Skip to main content

MDHAMINI FEDHA PEMBA: USIMAMIZI MALI ZA UMMA KUFIKIA MALENGO YA SERIKALI’

 

 

NA HASINA KHAMIS, OUT- PEMBA@@@@

AFISA Mdhamini wa Wizara ya Fedha na Mipango Pemba Abdull-wahbi Said Abuu-bakar, amesema usimamizi bora wa mali za umma itasadia kwa serikali, kufikia malengo yaliyokusudia.

 

Aliyasema hayo leo Juni 6, 2024 katika kikao cha kupokea maoni ya wadau, kwa muongozo wa uondoaji wa mali za umma na usimamizi, udhibiti wa matumizi ya vyombo vya moto vya serikali, ukumbi wa wizara hiyo Gombani Chake chake Pemba.

 


Alisema changamoto zilizopo katika wizara, taasisi za umma na mashirika, ni kushidwa kusimamia kutunza na kutumia vyema mali za umma kama sheria inavyotaka.

 

"Hatufanyi vyema katika kusimamia mali za umma, ambapo inasababisha kushidwa kufikia lengo la mali hizo, jambo ambalo sio sahihi,’’alieleza Afisa Mdhamini huyo.

 

Aidha aliwataka washiriki hao kutoka mashirika ya umma na taasisi za serikali, kutoa ushirikiano na ofisi ya usajili wa hazina, pamoja na kutumia fursa hiyo kwa kutoa elimu na maoni kwa jamii.

 


Nae Msajili wa Hazina Zanzibar, Wahdi Mohamed Ibrahim, alisema sheria nambari 6 ya mwaka 2021 ya usajili wa hazina, imewataka kutoa muongoza kama inavyoelekeza.

 

Alisema, upo umuhimu kwa sasa mambo ya serikali kuwa wazi kwa yale yanayostahiki, ili umma ufahamu utaratibu wa jinsi mali ya umma inavyoingia mpaka inapotoka.

 




"Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, inatumia fedha nyingi kwenye manunuzi kutumia muongozo wa usimamizi na udhibiti wa matumizi ya vyombo vya moto, na uondoaji wa mali za umma utaweza kupunguza gharama hizo na utitiri wa mali chakavu," alifafanua.

 

Kwa upande wa washiriki, akiwemo Amina Ali Mohamed, Afisa kutoka Wizara ya Kilimo, Maliasili na Mifugo, alisema rasimu hiyo ya muongozo wa uondoaji wa Mali za umma, ni jambo muhimu ambapo serikali ameamua kulifanya kupitia ofisi ya usajili wa hazina.

 

‘’Awali kila ofisi ilikuwa na utaratibu wao, lakini kupitia muongozo huu utaweza kudhibiti katika ngazi ya utumiaji, utunzaji mali na iwapo itakuwa chakavu, pia utaratibu utakuwemo na ikibidi kuuzwa basi pato la serikali litapatikana,’’alieleza.

 

Nae Said Shaame Bakari, kutoka Wizara ya Biashara, alisema mafunzo hayo yataweza kusaidia kupata uelewa wa pamoja, kwa taasisi zote na kufuata mfumo mmoja.

 



Kikao hicho cha siku moja, chenye moja ya lengo la kupunguza changamoto katika usimamizi wa mali za umma, ambapo miongozo miwili  imetolewa, na kuwasilishwa na kusubiri kupokea maoni ya wadua.

 

                            MWISHO 

 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan