Skip to main content

WAMBAA, CHUMBAGENI KUANZISHA MFUKO WA UCHINJAJI

 



 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WAUMINI wa dini ya kiislamu shehi za Wambaa na Chumbageni wilaya ya Mkoani Pemba, wamekutana na kukubaliana kuanzisha mfuko maalum wa uchinjaji, kila ifikapo mfunguo tatu, kwa ajili ya sadaka kwa wasiokua na uwezo.

Kwenye kikao hicho, kilichofanyika skuli ya Wambaa, waumini hao walisema, imeonekana kuna kundi kubwa kubwa la waumini wenzao, wamekuwa kikosa kitoweleo kwa siku za sikukuu, jambo ambalo sio sahihi.

Akizungumza Mwenyekiti wa muda wa mfuko huo Ali Abdi Mohamed, jana Juni 22, 2024  alisema wamekusudia kuwa mfuko huo uwasaidie, wale ambao uwezo wao uko chini.

Alieleza kuwa, mpango huo wa uchinjaji kila ifikapo mfunguo tatu, kwa hatua za awali utahusisha kila watu saba, kutakiwa kumiliki Ng’ombe mmoja na kumuwasilisha kwa kamati, kwa ajili ya uchinjaji.

Mwenyekiti huyo alisema, kisha baada ya kukamilisha taratibu za uchinjaji, kutagawiwa mafungu matatu, kama sheria ya dini ya kiislamu ilivyoelekeza, ambapo fungu moja hutolewa kwa wasiokuwa na uwezo.

‘’Kamati hii inaskusudia hasa kuwahamasisha wanawambaa na Chumbageni popote walipo, waungane na sisi katika kukusanya Ng’ombe wengi zaidi, na kuchinja kwa pamoja, ili kila mmoja apate kitoweleo siku ikifika,’’alieleza.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo huo wa muda, alisema kuanzia sasa, kila muumini wa dini ya kiislamu anayetaka kuungana na mfuko huo, awasilishe jina lake mapema.

Kwa upande wake Katibu wa muda wa mfuko Mwalimu Ali Ussi, alisema kwa kuanzia mwaka jana, walichinja Ng’ombe watatu, kwa mpango wa kushirikiana.

‘’Mahitaji yameonakana makubwa, maana kila mmoja alikuwa anahitaji kitoweleo, na ndio maana sasa tunatoa taarifa mapema, kuelekea mwakani, ili tukusanyika tuwe wengi,’’alieleza.

Sheha wa shehia ya Chumbageni Mgeni Othman, alisema wazo hilo ni zuri na ni jema mno, maana litaongeza umoja na mshikamano wao.



‘’Suala la kuanzisha mfuko wa uchinjaji, kwa lengo la kupata Ng’ombe wengi zaidi hapo mwakani ni jambo jema, maana ni kweli wapo wasiokuwa na uwezo, hula hadi dagaa siku ya sikukuu,’’alieleza.

Mjumbe wa mfuko huo Mohamed Juma Khamis, alisema ni vyema jamii ya kiislamu kushajiishana, ili mwakani walau wapatikane Ng’ombe 20, ili kila mmoja apate nyama siku ya sikukuu.

Kwa upande wake mjumbe Hadia Ramadhan, alisema changamoto aliyoiona kwa msimu uliomalizika, ni kujitokeza kwa watu wengi wenye hali ngumu, wanaohitaji kusaidiwa.

Akizungumzia umuhimu wa kuchinja kwa ajili ya Allah, sheikh Abdi Salim Khamis, alisema kila unyoya mmoja ya mnyama aliyechinjwa, wahusika wanaandikiwa thawabu.

‘’Haipendezi kuona siku ya sikukuu, wengine wanakula nyama na wengine wanakula dagaa, kwa sababu ya kukosa sadaka, lazima hili waumini wa Wambaa na Chumbageni tulifikirie,’’alifafanua.

Wakichangia kwenye mkutano huo, mshiriki Juma Abassi Ali, aliitaka kamati hiyo, kujipanga kutafuta Ng’ombe mapema, ili kuepuha kupanda bei, hapo baadae.

Nao washiriki Juma Ali Pandu, Juma Abdalla Jonga, Amini Haji Makame na Khamis Khatib Khamis, walitaka mfuko huo, uwe wa kudumu hapo baadae.

Akifunga kikao hicho, mjumbe wa mfuko huo Mohamed Abdi Mohamed, alisema kuanzia mwakani, watahakikisha hakuna muumini wa dini ya kiislamu ndani ya shehia za Wambaa na Chumbageni, atakaekosa kitoweleo.




Alifafanua kuwa, hilo litawezekana iwapo watajitokeza wadau wengi zaidi kuunga nguvu kupitia mfuko huo, au wafadhili wengine mbali mbali.

Mfuko huo wa uchinjaji wa shehia za Wambaa na Chumbageni wilaya ya Mkoani, kwa mwaka jana ulichinja Ng’ombe watatu na wastani wa waumini 56, walisambaaziwa sadaka hiyo, kati yao 14 ndio waliokuwa wagawaji.

                            Mwisho  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan