Skip to main content

UWANDANI CHAKE CHAKE WAKUMBUSHWA KUTOZITIA MKONO KESI ZA JINAI

 


 NA MWANDISHI WETU, PEMBA@@@@

WANANCHI wa shehia ya Uwandani wilaya ya Chake chake Pemba, wamekumbushwa kujitenga mbali na sulhu za kesi za jiani, ikiwemo za udhalilishaji, kwani kufanya hivyo, ni kuyapalilia matukio hayo.

Hayo yameelezwa leo Juni 25, 2024 na Mkuu wa Divisheni ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar ofisi ya Pemba, Bakar Ali Omar, kwenye hutuba iliyosomwa kwa niaba yake na Msaidizi wa sheria wa Jimbo la Wawi Haji Nassor, kwenye mkutano wa wazi, kwa wananchi waliomo ndani ya mpango wa kanusuru kaya maskini, ikiwa ni sehemu ya wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar.

Alisema, bado wapo baadhi ya wazazi, wamekuwa wakizikalia mkekani kesi hizo, kwa kuzifanyia sulhu, jambo ambalo kisheria ni kosa na kuongeza kichocheo kwa watendaji.



‘’Niwasihi sana wananchi wa Uwandani, tukiwa ndani ya wiki ya msaada wa kisheria, jambo hilo mliepuke na ikitokezea mkimbile mbele ya vyombo vya sheria,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, aliwataka wananchi hao, kuwatumia wasaidizi wa sheria waliomo ndani ya shehia yao, pale wanapokuwa na changamoto za kisheria.

Aidha aliwaeleza wananchi hao kuwa, moja ya jukumu la msingi kwa wasaidizi hao wa sheria, ni kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria kwa wananchi maskini bila ya malipo.

Hata hivyo, aliipongeza taasisi ya LFS, kwa kuendelea kufanyakazi na Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria, kupitia mradi wa upatikanaji haki.

Akizungumza kwenye mkutano huo, Sheha wa Uwandani wilayani humo, Ali Mussa Hamad alisema wazo la Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria pamoja na Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’ kufika shehiani humo, ni jema.



Alieleza kuwa, anajua zipo shehia 32 wilayani humo, hivyo wamethamini shehia ya Uwandani kuteuliwa na kupewa elimu ya kisheria.

Mapema Mwakilishi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania TASAF shehiani humo Khamis Seif Faki, alisema wazo la serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuuleta mfuko huo, umewakomboa walio wengi.

Aidha aliwakumbusha walengwa hao, kuendelea kujiwekea akiba kupitia vikundi mbali mbali vya ushirika, ili wakati watakapotoka ndani ya mpango huo, wasiwe tegemezi kwa familia zao.



Baadhi ya wananchi wa Uwandani akiwemo Khadija Abdalla Khamis, aliipongeza Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria pamoja na ‘CHAPO’ kuwafikishia elimu ya kisheria.

Kwa upande wake Saada Ali Khamis, alisema moja ya changamoto ndani ya ‘TASAF’ ni kuchelewa kwa malipo yao na wakati mwingine. kupungua kwa ruzuku.



Mwananchi Kombo Ali Abdalla ‘Mbunge’ aliwakumbusha wasaidizi wa sheria, kuendelea kuwasaidia wanawake wanaodhulumiwa mirathi, ardhi na migogoro ya ndoa.

Nae Anithun Ali Abdalla, alisema changamoto anayoiona ni wanawake walio wengi, wamekuwa na uwelewa hafifu wa sheria za nchi, na kusababisha kukosa haki zao.

Shehia ya Uwandani wilaya ya Chake chake, inao wakaazi 3,767 waliomo vijiji vya Gongoni, Pande, Mibungoni, Mkwajuni, Kwa joto, Kimbuni, Mperani na Mkaani ambapo kati yao 378 wamo katika mpango wa kupewa ruzuku na TASAF.

Wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar ilizinduliwa Juni 24, 2024 na Waziri wa Nchi Afisi, Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Zanzibar Haroun Ali Suleiman.

Ambapo shughuli nyingine zinazoendelea kwa Pemba, ni mikutano ya shehia za Micheweni na Uwandani kwa kuzungumza na walengwa wa mpango wa kunusuru kaya maskini na kongamano la wanafunzi wanaosomea uwalimu SUZA Mchanga mdogo.

Hii ni wiki ya tano wa Msaada wa Kisheria Zanzibar, ambapo ujumbe wa mwaka huu ni ‘tumia teknologia kurahisisha upatikanaji wa haki'  na mgeni rasmi wa kilele hicho anatarajiwa kuwa Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi.

                                Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan