazo dhidi yao.

“Kwenye mradi huu tunafanyakazi na waandishi wao wanauwezo wa kuibua changamoto, vikwazo lakini pia kuonesha wale wanawake waliofanikiwa kwenye michezo ambao watakuwa kielelezo kwenye jamii na mfano bora wa kuigwa

 Mradi huo unatekelezwa na  shirika la maendeleo la ujerumani GIZ,  Chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA ZANZIBAR   kwa kushirikiana na Jumuiya ya wanasheria wanawake Zanzibar ZAFELA na  kituo  cha majadiliano kwa Vijana (CYD)  lengo ikiwa ni kuipa elimu jamii ya kuwaunga mkono wanawake katika kushiriki michezo kwa maendeleo.  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan